Namna ya kutambuwa kibla na umuhimu wa kuelekea kibla wakati wa kuswali

4.

Namna ya kutambuwa kibla na umuhimu wa kuelekea kibla wakati wa kuswali

4. Kuelekea Qibla



Kuelekea Qibla ni sharti la nne la kusimamisha swala. Katika hali ya kawaida Muumini ni lazima aelekee โ€œQibla wakati akiswali.Qibla ni neno la Kiarabu linatokana na neno โ€œQabalaโ€ lenye maana ya kuelekea sehemu au upande ambao watu huelekeza nyuso zao. Kwa mtazamo wa Qur-an, Qibla ni sehemu wanapoelekea waislamu wakati wa kuswali. Katika Qur-an tunafahamishwa kuwa Qibla ni sehemu ya katikati inayowaunganisha waumini kuwa mwili mmoja (kitu kimoja).


โ€œNa po pote wendako geuza uso wako kwenye Msikiti Mtakatifu . Na hiyo ndiyo haki itokayo kwa Mola wako. Na Mw enyezi Mungu si Mwenye kughafilika na yale mnayoyatenda. (2:149)



Ummati wa Muhammad (s.a.w) Qibla chake ni Kaโ€™aba, nyumba tukufu ya Allah iliyoko mjini Makkah, Saudi Arabia. Waislamu wote ulimwenguni huielekea Kaโ€™aba wakati wa kuswali. Swala yoyote itakayoswaliwa bila ya kuelekea upande ilipo Kaโ€™aba, pasipo na dharura inayokubalika kisheria kama vile kuwa mgonjwa, au kuwa safarini, ha is wih i.



Namna ya Kutafuta Qibla



Kukisia ulipo mji wa Makka, Saudi Arabia, ambao ndani yake iko Kaโ€™aba ni jambo rahisi kwa kutumia utaalamu wa Jiografia. Chombo


kizuri cha kumuwezesha mtu kukisia ilipo Kaโ€™aba ni ramani ya dunia. Utakapojua ulipo katika sehemu yoyote ya dunia utaweza kujua Kaโ€™aba iko upande gani wa dira kutokea pale ulipo kwa kutumia jua au chombo cha dira (Magnetic Compass). Kwa mfano ukiwa Tanzania, utaelekea Kaskazini kamili, ukiwa Pwani kama vile Dar es Salaam na ukiwa bara kama vile Kigoma, utaelekea Kaskazini ya Kaskazini Mashariki.



Kabla ya Muislamu hajaanza kuswali, hasa anapokuwa mgeni wa mahali hana budi kufanya jitihada ya kutafuta Qibla kwanza. Ni vyema mtu asafiripo awe na dira (Magnetic Compass) na ramani ili vifaa hivi vimsaidie kutafuta Qibla, vinginevyo itabidi awaulize wenyeji wa sehemu h iyo.



Mtu akishindwa kabisa kukibaini Qibla baada ya kujitahidi mwisho wa jitihada zake, popote atakapoelekea patafaa, kwani hii sasa imekuwa ni dharura, huku tukizingatia kuwa โ€œMashariki na Magharibi ni ya Mwenyezi Munguโ€.


Na Mashariki na Magharibi ni ya Mw enyezi Mungu. Basi mahala popote mgeukiapo (alikokuamrisheni Mw enyezi Mungu mtazikuta) huko radhi za Mwenyezi Mungu. Bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa (mkubwa kabisa) na Mwenye kujua (kukubwa kabisa vile vile). (2:115)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 4802

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi

Soma Zaidi...
HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุงุจู’ู†ู ู…ูŽุณู’ุนููˆุฏู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ู‚ูŽุงู„ูŽ: ู‚ูŽุงู„ูŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… "ู„ูŽุง ูŠูŽุญูู„ูู‘ ุฏูŽู…ู ุงู…ู’ุฑูุฆู ู…ูุณู’ู„ูู…ู [ ูŠุดู‡ุฏ ุฃู† ู„?...

Soma Zaidi...
Ni zipi najisi katika uislamu

Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.

Soma Zaidi...
Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea

Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir

Soma Zaidi...
Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.

Soma Zaidi...