Wajibu kwa Jirani
Pamoja na kuwajibika kutekeleza haki mbali mbali kwa wanafamilia tunawajibika vile vile kuwatendea wema majirani zetu wakiwa waislamu au katika dini nyingine. Qur-an inasisitiza:
"... Na wafanyieni ihsani wazazi wawili, jamaa, yatima, maskini najirani waliokaribu najirani walio mbali na rafiki walio ubavuni mwenu..." (4:36)
Mtume wa Allah (s.w) ametuusia juu ya suala Ia kuwafanyia ihsani jirani kwa uzito mkubwa kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
"Anas(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ambayejirani yake hasalimiki kutokana na ukorofi wake, hataingia peponi." (Muslim)
Aysha na Ibn 'Umar (r. a) wameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Jibril hakuacha kunihimiza juu ya jirani mpaka nikahisi kuwa si muda mrefujirani atafanywa kuwa mrithi." (Bukhari na Muslim)
Katika hadith iliyosimuliwa na lbn Mas'ud (r.a) Mtume (s.a.w) amesikika akisisitiza:
"... Naapa kwa yule aliyeshikilia maisha yangu mkononi mwake, mtu hatakuwa Muislamu wa kweli mpaka moyo wake na ulimi wake viukiri Uislamu, na hatakuwa muumini wa kweli mapaka jirani yake asalimike na kero zake." (Ahmad)
Pia Mtume (s.a.w) anatufahamisha kuwa kipimo cha mtu kuwa ni mwema au ni mbaya ni jirani zake kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Ibn Mas 'ud (r.a) ameeleza kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume wa Allah: "Ee Mtume wa Allah! Nitatambuaje kuwa nimefanya mazuri na nitajuaje kuwa nimefanya mabaya?" Mtume (s.a.w) alimjibu: "Utakapowasikia majirani zako wakisema umefanya vizuri," basi umefanya vizuri na utakapowasikia wakisema - umefanya vibaya basi umefanya vibaya. Huu ndio ukweli kwa sababu majirani wako karibu sana na wewe na kwa hiyo wanaijua vema tabia yako.
Umeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.
Soma Zaidi...- Uislamu ulieneza nadharia kuwa wanaadamu wote ni sawa na wote ni watumwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.
Soma Zaidi...Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.
Soma Zaidi...Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Soma Zaidi...Ni haramu kufunga katika masiku haya. Na endapo utafunga basi funga haitakuwa na malipo.
Soma Zaidi...Mambo haya yanaweza kuharibu funga ya mtu ama kupunguza malipo ya funga.
Soma Zaidi...