picha

Dawa ya kutibu UTI

Nitakujuza dalili za UTI na dawa za kutibu UTI. Pia tutaona njia za kujikinga na UTI pamoja na dalili za UTI

Dawa ya kutibu UTI

Dawa ya UTI na UTI iliyo sugu
Kama ulishawahi kujiuliza masalikama chanzo cha UTI, sababu zake, njia za kukabiliana na uti vipi uti inaenezwa na ni zipi dawa zake. Makala hii ni kwa ajili yako, nimeiandaa kwa ufupi na kwa ufanisi kiasi cha kuweza kukuridhisha kwa majibu ya maswali yako. Kama utakuwa na mawazo zaidi, tuachie maoni yako hapo chini.



Ugonjwa wa UTI ni nini?
UTI ni kifupisho cha maneno Urinary Track Infection. Ni maambukishi na mashambulizi ya bakteria aina ya E.coil katika mfumo wa mkojo. Mwanzoni bakteria huingia kwenye kibofu, figo ama sehemu yeyote kwenye mfumo wa mkojo. Kisha bakteria huyu anaanza kushambulia na kuathiri mfumo huu na ndipo dalili za UTI huanza kuonekana kama maumivu wakati wa kukojoa. Dalili za uti huonekana kuanzia siku 3 mpaka 8 toka kuambukizwa.



Ni zipi sababu za UTI
Sababu kuu za ugonjwa wa UTI ni bakteria aina ya E.coil. Bakteria huyu huishi kwenye utumbo. Sasa endapoa atapata njia kutoka kwenye utumbo kupitia haja kubwa na akaingi kwenye mfumo wa mkojo hasa hasa kwa wanawake anasababisha UTI. Pia bakteria wanaoishi kwenye uke, mkundu na kuzunguka sehemu za siri wanaweza rahisi kupata njia na kuingia kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha uti. Pia UTI inaweza kusababishwa na baadhi ya magonjwa ya ngono kama gonorrhea, chlamydia na mengine.



Ugonjwa wa uti unaenezwa vipi?
Mtu ataweza kupata UTI kama atafanya chochote ambacho kitaletwa bakteria wanaoishi kwenye utumbo kwenye kwenye nia ya mkojo. Kwa mfano kama wakati wa kuchamba alichamba kwa kuelekea mbele kisha bakteria waliotoka kupitia haja kubwa wakafikia kwenye uume ama uuke, hawa wataingi ndani na kusababisha uti. Si kawaida sana uti kuambukizwa kupitia ngono lakini inaweza kutokea. Na ndio maana inashauriwa ukakojoe baada ya kufanya ngono.



Pia maeneo ya chooni mtu anaweza kupata UTI ila pia hii hutokea mara chache sana na ni kwa wanawake ama kwa wale ambao wanajisaidi kwenye vyoo vya kukaa na si kucuchuchumaa ama kusimama hata hivyo si ahisi kwani lamda kama choo ni kichafu ndipo utapata UTI. Hata hivyo watu hawa wapo hatarini zaidi kupata UTI



1.Kama ulishawahi kupata UTI
2.Kama una kisikari
3.Kama una kiriba tumbo
4.Kama unatumia baadhi ya njia za kidhibiti uzazi kama spermicides au diaphrahm
5.Kama una vijiwe kwenye figo au kibofu na vijiwe hivi vikawa vinazuia mkojo kutoka kwa urahisi.
6.Kama ni mjamzito



Ni zipi dalili za UTI?
1.Maumivu wakati wa kukojoa na wakati mwingine yanafanana na kuhisi kuunguwa
2.Mkojo kuwa mchafu kkama wa mawingi ivi na unatowa harufu kali sana
3.Pia mgonjwa anaweza kuona damu ama kama usaha kwenye mkojo
4.Maumivu chini ya tumbo na mgongo
5.Homa
6.Kupatwa na baridi na hatimaye utetemeka
7.Kichefuchefu
8.Kutapika
9.Kuhisi uchovu sana.



NJIA ZA KUJIKINGA NA UTI
1.Kunywa maji mengi na ya kutosha
2.Dhibiti kisukari kama na kisukari
3.Punguza kula vitu vyenye sukari kwa wingi
4.Unapochamba jifute kuelekea nyuma
5.Punguza michepuko
6.Kojoa baada ya kushiriki tendo la ndoa
7.Kojoa pindi unapohisi mkojo
8.usitumie kondomu isiyo na vilainishi



Dawa ya uti
1.Amoxicillin/augmentin
2.Cetriaxone(rocephin)
3.Trimethoprim/sulfamethoxazole
4.Cephalexin
5.Ciprofloxacin (cipro)
6.Fosfomycin
7.Levofloxacin
8.Nitrofurantoin (mecrodantin)



Dawa kama ciprofloxacin na levofloxacin hutumika kutibu UTI sugu, hivyo si vyema kutumiwa kwa uti ya kawaida. Hata hivyo kabla ya kutumia dawa hizi hakikisha unapata ushauri wa daktari kwanza.





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2375

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 web hosting     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu fangasi kwenye kucha

Makala hiii inakwenda kukueleza dawa za kutibu fangasi kwenye kucha.

Soma Zaidi...
Dawa za fangasi ukeni

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi ukeni

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu fangasi wa kwenye mdomo na kinywa

Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya kupunguza maumivu

Post hii inahusu dawa ya aspirin katika kupunguza maumivu,ni dawa ambayo upunguz maumivu ya Kawaida, kushusha homa na pia usaidia kwenye magonjwa ya moyo hasa kuzuia stroke kama imetokea mda ndani ya masaa ishilini na manne

Soma Zaidi...
Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.

Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia.

Soma Zaidi...