Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Ni aina ya Hijja amapo Hajj anavaa Ihram kwa nia ya kufanya Hijjah tu bila ya Umrah.
- Huanza kwa Talbiya; “Allaahumma labbaykal-Hijja” – ‘Nimeitika kwa Hijjah’
- Hajj huvaa Ihram mpaka amalize matendo yote ya Hija mwezi 10, Dhul-Hijjah.
- Hajj halazimiki kuchinja siku ya mwezi 10, Dhul-Hijah.
- Ni aina ya Hija ambapo Hajj hunuia kufanya Hija na Umrah pamoja.
- Hajj huitika kwa Talbiya; “Allaahumma labbaykal-Hijja wal-Umrata” – ‘Nimeitika kwa Hijjah na Umrah.’
- Hajj huwa katika Ihram mpaka alenge mawe minara mitatu, atufu Tawaful-Ifaadha na kunyoa mwezi 10, Dhul-Hijjah.
- Hajj analazimika kuchinja mnyama.
- Aina hii ya Hija hufanywa na wakazi wa Makka na wale waliokuja na wanyama.
- Ni aina ya Hijah ambapo Hajj hunuia kufanya Umrah tu, kwa kuitika; “Allaahumma labbaykal-Umrah” – ‘Nimeitika kwa Umrah.’
- Hajj huvua Ihram baada ya kufanya matendo yote ya Umrah na kunyoa na kuwa huru na miiko ya Ihram.
- Hajj huvaa tena Ihram siku ya mwezi 8, Dhul-Hija na kuitika; “Allaahumma labbaykal-Hijjah” – ‘Nimeitika kwa Hijjah.’
- Hajj atavua tena Ihram baada ya kutupa mawe na kunyoa mwezi 10, Dhul-Hija.
- Hajj atalazimika kuchinja mnyama siku ya mwezi 10, Dhul-Hija kwa kununua mnyama kama hakuja nayo. Qur’an (2:196).
- Aina hii ya Hija ni bora na nafuu kwa wanaotoka mbali na hawana wanyama wa kuchinja
Umeionaje Makala hii.. ?
Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.
Soma Zaidi...Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf
Soma Zaidi...Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada.
Soma Zaidi...Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...Je unadhani ni kwa nini waislamu wanaelekea kibla, na jinsi gani utaweza kukipata kibla.
Soma Zaidi...