picha

Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones

Post hii inahusu dawa ya kupambana na bakteria, hili kundi la fluoroquinolones lina dawa kuu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin.

Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones .

1. Hii ni mojawapo ya dawa za kupambana dhidi ya maambukizi ya bakteria dawa hii kama tulivyoona hapo mwanzoni Ina dawa muhimu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin na kundi hili pamoja na kutibu magonjwa mengine ni maarufu katika matibabu ya maambukizi kwenye mfumo wa hewa, maambukizi kwenye ngozi ambayo uambatana na viupele pamoja na miwasho, maambukizi ya kaswende na kisonono au kwa lugha ya kitaamu huiitwa sexual transmission diseases and sexual transmission infection.

 

2. Dawa hizi ufanya kazi mwili kwa kuharibu kabisa kazi ya bakteria kwa kuingilia DNA ya bakteria na kuzuia bakteria kuendelea kuzaliana hatimaye kufa, dawa hizi kwa kawaida utumiwa kwenye mdomo kama vidonge na pia uweza kuingia kwenye mmengenyo wa chakula na kuelekea kwenye mzunguko wa damu ambapo usambaza sehemu mbalimbali kama vile kwenye sehemu zozote za mwili zenye maambukizi na kuharibu kabisa kazi ya bakteria kwa kuingilia DNA ya bakteria.

 

3. Pamoja na magonjwa ambayo utibiwa na dawa hizi Kuna magonjwa mengine kama hays kuharisha na kutapika, maambukizi kwenye kibofu cha mkojo, kwenye joint na kweye magoti, kwenye tumbo na pia maambukizi kwenye via nya uzazi kama Kuna bakteria ameshambulia huko.

 

4. Ambao hawapaswi kutumia dawa hii ni wale wenye aleji na dawa hii pamoja na watoto chini ya miaka kumi na minane pamoja na wanawake wenye mimba.pia utumika kwa uangalizi kwa wenye magonjwa ya Figo na inii.

 

5. Maudhi madogo madogo ya dawa hii ni pamoja na kizunguzungu, maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika, kuharibu na pengine kupandisha sukari.

 

6. Kwa hiyo dawa hii haiitumiki kiholela mpaka kuwepo kwa maagizo ya wataalamu wa afya kwa sababu dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kuleta shida ikiwa mgonjwa yupo nyumbani ila kama yupo hospital ni rahisi kumpatia huduma ya kwanza.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2196

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 web hosting     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 ai web app     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.

Soma Zaidi...
Dawa ya penicillin ambayo uzuia asidi ya bakteria.

Post hii inahusu zaidi dawa ya phenoxy-methyl penicillin ambayo upambana na aina ya bakteria ambao utoa sumu Ili kuzuia dawa isifanye kazi.

Soma Zaidi...
Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)

Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin,

Soma Zaidi...
Dawa ipi ya manjano kwa mtoto mwenye umri miaka miwili?

Ugonjwa wa manjano ni moja kati ya maradhibyanayosumbuwa ini. Ugonjwa huu unahitaji uangalizi wa haraka hospitali. Posti hii itakwenda kukujuza ninivufanyebendapobmtoto wako ana ugonjwa wa manjano.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu minyoo

Zijuwe aina za minyoo na tiba yake. Dawa 5 za kutibu minyoo ya aina zote

Soma Zaidi...
Vyakula vya wanga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya wanga

Soma Zaidi...