Dawa ya Vidonda vya tumbo

Nitakujuza dawa ya kutibu vidonda vya tumbo, na kutibu vidonda vya tumbo sugu

Dawa ya Vidonda vya tumbo

DAWA YA VIDONDA VYA TUMBO
Dawa za vidonda vya tumbo zinategemea aina za vidonda alivyo navyo, mahala vilipo na sababu za vidonda hivyo. Kitu cha kwanza kuangalia ni sababu gani zilizopelekea vidonda hivyo?. kisha baada ya kuijuwa sababu ndipo maibabu yatafuata. Kama tulivyokwisha jifunza kuwa sababu kuu za vidonda vya tumbo ni bakteria aina ya Hypylori. Hivyo kama sababu ni hii mgonjwa atapewa dawa ya kuwauwa hawa bakteria. Pia kama sabau ni asidi tumboni atapewa dawa za kupunguza uzalishwaji wa hizi asidi. Dawa za vidonda vya tumbo ni kama zifuatazo:-



1.Dawa kwa ajili ya kuuwa bakteria. Hapa mgonjwa atapewa dawa kama:-
A.Amoxicillin (amoxil)
B.Clarithromycin (Biaxin)
C.Metronidazole (flagyl)
D.Tinidazole (tindamax)
E.Tetracyline
F.Levolaxacin



2.Dawa za kuzuia uzalishwaji wa asidi mwilini (proton pump inhibitors (PPIs))
A.Omeprazole (Prilosec)
B.Lansoprazole (Prevacid)
C.Rabeprazole (Aciphex)
D.Esomeprazole (Nexium)
E.Panztoprazole (Protonix)



3.Dawa za kupunguza uzalishwaji wa asidi tumboni (Acid blockers (histamine (H-2))
A.Famoditine (Pepcid AC)
B.Cimetidine (Tagamet HB)
C.Nizatidine (Axid AR)



4.Dawa zinzzolinda ukuta wa utumbo na tumbo
A.Cytoprotective agents
B.Sucralfate (Carafate)
C.Misoprostol (Cytotec)



TIBA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO.
Wataalamu wa afya pia wanakubali uwepo wa tiba mbadala katika kutibi vidonda vya tumbo. Zipo nyingi sana, miongoni mwazo ni:-
A.Bamia
B.Kitunguu thaumu
C.Asali



Kwa nini vidonda haviponi hata baada ya kutumia dawa?
Hii hutokea endapo:-
A.Kama mgonjwa hakutumia dawa kwa kufuata masharti vyema
B.Haswa kuna baadhi ya bakteria wa vidonda vya tumbo wana usugu wa kufa na dawa
C.Kama unatumia tumbaku
D.Kama unatumia dawa za NSAIDs



Pia mara chache vidonda vya tumbo vinaweza kusababishwa na:-
A.Uzalishwaji wa asidi kupitiliza
B.Mashambulizi mengie yasiyo ya H.pylori
C.Saratani ya tumbo
D.Kuwa na maradhi mengine





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 2479

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa ya fluconazole ni dawa ya kutibu fangasi za aina au za sehemu mbalimbali,

Soma Zaidi...
Dawa ya vidonda vya tumbo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital

Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.

Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulik

Soma Zaidi...
Matibabu ya Fangasi ukeni na dawa za fangasi wanaoshambulia uke.

Fangasi wanaweza kushambulia uke, kwa juu kwenye mashhav ya uke ama kwa ndani. Hali hii inaweza kusababisha miwasho na maumivu pia. Inaweza kusababisha michubuko na kutofurahia tendo la ndoa. Makala hii inakwenda kukujuza dawa na matibabu ya fangasi ukeni

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Soma Zaidi...
Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.

Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.

Soma Zaidi...
Dawa ya maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukuletea dawa ya maumivu ya jino

Soma Zaidi...