picha

Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.

Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu.

1.Tiba ya kifua kikuu imegawanyika katika makundi mawili na kila kundi huwa na dawa zake kutofautiana na kundi jingine, makundi menyewe ni kama ifuatavyo.

 

2. Kundi la kwanza ambalo kwa kitaalamu huitwa initial phase, kundi hili lina madawa ya rifampin, isoniazid,pyrazinamide na ethambutol dawa hizi utumika kwa miezi miwili kwa mgonjwa anayeanza matibabu yaani mgonjwa mpya.

 

 

3. Na pia mgonjwa uongezewa dawa nyingine mpya ya streptomycin, na zile za mwanzo nazo utumika ambazo ni isoniazid, rifampin, ethambutol na pyrazinamide dawa hizi utumika kwa miezi miwili tena kwa mgonjwa mpya.

 

 

 

4. Pia mgonjwa uongezewa mwezi mwingine mmoja kwa dawa zile za mwanzo ambazo ni isoniazid, rifampin, pyrazinamide and ethambutol kwa hiyo kwa ujumla mgonjwa mpya utumia miezi mitano katika matibabu.

 

 

5. Kipindi cha pili utumia miezi tisa ikiwa mgonjwa alipotumia dawa kwenye kipindi cha kwanza akaona na baada ya siku chache ugonjwa ukajiridia tena na matibabu uanza upya kama ifuatavyo.

 

 

6. Kwenye miezi minne ya mwanzo mgonjwa utumia dawa zifuatazo rifampin na isoniazid kwa kipindi cha miezi minne na pia mgonjwa uongezewa dawa nyingine moja ambayo ni ethambutol kwa kipindi cha miezi mitano yaani miezi minne ya kwanza mgonjwa utumia rifampin, isoniazid, na katika kipindi cha miezi mitano ya mwisho mgonjwa utumia rifampin, isoniazid na ethambutol kwa miezi mitano kwa hiyo kipindi cha mwisho utumia miezi mitano katika matibabu.

 

 

 

7. Katika siku za mwanzoni mgonjwa anapogunduliwa kubwa na kifua kikuu anaweza kuambukiza watu wengine ila baada ya kuanza dawa kwa kipindi cha wiki mbili mgonjwa hawezi kuambukiza wengine kwa hiyo ni vizuri zaidi na kuchukua tahadhari kwa sababu ugonjwa huu utibiwa kwa mda mrefu ingawa watu wanapona lakini tahadhari ni ya muhimu.

 

 

 

8. Kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu kwa watu kuhusu ugonjwa huu kwamba unapina na pia kuachana na mila na desturi za kuwatenga watu wenye ugonjwa huu na pia kuwaficha watu wenye ugonjwa huu kwa sababu ya mila na desturi kwa sababu kadri watu wanabyofichwa kwenye majumba na kuhudumiwa wakiwa wamefichwa usababisha kuongezeka kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kudai kwamba familia fulani kuna kifua kikuu , kwa hiyo jamii inapaswa kuelezwa kwamba ugonjwa huu unatibika na watu wanapona.

 

 

 

 

9. Pia tunapaswa kuacha imani kwamba kila mtu mwenye kifua kikuu ana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi siyo kweli kwa sababu tumeona jinsi kifua kikuu kinavyoonezaa kwa hiyo watu watoe hofu kwamba sio kila mwenye kifua kikuu ni mwathirika wa maambukizi ya Virusi vya, ila kupima maambukizi ni vizuri ili kujua afya zetu.

 

 

 

 

10. Pia na dawa tulizoziona za kutibu kifua kikuu ni lazima kuzipata hospitali sio mitaani au madukani kwa sababu kuna maelekezo ya kufuata katiks matumi na tutaweza kuchambua dawa moja na nyingine hapo mbeleni.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/12/16/Friday - 12:02:02 am Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1192

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 web hosting    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Fahamu Dawa itwayo Diazepam

Diazepam ni nini? Diazepam ni Dawa ambayo Huathiri kemikali kwenye ubongo ambazo zinaweza kukosa uwiano na kusababisha wasiwasi. Diazepam hutumiwa kutibu matatizo ya wasiwasi, dalili za kuacha pombe, au misuli. Diazepam wakati mwingine hutumiwa pamoja n

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Ampicillin.

Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici

Soma Zaidi...
dawa ya kutibu infection kwenye kizazi nisaidie doctor

Je unasumbuliwa na maambukizi na mashambulizi ya virusi na bakteria kwenye sehemu za siri ama via vya uzazi?. Posti hii inakwenda kuupa ushauri.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.

Soma Zaidi...
Penicillin dawa ya kutibu maambukizi ya bakteria mwilini

Post hii Inahusu zaidi dawa za kutibu maambukizi yoyote Yale yanayosababishwa na bakteria dawa hizi kwa kitaamu huiitwa antibiotics Kuna dawa mbalimbali zinazotibu maambukizi ya bakteria leo tutaanza na dawa ambayo inaitwa penicillin.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa

Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole

Post hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia kutibu minyoo, na pia imefanikiwa sana kadri ya watumiaji wa dawa hiyo.

Soma Zaidi...
Dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo.

Posti hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo, ni Aina mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu Minyoo inayosababishwa na bakteria mbalimbali.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa ya fluconazole ni dawa ya kutibu fangasi za aina au za sehemu mbalimbali,

Soma Zaidi...