FAHAMU KUHSU VITAMINI E NA KAZI ZAKE MWILINI


image


Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.


 

VITAMINI E NA FAIDA ZAKE MWILINI

Vitamini E ni moja kati aya vitamini ambavyo vinapatikana kwenye vyakula, matunda na mboga. Pia unaweza kuvipata kwa njia ya vidonge kutoka kwenye maduka ya madawa. Kama vilivyo vitamini A, B, C, D na K vitamini E navyo endapo vitapungua mwilini kutakuwepo na madhara kiafya. Ijapokuwa upungufu wa vitamini hivi ni aghalabu sana kutokea. Katika makala hii nitakwenda kukupa somo linalohusu vitamini E, kazi zake, chanzo chake na madhara ya upungufu wake.


 

YALIYOMO:

  1. Maana ya vitamini E
  2. Kazi za vitamini E
  3. Vyakula vya vitamini E
  4. Upungufu wa vitamini E
  5. Tafiti kuhusu vitamini E


 

Maana ya Vitamini E

Mnamo mwaka 1922 wanasayansi wawili kwa majina ya Herbert Mclean Evans na mwenzie Katharine Scott Bishop waligundua vitamini E. baada ya ugunduzi wa vitamini E tafiti mbalimbali ziilifanywa katika kuonyesha ni zipi kazi za vitaini E mwilini. Kwa mfano Mwaka 1946 wanasayansi walikuwa wakifanya tafiti juu ya nadharia inayodai kuwa vtamini E husaidia dhidi ya maradhi ya moyo na mishipa ya damu (coronary heart diseases). mwaka 1949 tafiti zilifanywa kuhusu nadharia ya kuwa vitamini E huweza kusaidia watoto njiti kuwakinga na maradhi kadhaa.


 

Kazi za vitamini E mwilini
Vitamini E katika miili yetu zina kazi kuu zifuatazo:
Vitamini E bi antioxidant, ndani ya miili yetu husaidia katika kuzuia athari za kemikali mbaya zifiharibu miiliyetu.
Husaidia katika utengenezwaji wa utando wa seli,na kulinda seli dhidi ya uharibifu wa kemikali.
Husaidia katika ukuaji mzuri wa misuli.
Husaidia katika utengenezwaji wa utando maeneo mbalimbali ya mwili kama kwenye neva, mapafu, na maeneo mengine


 

Upungufu wa vitamini E
Upungufu wa vitamini E hutokea nadra sana lakini tafiti zinaonyesha kuwa vitamini E vikipungua mwilini vinaweza kusababisha matatizo kwenye mfumo wa fahamu., ukuaji mzuri wa misuli na udhaifu wa misuli. Pia upungufu wa vitamini E unaweza kuathiri macho na hivyo kupelekea mtu kutoona vizuri.


 

Vyakula vya vitamini E

  1. Nyama ya kuku, ngo’ombe

  2. Maini

  3. Mayai

  4. Alizeti

  5. Karanga

  6. Spinach

  7. Korosho

  8. Mchele

  9. Viazi vitamu

  10. Siagi

  11. Samaki

  12. Maziwa

  13. palachichi

 


 

Tafiti mbalimbali kuhusu vitamini E
Tafiti hizi zilifanya lakini zinahitaji kuendelea zaidi maana bado majibu ya uhakika hayajapatikana juu ya matokeo ya tafiti hizo. Ijapokuwa maneno ni kama hivyo lakini ukweli ni kuwa vitamini E vina faida katika afya zetu:-
1. Mwaka 2017 tafiti zilifanya na kuonyesha kuwa vitamini E husaidia katika kupunguza udhaifu wa misuli wakati wa kuzeheka
2. Tafiti zinaonyesha kuwa vitamini E husaidia katika kulinda mtu dhidi ya maradhi ya ubongo kama kusahausahau na kuchanganyikiwa.
3. Tafiti zinaonyesha kuwa vitamini E mwilini husaidia katika kupunguza uwezekano wa kupata saratani ya figo, kibofu, mapafu na korodani.
4. Husaidia kulinda mwili dhidi ya maradhi ya moyo na mishipa ya damu
5. Husaidia kwa wajawazito

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Madrasa kiganjani    





Je una umaswali, maoni ama mapendekezo?
Download App yetu kuwasiliana nasi




Post Nyingine


image Vyakula hatari kwa mwenye kisukari
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula hatari kwa mwenye kisukari Soma Zaidi...

image Fahamu kuhsu vitamini E na kazi zake mwilini
Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...

image je ni vipi vyakula vyenye protini kwa wingi?
Makala hii iatakuletea aina kuu tano za vywkula vyenye protini nyingi zaidi. Kama ulikuwa unajiuliza kuwa ni vyakula ipi hasa vinaweza kukupatia protini kwa wingi ni vipi, makala hii ndio majibu yako kwa swali hilo. Soma Zaidi...

image Vyakula vyenye vitamini C kwa wingi
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya vyakula vyenye vitamini C kwa wingi Soma Zaidi...

image Faida za kunywa maziwa
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kunywa maziwa kiafya Soma Zaidi...

image Vyakula vinavyosaidia kupunguza uzito
Posti hii inahusu vyakula ambavyo vinasaidia kupunguza uzito, ni baadhi ya vyakula ambavyo unaweza kutumia ili kuweza kuweka kwenye hali ya kawaida. Soma Zaidi...

image Kazi za vitamini B mwilini Na upungufu wa vitamini B mwilini
vitamini B vipo katika makundi mengi kma aB1, B2, B3, B5, B6, B7 na B12. Makala hii itakwenda kukutajia kazi kuu za Vitamini B katika miili yetu Soma Zaidi...

image Faida za kahawa mwilini.
Posti hii inahusu zaidi faida za kahawa mwilini, ni faida ambazo ujitokeza hasa kwa watumiaji wa kahawa. Soma Zaidi...

image Madhara ya chakula kutosagwa vizuri tumboni.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya chakula kushindwa kumengenywa vizuri tumboni, haya ni madhara ambayo utokea kwa sababu ya chakula kushindwa kumengenywa vizuri tumboni. Soma Zaidi...

image Fahamu tiba ya lishe ya ugonjwa wa kisukari
Post hii inahusu zaidi tiba ya lishe ya ugonjwa wa kisukari ni tiba ambayo utumiwa sana na wagonjwa wa kisukari na walio wengi na wamefanikiwa kupona Soma Zaidi...