picha

Dapsone na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi dawa ya Dapsone na kazi zake, hii ni dawa ambayo utumika katika kutibu ugonjwa wa ukimwi, dawa hii ufanya kazi kwa mchanganyiko wa dawa nyingine kama vile Rifampicin na clofaximine.

Dapsone na kazi zake.

1.Ni mojawapo ya dawa inayotumika kutibu maambukizi kwenye ngozi ikiwemo na ukoma kama tulivyoona hapo juu kuwa dawa hii haitibu ugonjwa huu peke yake na huwa na mchanganyiko na dawa nyingine, dawa hii ufanya kazi kwa kufubaza bakteria ambao usababisha ukoma na hatimaye wadudu uishiwa nguvu na kutoweka kabisa.

 

2.Katika matumizi ya Dawa hii pamoja na dawa ambazo uambatana nazo yaani utolewa kwa vipindi viwili muhimu  ambavyo ni miezi sita na miezi kumi na miwili katika miezi kumi na miwili mgonjwa utumia mchanganyiko wa Rifampicin, Dapsone na clofazimine na wakati wa kipindi cha miezi sita mgonjwa utumia Rifampicin na Dapson, mchanganyiko huo utolewa ili kuwezesha uponyaji kwa wagonjwa wa ukoma 

 

3.Pia  katika matumizi ya dawa hizi ya Dapson kuna maudhi madogo madogo ambayo uweza kutokea kama vile kutapika, kichefuchefu, kuharisha, maumivu ya kichwa, mapigo ya moyo kubadilika, kusinzia sinzia,kuchanganyikiwa kwa mgonjwa kwa hiyo katika matumizi ya dawa hizi mgonjwa anapaswa kuwa katika uangalizi wa karibu zaidi ili pakitokea maudhi yanazidi aweze kupewa msaada wa matibabu.

 

4.Katika matumizi ya dawa hii kuna wale ambao wanapaswa kutumia dawa hizi kwa uangalizi kwa mfano hii dawa usababisha mapigo ya moyo kubadilika kwa hiyo wenye Magonjwa ya moyo wanapaswa kutumia kwa uangalifu zaidi,na kwa wale wenye matatizo ya kuishiwa damu wanapaswa kutibu kwanza kuishiwa damu na hatimaye kutumia dawa hizi.

 

5.Kw hiyo tunajua kubwa Ugonjwa wa ukoma upo na kadiri Watu wanavyotumia dawa unazidi kupungua kwa hiyo tunapaswa kuwaleta wagonjwa wa ukoma hospitalini ili wapewe dawa kwa maana ugonjwa huu unatibika na tuache kuwanyanyapaa wagonjwa wa ukoma ila tuwapeleke wapate tiba sio kuwafukuza majumbani mwetu na kuwatenga wakashinda wanaomba omba ili kupata mahitaji kwa hiyo jamii inapaswa kupewa elimu ya kutosha kuhusu tiba ya ugonjwa huu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2816

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 web hosting     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea.

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...
Dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo.

Posti hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo, ni Aina mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu Minyoo inayosababishwa na bakteria mbalimbali.

Soma Zaidi...
Dawa ya Isoniazid na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi dawa ya lsoniazid nA kazi zake, ni dawa ambayo inasaidia kutibu kifua kikuu kati ya madawa yaliyoteuliwa na kuwa na sifa ya kutibu kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa

Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa

Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.

Soma Zaidi...