Menu



Ijue dawa ya kutibu ugonjwa wa ukoma

Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu ukoma,na dawa hiyo ni dawa ya Dapsoni, hii dawa usaidia kuzuia nerve zisiendelee kupoteza kazi yake pia na ngozi iendelee kuwa kawaida

Ijue dawa ya kutibu ugonjwa wa ukoma .

1. Ukoma ni mojawapo ya ugonjwa ambao uharibu nerve na mfumo mzima wa fahamu ambapo mgonjwa mara nyingi ushindwa kuhisi vitu vya hatari kama moto kwa sababu ya kuharibika kwa mfumo wa fahamu, pia na viungo kama vidole uweza kukatika yeye bila kuwa na taarifa yoyote Ile hali ambayo upelekea na ngozi ya mwili kutonawili ,kwa hiyo hata jamii uwatenga wagonjwa hawa, kwa matumizi ya dawa ya dapsoni utibu uaribifu wa nerve na kuzuia uaribifu wa ngozi na kumweka mgonjwa kwenye hali nzuri na akakubarika katika jamii.

 

2. Dawa hii kwa kawaida IPO kwenye mfumo wa vidonge na utumiwa kila kila siku kwa kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, matibabu ya ugonjwa huu dawa uanza kutumika kidogo kidogo na baadae dozi uongezeka kuanzia mwezi wa kwanza mpaka wa pili, na matibabu yake ni marefu kidogo kwa sababu utumia takribani miezi kumi na minane na matibabu yanaweza kuendelea kwa kutegemea hali ya mgonjwa kwa sababu kuna wagonjwa ambao uanza matibabu mwanzoni mara tu wanapoona dalili Ila Kuna wale wanaoanza kwa kuchelewa na Kuna wale wanaofuatwa kutoka majumbani kwao kwa kulazimishwa Ili kuzuia kuendelea kuongezeka kwa ugonjwa.

 

3. Kwa sababu tofauti tofauti na matibabu utofautiana kwa sababu Kuna wanaopenda kupona haraka, Kuna ambao hawajali na Kuna wanaolazimishwa kutumia dawa, kwa hiyo kupona utegemea bidii ya mgonjwa kuanza matibabu na uaminifu katika matumizi ya dawa, dawa hii ikitumiwa uweza kukaa mwilini kuanzia masaa mawili mpaka masaa nane baada ya kuitumia, kwa hiyo ikitumiwa tu uenda kufanya kazi kwenye ngozi,nyama za mwili kwa kitaamu muscle na pia dawa hii inaenda kwenye ini na kweye Figo ambapo inawezekana kukaa kwa mda wa wiki tatu hivi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kunywa sana maji Ili kuweza kuondoa sumu ya dawa inayokaa kwenye ini na Figo.

 

4. Dawa hii inatumika na watu wenye ukoma na pia wale ambao Wana dalili za ukoma na haujajitikeza kwa kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya na pia watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii ni wale wenye aleji na dapson drug na pia wale ambao maudhi madogo madogo yamekuwa mengi kiasi cha kwamba hawezi kuendelea kutumia dawa hii.

 

5. Pia katika matumizi dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile kichefuchefu na kutapika, kuharisha mapigo ya moyo kwenda mbio, maumivu ya kichwa, mwili kukosa nguvu kukosa hamu ya kula,ikiwa maudhi haya yameongezeka zaidi ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na pia maudhi madogo madogo kwa wagonjwa wa ukoma ni makubwa kidogo kwa hiyo jamii inapaswa kuwa karibu na wagonjwa hawa kuepuka tabia mbaya ya kuwanyanyapaa na kuona  kwamba sio binadamu , wanapaswa kutunzwa vizuri kwa sababu dawa wanazozitumia ni kali.

 

6. Pia kwa wale walio na matatizo ya moyo na presha wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa Ili kuweza kupata ushauri zaidi na pia dawa hizi hazitolewi kiholela holela Bali ni kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1675

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Matumizi ya dawa ya vidonda vya tumbo

Posti hii inahusu zaidi matumizi ya dawa za vidonda vya tumbo, ili kuweza kutumia dawa hizi ni vizuri kabisa kufuata mashariti kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa

Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya kaoline

Post hii inahusu dawa ya kaoline katika kutibu au kuzuia kuharisha ni dawa ambayo imependekezwa kutumiwa hasa kwa wale walioshindwa kutumia dawa ya loperamide.

Soma Zaidi...
Fahamu kazi za homoni katika kupamba na kansa.

Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa.

Soma Zaidi...
Njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake

Posti hii inahusu zaidi njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake, hii njia dawa umengenywa kwenye tumbo na kupitia kwenye utumbo mdogo na baadae kwenye damu,

Soma Zaidi...
Dawa ya maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukuletea dawa ya maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mucolytic dawa ya kutibu kikohozi

Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.

Soma Zaidi...
Faida za dawa za NMN

Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile.

Soma Zaidi...
Fahamau madhara ya flagyl (Metronidazole)

Flagyl ni nini? Flagyl (metronidazole) ni antibiotic. Inapigana na bakteria katika mwili wako. Flagyl hutumiwa kutibu maambukizo ya bakteria ya uke, tumbo, ngozi, viungo na njia ya upumuaji.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutibu mafua

Post hii inahusu dawa za kutibu mafua ambazo ni cough seppessants na nasal congestion ni dawa ambazo zimependekezwa kwa ajili ya kutibu mafua.

Soma Zaidi...