Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Ni aina ya Hijja amapo Hajj anavaa Ihram kwa nia ya kufanya Hijjah tu bila ya Umrah.
- Huanza kwa Talbiya; “Allaahumma labbaykal-Hijja” – ‘Nimeitika kwa Hijjah’
- Hajj huvaa Ihram mpaka amalize matendo yote ya Hija mwezi 10, Dhul-Hijjah.
- Hajj halazimiki kuchinja siku ya mwezi 10, Dhul-Hijah.
- Ni aina ya Hija ambapo Hajj hunuia kufanya Hija na Umrah pamoja.
- Hajj huitika kwa Talbiya; “Allaahumma labbaykal-Hijja wal-Umrata” – ‘Nimeitika kwa Hijjah na Umrah.’
- Hajj huwa katika Ihram mpaka alenge mawe minara mitatu, atufu Tawaful-Ifaadha na kunyoa mwezi 10, Dhul-Hijjah.
- Hajj analazimika kuchinja mnyama.
- Aina hii ya Hija hufanywa na wakazi wa Makka na wale waliokuja na wanyama.
- Ni aina ya Hijah ambapo Hajj hunuia kufanya Umrah tu, kwa kuitika; “Allaahumma labbaykal-Umrah” – ‘Nimeitika kwa Umrah.’
- Hajj huvua Ihram baada ya kufanya matendo yote ya Umrah na kunyoa na kuwa huru na miiko ya Ihram.
- Hajj huvaa tena Ihram siku ya mwezi 8, Dhul-Hija na kuitika; “Allaahumma labbaykal-Hijjah” – ‘Nimeitika kwa Hijjah.’
- Hajj atavua tena Ihram baada ya kutupa mawe na kunyoa mwezi 10, Dhul-Hija.
- Hajj atalazimika kuchinja mnyama siku ya mwezi 10, Dhul-Hija kwa kununua mnyama kama hakuja nayo. Qur’an (2:196).
- Aina hii ya Hija ni bora na nafuu kwa wanaotoka mbali na hawana wanyama wa kuchinja
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.
Soma Zaidi...Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...