image

Nini maana ya riba, na yapi madhara yake?

8.

Nini maana ya riba, na yapi madhara yake?

8. Tatizo la Riba
Riba ni kupata chochote kile cha ziada kutoka katika mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara. Mwenyezi Mungu anatufahamisha katika Qur’an:



Wale wanaokula riba hawasimami ila kama anavyosimama yule ambaye shetani kamzuga kwa kumsawaa; haya ni kwa sababu wamesema, Biashara ni kama riba, hali Mwenyezi Mungu amehalalisha biashara na kuiharamisha riba.(2:275)


Mwenyezi Mungu huyafutia (baraka mali ya) riba; na kuyatia baraka (mali iliyotolewa) sadaka (2:2 76).
Madhara ya riba katika jamii



(i)Riba inachafua nafsi ya Tajiri na uchumi wake. Tajiri ambaye hayuko tayari kukukopesha mali yake pasi na riba, kamwe hawezi kutoa mali yake bure kuwasaidia wanyonge na wenye dhiki. Tajiri asiye tayari kutoa mali yake kuwasaidia wenziwe wenye dhiki na shida katika jamii huwa mchoyo, bahili, mpupiaji mali, asiyetosheka na utajiri alionao, mfujaji, muonevu na dhalimu. Tajiri mwenye moyo wa namna hii hata kama atajiita Muislamu hawezi kamwe kuchunga mipaka ya halali na haramu katika kuchuma!



(ii)Riba inamkandamiza Mnyonge mwenye dhiki. Wanyonge na wenye dhiki katika jamii inayoendesha uchumi wake katika misingi ya riba, hawapati msaada wowote wa bure kutoka kwa matajiri kwa kiasi ambacho wengi wa wale wasiojiweza kabisa kujitosheleza kwa mahitaji muhimu ya maisha yao kwa namna duni sana - wengi hujipatia chakula chao kutoka katika mapipa ya taka (watoto wa mtaani), wengi hujisitiri kwa masalio yaliyookotezwa hapa na pale na wengi makazi yao ni stesheni na sokoni. Hawa, kisaikolojia, hujiona ni watu duni wasio na maana yoyote katika jamii na huwaona matajiri na watu wenye uwezo kuwa ndio wenye maana. Na hapa ndipo inapojengeka chuki baina ya wasionacho kuwachukia walio nacho.



(iii) Riba inaharibu uchumi wa jamii na maendeleo yake. Riba na msingi wake wa unyonyaji imma ikitozwa na tajiri mmoja au kikundi cha matajiri, imefanywa msingi wa uchumi wa taifa au wa kimataifa. Kwa bahati mbaya kutokana na mazoea tuliyonayo juu ya vyombo vya uchumi vya kitaifa na kimataifa vinavyoendeshwa katika misingi ya Riba kama vile mabenki ya taifa na shirika la Bima la Kimataifa, baadhi ya watu wamediriki kuhalalisha Riba ya mabenki na Bima. Kuhalalisha huku kwa riba ya mabenki na Bima aidha kumetokana na uzoefu wa uchumi haramu katika jamii zetu au umetokana na kushindwa kuona ubaya wa riba kitaifa au kimataifa.
Waislamu hatuna budi kukumbuka kuwa alichokiharamisha Allah (s.w) kinakuwa ni haramu katika wingi wake na katika uchache wake. Tukichukua mfano wa pombe Mtume (s.a.w.) amesema:



Kinacholewesha kikiwa kingi ni haramu pia hata kikiwa kichache. (Tirmidh, Abu Daud, Ibn Majah). Kwa hiyo kilicho haramishwa kwa mtu binafsi, pia ni haramu kwa taifa na ni haramu kwa mataifa yote ulimwenguni. Kwa upande mwingine jambo la haramu litakapotendwa kitaifa litakuwa na athari mbaya zaidi kwa jamii kuliko likitendwa katika kiwango cha mtu binafsi, hali kadhalika jambo baya likitendwa kimataifa huwa na athari kubwa na mbaya zaidi kwa jamii ya mwanadamu kuliko likitendwa katika kiwango cha kitaifa.



(iv) Riba ni mali ya dhulma inayonyakuliwa na matajiri kutoka kwa wanyonge kwa njia moja au nyingine kiuchumi, pia riba inaukandamiza na kuudidimiza uchumi wa kitaifa au kimataifa. Mali ya riba kwa kuwa ni mali inayopatikana bila jasho na bila hata ya kushiriki katika mashaka ya uchumi, huwafanya matajiri na wenye uwezo wa kuendesha miradi mbali mbali ya kiuchumi wakae tu bila kazi wakingojea fedha zao zizae katika mabenki ambazo wana kila uhakika wa kuzipata hata itokee gharka ya namna gani. Kwa hiyo kutokana na riba, jamii huwakosa watu wenye uwezo mkubwa wa kuzalisha mali ambao wangaliweza kuendesha miradi mbali mbali ya kiuchumi ambayo ingaliinua uchumi wa taifa na wa kimataifa kwa ujumla.



Wataalam wa uchumi wanakiri kuwa riba inaporomosha uchumi. Wamegundua kuwa kadiri kiwango cha riba kinavyokuwa kikubwa ndivyo uchumi unavyozidi kushuka kwa sababu matajiri huona kuwa wanapata faida kubwa zaidi na kwa njia nyepesi isiyotoa jasho lolote wakiweka fedha zao benki kuliko kuziingiza katika miradi ya kiuchumi. Hivyo utaona kuwa riba hupunguza uzalishaji na huongeza gharama za uzalishaji.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 781


Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mifumo ya benk na uchumi wa kiislamu
7. Soma Zaidi...

darsa nzuri zenye kuelimisha hasa katika ndoa ya kiislam.
Assalaam alykum warahmatullah wabarakatuh. Soma Zaidi...

Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya Jamii
(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi. Soma Zaidi...

Siku ambazo haziruhusiwi kufunga
Ni haramu kufunga katika masiku haya. Na endapo utafunga basi funga haitakuwa na malipo. Soma Zaidi...

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...

Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba
Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo Soma Zaidi...

Faida na umuhimu wa ndoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...

Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu
Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu. Soma Zaidi...

Je ni nani mwenye haki ya kutaliki
Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye. Soma Zaidi...

Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii. Soma Zaidi...

Namna lengo la zakat linavyofikiwa
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...