Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu ukoma,na dawa hiyo ni dawa ya Dapsoni, hii dawa usaidia kuzuia nerve zisiendelee kupoteza kazi yake pia na ngozi iendelee kuwa kawaida
1. Ukoma ni mojawapo ya ugonjwa ambao uharibu nerve na mfumo mzima wa fahamu ambapo mgonjwa mara nyingi ushindwa kuhisi vitu vya hatari kama moto kwa sababu ya kuharibika kwa mfumo wa fahamu, pia na viungo kama vidole uweza kukatika yeye bila kuwa na taarifa yoyote Ile hali ambayo upelekea na ngozi ya mwili kutonawili ,kwa hiyo hata jamii uwatenga wagonjwa hawa, kwa matumizi ya dawa ya dapsoni utibu uaribifu wa nerve na kuzuia uaribifu wa ngozi na kumweka mgonjwa kwenye hali nzuri na akakubarika katika jamii.
2. Dawa hii kwa kawaida IPO kwenye mfumo wa vidonge na utumiwa kila kila siku kwa kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, matibabu ya ugonjwa huu dawa uanza kutumika kidogo kidogo na baadae dozi uongezeka kuanzia mwezi wa kwanza mpaka wa pili, na matibabu yake ni marefu kidogo kwa sababu utumia takribani miezi kumi na minane na matibabu yanaweza kuendelea kwa kutegemea hali ya mgonjwa kwa sababu kuna wagonjwa ambao uanza matibabu mwanzoni mara tu wanapoona dalili Ila Kuna wale wanaoanza kwa kuchelewa na Kuna wale wanaofuatwa kutoka majumbani kwao kwa kulazimishwa Ili kuzuia kuendelea kuongezeka kwa ugonjwa.
3. Kwa sababu tofauti tofauti na matibabu utofautiana kwa sababu Kuna wanaopenda kupona haraka, Kuna ambao hawajali na Kuna wanaolazimishwa kutumia dawa, kwa hiyo kupona utegemea bidii ya mgonjwa kuanza matibabu na uaminifu katika matumizi ya dawa, dawa hii ikitumiwa uweza kukaa mwilini kuanzia masaa mawili mpaka masaa nane baada ya kuitumia, kwa hiyo ikitumiwa tu uenda kufanya kazi kwenye ngozi,nyama za mwili kwa kitaamu muscle na pia dawa hii inaenda kwenye ini na kweye Figo ambapo inawezekana kukaa kwa mda wa wiki tatu hivi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kunywa sana maji Ili kuweza kuondoa sumu ya dawa inayokaa kwenye ini na Figo.
4. Dawa hii inatumika na watu wenye ukoma na pia wale ambao Wana dalili za ukoma na haujajitikeza kwa kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya na pia watu ambao hawapaswi kutumia dawa hii ni wale wenye aleji na dapson drug na pia wale ambao maudhi madogo madogo yamekuwa mengi kiasi cha kwamba hawezi kuendelea kutumia dawa hii.
5. Pia katika matumizi dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile kichefuchefu na kutapika, kuharisha mapigo ya moyo kwenda mbio, maumivu ya kichwa, mwili kukosa nguvu kukosa hamu ya kula,ikiwa maudhi haya yameongezeka zaidi ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na pia maudhi madogo madogo kwa wagonjwa wa ukoma ni makubwa kidogo kwa hiyo jamii inapaswa kuwa karibu na wagonjwa hawa kuepuka tabia mbaya ya kuwanyanyapaa na kuona kwamba sio binadamu , wanapaswa kutunzwa vizuri kwa sababu dawa wanazozitumia ni kali.
6. Pia kwa wale walio na matatizo ya moyo na presha wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa Ili kuweza kupata ushauri zaidi na pia dawa hizi hazitolewi kiholela holela Bali ni kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa zinazofanya kazi ya kupunguza maumivu kwa kawaida dawa hizi ufanya kazi kwa kupitia kwenye mfumo wa fahamu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya phenoxy-methyl penicillin ambayo upambana na aina ya bakteria ambao utoa sumu Ili kuzuia dawa isifanye kazi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ibuprofen katika kutuliza maumivu, ni aina mojawapo ya dawa na yenyewe ufanya kazi kama aspirin na paracetamol
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.
Soma Zaidi...Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulik
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...