picha

Aina za hijjah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

 

  1. Ifraad.

-    Ni aina ya Hijja amapo Hajj anavaa Ihram kwa nia ya kufanya Hijjah tu bila ya Umrah. 

-    Huanza kwa Talbiya; “Allaahumma labbaykal-Hijja” ‘Nimeitika kwa Hijjah’

-    Hajj huvaa Ihram mpaka amalize matendo yote ya Hija mwezi 10, Dhul-Hijjah.

-    Hajj halazimiki kuchinja siku ya mwezi 10, Dhul-Hijah. 

 

  1. Qiran.

-    Ni aina ya Hija ambapo Hajj hunuia kufanya Hija na Umrah pamoja.

-    Hajj huitika kwa Talbiya; “Allaahumma labbaykal-Hijja wal-Umrata”‘Nimeitika kwa Hijjah na Umrah.’

 

-    Hajj huwa katika Ihram mpaka alenge mawe minara mitatu, atufu Tawaful-Ifaadha na kunyoa mwezi 10, Dhul-Hijjah.

 

-    Hajj analazimika kuchinja mnyama.

-    Aina hii ya Hija hufanywa na wakazi wa Makka na wale waliokuja na wanyama.

 

  1. Tamattu.

-    Ni aina ya Hijah ambapo Hajj hunuia kufanya Umrah tu, kwa kuitika; “Allaahumma labbaykal-Umrah” – ‘Nimeitika kwa Umrah.’

 

-    Hajj huvua Ihram baada ya kufanya matendo yote ya Umrah na kunyoa na kuwa huru na miiko ya Ihram.

 

-    Hajj huvaa tena Ihram siku ya mwezi 8, Dhul-Hija na kuitika; “Allaahumma labbaykal-Hijjah”‘Nimeitika kwa Hijjah.’

 

-    Hajj atavua tena Ihram baada ya kutupa mawe na kunyoa mwezi 10, Dhul-Hija.

-    Hajj atalazimika kuchinja mnyama siku ya mwezi 10, Dhul-Hija kwa kununua mnyama kama hakuja nayo. Qur’an (2:196).


-    Aina hii ya Hija ni bora na nafuu kwa wanaotoka mbali na hawana wanyama wa kuchinja

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 4439

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma

Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.

Soma Zaidi...
Maana ya mirathi katika uislamu

Post hii itakufundishabkuhusu mirathi ya kiislamu, maana yake.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu

Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.

Soma Zaidi...