Dawa ya kutibu maumivu ya jino
Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino
Dawa ywa maumivu ya jino.
Maumivu ya jino ma kwa jina lingine hufahamka kama odontalgia, ni maumivu makali yanayoweza kutokea kwenye ufinzi, mdomo na mifupa inayolishika jino. Maumivu haya yanaweza kuwa makali sana kiasi cha mtu kuomba msada. Wakati mwingine maumivu haya hutokea baada ya kula vitu ama kufanya jambo lakini hii sio lazima. Huwenda pia yakatokea bila hata ya sababu yeyote ile.
Je na wewe ni miongoni mwa wanaosumbuliwa na maumivu ya meno. Makala hii ni kwa ajili yako. Utajifunza sababu za maumivu ya jino, yanatokeaje, utakabiliana vipi na dawa gani utumie. Kama ukipenda makala hii usiwache kututupia maoni hapo chini:-
Sababu za kutokea maumivu ya jino:
1.Kuwa na majeraha kwenye jino ama kuzungukia jino. Majeraha ni kawaida sana kusababisha kubenduka na kukatika kwa meno.
2.Maambukizi na mashambulizi ya jino yaliyosababishwa na wadudu.
3.Kusaga ma kugonga meno hasa wakati wa usiku unapolala
4.Kuwa na magonjwa kwenye ufinzi
Dalili za maumivu ya jino
1.Maumivu wakati unapotafuna
2.Kuhisi mabadiliko endapo hali ya hewe itabadilika
3.Kuvimba kwa shavu ama kidevu
4.Mafinzi kutoa damu ama kutoma majimaji
5.Maumivu ya kichwa
6.Homa
7.Maumivu ya sikio
8.Kupotea kwa ladha ya chakula
9.Maumivu ya shingo
Dawa ya maumivu ya jino
Kuna matibabu kadha anaweza kupatiwa mgonjwa kama kung’oa jino, kuuwa bakteria kama ndio sababu. Pia kutumia dawa za kupunguza maumivu. Miongoni mwa dawa za maumivu ya meno ni:-
1.Ibuprofen
2.Naproxen
3.Acetaminophen
NITAJILINDA VIPI MA MAGONJWA YA MENO?
1.Punguza kula vitu vyenye sukari nying kwa wingi kama pipi
2.Safisha kinywa kwa mswaki kara kwa mara
3.Usilale na mabaki ya chakula mdomoni.
Dawa za mitishamba za kutibu meno
1.Kutumia muarobaini, unatafuna vijani vichanga na kuelekeza kwenye jino linalouma
2.Tafuna karafuu kuelekea kwenye jino linalouma
3.Tafuna kitunguu thaumu kuelekea jino linalouma
4.Bandua gome la muembe kish alichune gamba la juu, kisha chemsha hilo gamba kisha kunywa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Fahamu kuhusu dawa ya griseofulvin
Post hii inahusu zaidi dawa ya griseofulvin ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye ngozi ambazo usababisha mabaka mabaka kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ambazo uchangia kupungua kwa nguvu za kiume
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali ambazo uchangia katika kupunguza nguvu za kiume , hii ni kwa sababu ya wataalamu mbalimbali wanavyosema
Soma Zaidi...Dawa ya fluconazole kama dawa ya fangasi
Post hii inahusu zaidi dawa za fangasi na matumizi yake kwa kutumia dawa ya fluconazole kama dawa mojawapo ya fangasi.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha
Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)
Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin,
Soma Zaidi...Dawa ya chango na maumivu ya hedhi
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na maumivu ya hedhi
Soma Zaidi...