picha

Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.

Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu.

1.Tiba ya kifua kikuu imegawanyika katika makundi mawili na kila kundi huwa na dawa zake kutofautiana na kundi jingine, makundi menyewe ni kama ifuatavyo.

 

2. Kundi la kwanza ambalo kwa kitaalamu huitwa initial phase, kundi hili lina madawa ya rifampin, isoniazid,pyrazinamide na ethambutol dawa hizi utumika kwa miezi miwili kwa mgonjwa anayeanza matibabu yaani mgonjwa mpya.

 

 

3. Na pia mgonjwa uongezewa dawa nyingine mpya ya streptomycin, na zile za mwanzo nazo utumika ambazo ni isoniazid, rifampin, ethambutol na pyrazinamide dawa hizi utumika kwa miezi miwili tena kwa mgonjwa mpya.

 

 

 

4. Pia mgonjwa uongezewa mwezi mwingine mmoja kwa dawa zile za mwanzo ambazo ni isoniazid, rifampin, pyrazinamide and ethambutol kwa hiyo kwa ujumla mgonjwa mpya utumia miezi mitano katika matibabu.

 

 

5. Kipindi cha pili utumia miezi tisa ikiwa mgonjwa alipotumia dawa kwenye kipindi cha kwanza akaona na baada ya siku chache ugonjwa ukajiridia tena na matibabu uanza upya kama ifuatavyo.

 

 

6. Kwenye miezi minne ya mwanzo mgonjwa utumia dawa zifuatazo rifampin na isoniazid kwa kipindi cha miezi minne na pia mgonjwa uongezewa dawa nyingine moja ambayo ni ethambutol kwa kipindi cha miezi mitano yaani miezi minne ya kwanza mgonjwa utumia rifampin, isoniazid, na katika kipindi cha miezi mitano ya mwisho mgonjwa utumia rifampin, isoniazid na ethambutol kwa miezi mitano kwa hiyo kipindi cha mwisho utumia miezi mitano katika matibabu.

 

 

 

7. Katika siku za mwanzoni mgonjwa anapogunduliwa kubwa na kifua kikuu anaweza kuambukiza watu wengine ila baada ya kuanza dawa kwa kipindi cha wiki mbili mgonjwa hawezi kuambukiza wengine kwa hiyo ni vizuri zaidi na kuchukua tahadhari kwa sababu ugonjwa huu utibiwa kwa mda mrefu ingawa watu wanapona lakini tahadhari ni ya muhimu.

 

 

 

8. Kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu kwa watu kuhusu ugonjwa huu kwamba unapina na pia kuachana na mila na desturi za kuwatenga watu wenye ugonjwa huu na pia kuwaficha watu wenye ugonjwa huu kwa sababu ya mila na desturi kwa sababu kadri watu wanabyofichwa kwenye majumba na kuhudumiwa wakiwa wamefichwa usababisha kuongezeka kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kudai kwamba familia fulani kuna kifua kikuu , kwa hiyo jamii inapaswa kuelezwa kwamba ugonjwa huu unatibika na watu wanapona.

 

 

 

 

9. Pia tunapaswa kuacha imani kwamba kila mtu mwenye kifua kikuu ana maambukizi ya Virusi vya Ukimwi siyo kweli kwa sababu tumeona jinsi kifua kikuu kinavyoonezaa kwa hiyo watu watoe hofu kwamba sio kila mwenye kifua kikuu ni mwathirika wa maambukizi ya Virusi vya, ila kupima maambukizi ni vizuri ili kujua afya zetu.

 

 

 

 

10. Pia na dawa tulizoziona za kutibu kifua kikuu ni lazima kuzipata hospitali sio mitaani au madukani kwa sababu kuna maelekezo ya kufuata katiks matumi na tutaweza kuchambua dawa moja na nyingine hapo mbeleni.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 1412

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa

Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.

Soma Zaidi...
Dawa ya Vidonda vya tumbo

Nitakujuza dawa ya kutibu vidonda vya tumbo, na kutibu vidonda vya tumbo sugu

Soma Zaidi...
Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole

Post hii inahusu zaidi dawa ya mebendazole ni dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo utokea kwa watoto na watu wazima.

Soma Zaidi...
Dawa za mitishamba za kutibu meno

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za mitishamba za kutibu meno

Soma Zaidi...
Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin

Soma Zaidi...