image

Haki na wajibu kwa jirani

Haki na wajibu kwa jirani

Wajibu kwa Jirani



Pamoja na kuwajibika kutekeleza haki mbali mbali kwa wanafamilia tunawajibika vile vile kuwatendea wema majirani zetu wakiwa waislamu au katika dini nyingine. Qur-an inasisitiza:


"... Na wafanyieni ihsani wazazi wawili, jamaa, yatima, maskini najirani waliokaribu najirani walio mbali na rafiki walio ubavuni mwenu..." (4:36)
Mtume wa Allah (s.w) ametuusia juu ya suala Ia kuwafanyia ihsani jirani kwa uzito mkubwa kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:



"Anas(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ambayejirani yake hasalimiki kutokana na ukorofi wake, hataingia peponi." (Muslim)
Aysha na Ibn 'Umar (r. a) wameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Jibril hakuacha kunihimiza juu ya jirani mpaka nikahisi kuwa si muda mrefujirani atafanywa kuwa mrithi." (Bukhari na Muslim)



Katika hadith iliyosimuliwa na lbn Mas'ud (r.a) Mtume (s.a.w) amesikika akisisitiza:
"... Naapa kwa yule aliyeshikilia maisha yangu mkononi mwake, mtu hatakuwa Muislamu wa kweli mpaka moyo wake na ulimi wake viukiri Uislamu, na hatakuwa muumini wa kweli mapaka jirani yake asalimike na kero zake." (Ahmad)



Pia Mtume (s.a.w) anatufahamisha kuwa kipimo cha mtu kuwa ni mwema au ni mbaya ni jirani zake kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:


Ibn Mas 'ud (r.a) ameeleza kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume wa Allah: "Ee Mtume wa Allah! Nitatambuaje kuwa nimefanya mazuri na nitajuaje kuwa nimefanya mabaya?" Mtume (s.a.w) alimjibu: "Utakapowasikia majirani zako wakisema umefanya vizuri," basi umefanya vizuri na utakapowasikia wakisema - umefanya vibaya basi umefanya vibaya. Huu ndio ukweli kwa sababu majirani wako karibu sana na wewe na kwa hiyo wanaijua vema tabia yako.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 291


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Tathmini ya swala zetu, kwa nini swala zetu hazijibiwi?
Soma Zaidi...

Utaratibu wa kuzika, hatua kwa hatua, na namna ya kusindikiza jeneza
4. Soma Zaidi...

haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu
Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee. Soma Zaidi...

Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

Funga za Sunnah na namna ya kuzitekeleza
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mifumo ya benki na kazi zake
Hapa utajifunza kazi za benki. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke Ulaya chini ya kanisa hapo zamani
Soma Zaidi...

Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu
Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli. Soma Zaidi...

Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu
Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi. Soma Zaidi...

Zijuwe sunnha 9 za swala
Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki. Soma Zaidi...

Kusimamisha Swala
Kusimamisha Swala. Soma Zaidi...

Namna ya kuswali
2. Soma Zaidi...