Uharamu wa Riba katika Uislamu
Kwanza, Uislamu umeharamisha riba kwa sababu ni dhulma (unyonyaji).Ukichukua mkopo wa riba uliochukuliwa kwa madhumuni ya kukidhi haja ya matumizi ya lazima ya nyumbani, utozaji wa riba unakiuka lengo la Allah la kuumba (kuleta) mali kwa wanadamu. Utaratibu aliouweka Allah ni kwamba kwa kuwa mali ameileta kwa wanaadamu wote:
“Yeye (Allah) Ndiye aliyekuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi...” (2:29).
Ni lazima matajiri (wenye mali) wawapatie wanyonge na wenye dhiki mahitaji yao muhimu ya maisha.
Pili, riba imeharamishwa katika Uislamu kwa sababu inahamisha mali kutoka kwa maskini au wanyonge na kuipeleka kwa tajiri ambayo huzidi kuondoa usawa katika mgawanyo wa mali. Hii ni kinyume na mahitaji ya jamii. Uislamu unataka kila mtu apate mahitaji muhimu ya maisha. Hivyo wale walio na ziada ya mahitaji muhimu ya maisha wanatakiwa wawape wasionacho kabisa au wale waliopungukiwa kwa upendo na udugu. Riba inakanusha kabisa msimamo huu.
Tatu, riba imeharamishwa katika Uislamu kwa sababu hufanya kundi la watu katika jamii liishi kivivu bila ya kufanya shughuli yoyote ya uzalishaji, likitegemea kuishi kwa riba kutokana na mali zao walizozikusanya katika mabenki, bima, na vyombo vingine vya riba. Jamii inakosa mchango wa watu hawa katika uzalishaji na si hivyo tu, bali watu hawa wanakuwa mzigo na bughudha katika jamii. Ufasiki (uharibifu) wa aina zote katika ardhi hufanywa na kundi hili.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 475
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani
👉2 kitabu cha Simulizi
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 Kitau cha Fiqh
Namna ya kuswali
2. Soma Zaidi...
nyakati za swala
3. Soma Zaidi...
Kumuandaa maiti kabla ya kufa na baada ya kufa, mambo muhimu anayopasa kufanyiwa maiti wa kiislamu
3. Soma Zaidi...
Hukumu na sherei zinazohusu ajira na kazi katika uislamu
Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada. Soma Zaidi...
Nini maana ya riba, na yapi madhara yake?
8. Soma Zaidi...
Nguzo za swala.
Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali. Soma Zaidi...
Njia haramu za uchumi.
Njia hizi ni haramu katika kukuza uchumi wako. Soma Zaidi...
Historia ya adhana na Iqama na jinsi ya kuadhini.
Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu. Soma Zaidi...
Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...
Maana ya uadilifu na usawa na tofauti zao
Posti hii itakwenda kukufunza utofauti kati ya uadilifu na usawa Soma Zaidi...
Mifumo ya benki ya kiislamu.
Hapa utajifunza njia ambazo nenk ya kiislamu hutumia ili kujiendesha Soma Zaidi...