Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia kutibu minyoo, na pia imefanikiwa sana kadri ya watumiaji wa dawa hiyo.
Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole .
1. Dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambayo imechaguliwa kutibu minyoo aina ya ascrarisisi, hookworm, maambukizi yatokanayo na minyoo,strongyloidiasis,trichuria,anterobiasisi na trichostrongyloidiasi hayo ni majina ya kitaalamu yanayotumika kuitwa na minyoo ambayo utibiwa na dawa ya Albendazole,
2. Kwa kawaida dawa hizi uwekwa kwenye tumbo lililowazi ili kama wadudu wapo waweze kuuawa vizuri bila kujificha kwenye chakula na pia ushauliwa kutumiwa wakati wa asubuhi kabla mtu hajala chakula chochote na kwa kawaida dawa hizo utafunwa na pia kumezwa bila maji na baadae mtu anaweza kula chakula.
3. Pia dawa hii huwa na maudhui madogo madogo ambayo ujitokeza baada ya kutumia dawa na maudhui hayo yakizidi ni vizuri kumwona daktari au mtaalamu wa mambo ya afya, na maudhui hayo ni kama kiungulia,kuharisha, maumivu ya kichwa, kichefuchefu na kutapika, kizunguzungu kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa za Albendazole baada ya kuona dalili kama hizo ni matokeo ya dawa.
4. Kwa kawaida dawa hizi hazitumiki kwa watu wote, wengine wanaweza kutumia ila akina Mama wenye mimba changa na wajawazito hawapaswi kutumia na watoto chini ya miaka miwili hawapaswi kutumia dawa hii kwa sababu ya matokeo yake kwao kama mimba kutoka kwa wanawake wenye mimba changa na watoto wadogo wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa degedege.
5. Kwa hiyo katika kutumia dawa hiii ni vizuri kabisa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya sio kutumia kiholela kwa sababu madhara yake yanaweza kuwa makubwa zaidi ikiwa dawa hii inatumika visivyo kwa hiyo ni lazima kuwaona wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa hizi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 ai web app 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Dawa ya Isoniazid na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi dawa ya lsoniazid nA kazi zake, ni dawa ambayo inasaidia kutibu kifua kikuu kati ya madawa yaliyoteuliwa na kuwa na sifa ya kutibu kifua kikuu.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing
Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...Dawa ya fluconazole kama dawa ya fangasi
Post hii inahusu zaidi dawa za fangasi na matumizi yake kwa kutumia dawa ya fluconazole kama dawa mojawapo ya fangasi.
Soma Zaidi...Kazi ya Dawa ya salbutamol
Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.
Soma Zaidi...Umuhimu wa kutumia dawa za ARV
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .
Soma Zaidi...