Nitakujuza dalili za UTI na dawa za kutibu UTI. Pia tutaona njia za kujikinga na UTI pamoja na dalili za UTI
Dawa ya UTI na UTI iliyo sugu
Kama ulishawahi kujiuliza masalikama chanzo cha UTI, sababu zake, njia za kukabiliana na uti vipi uti inaenezwa na ni zipi dawa zake. Makala hii ni kwa ajili yako, nimeiandaa kwa ufupi na kwa ufanisi kiasi cha kuweza kukuridhisha kwa majibu ya maswali yako. Kama utakuwa na mawazo zaidi, tuachie maoni yako hapo chini.
Ugonjwa wa UTI ni nini?
UTI ni kifupisho cha maneno Urinary Track Infection. Ni maambukishi na mashambulizi ya bakteria aina ya E.coil katika mfumo wa mkojo. Mwanzoni bakteria huingia kwenye kibofu, figo ama sehemu yeyote kwenye mfumo wa mkojo. Kisha bakteria huyu anaanza kushambulia na kuathiri mfumo huu na ndipo dalili za UTI huanza kuonekana kama maumivu wakati wa kukojoa. Dalili za uti huonekana kuanzia siku 3 mpaka 8 toka kuambukizwa.
Ni zipi sababu za UTI
Sababu kuu za ugonjwa wa UTI ni bakteria aina ya E.coil. Bakteria huyu huishi kwenye utumbo. Sasa endapoa atapata njia kutoka kwenye utumbo kupitia haja kubwa na akaingi kwenye mfumo wa mkojo hasa hasa kwa wanawake anasababisha UTI. Pia bakteria wanaoishi kwenye uke, mkundu na kuzunguka sehemu za siri wanaweza rahisi kupata njia na kuingia kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha uti. Pia UTI inaweza kusababishwa na baadhi ya magonjwa ya ngono kama gonorrhea, chlamydia na mengine.
Ugonjwa wa uti unaenezwa vipi?
Mtu ataweza kupata UTI kama atafanya chochote ambacho kitaletwa bakteria wanaoishi kwenye utumbo kwenye kwenye nia ya mkojo. Kwa mfano kama wakati wa kuchamba alichamba kwa kuelekea mbele kisha bakteria waliotoka kupitia haja kubwa wakafikia kwenye uume ama uuke, hawa wataingi ndani na kusababisha uti. Si kawaida sana uti kuambukizwa kupitia ngono lakini inaweza kutokea. Na ndio maana inashauriwa ukakojoe baada ya kufanya ngono.
Pia maeneo ya chooni mtu anaweza kupata UTI ila pia hii hutokea mara chache sana na ni kwa wanawake ama kwa wale ambao wanajisaidi kwenye vyoo vya kukaa na si kucuchuchumaa ama kusimama hata hivyo si ahisi kwani lamda kama choo ni kichafu ndipo utapata UTI. Hata hivyo watu hawa wapo hatarini zaidi kupata UTI
1.Kama ulishawahi kupata UTI
2.Kama una kisikari
3.Kama una kiriba tumbo
4.Kama unatumia baadhi ya njia za kidhibiti uzazi kama spermicides au diaphrahm
5.Kama una vijiwe kwenye figo au kibofu na vijiwe hivi vikawa vinazuia mkojo kutoka kwa urahisi.
6.Kama ni mjamzito
Ni zipi dalili za UTI?
1.Maumivu wakati wa kukojoa na wakati mwingine yanafanana na kuhisi kuunguwa
2.Mkojo kuwa mchafu kkama wa mawingi ivi na unatowa harufu kali sana
3.Pia mgonjwa anaweza kuona damu ama kama usaha kwenye mkojo
4.Maumivu chini ya tumbo na mgongo
5.Homa
6.Kupatwa na baridi na hatimaye utetemeka
7.Kichefuchefu
8.Kutapika
9.Kuhisi uchovu sana.
NJIA ZA KUJIKINGA NA UTI
1.Kunywa maji mengi na ya kutosha
2.Dhibiti kisukari kama na kisukari
3.Punguza kula vitu vyenye sukari kwa wingi
4.Unapochamba jifute kuelekea nyuma
5.Punguza michepuko
6.Kojoa baada ya kushiriki tendo la ndoa
7.Kojoa pindi unapohisi mkojo
8.usitumie kondomu isiyo na vilainishi
Dawa ya uti
1.Amoxicillin/augmentin
2.Cetriaxone(rocephin)
3.Trimethoprim/sulfamethoxazole
4.Cephalexin
5.Ciprofloxacin (cipro)
6.Fosfomycin
7.Levofloxacin
8.Nitrofurantoin (mecrodantin)
Dawa kama ciprofloxacin na levofloxacin hutumika kutibu UTI sugu, hivyo si vyema kutumiwa kwa uti ya kawaida. Hata hivyo kabla ya kutumia dawa hizi hakikisha unapata ushauri wa daktari kwanza.
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.
Soma Zaidi...kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa zinazofanya kazi ya kupunguza maumivu kwa kawaida dawa hizi ufanya kazi kwa kupitia kwenye mfumo wa fahamu.
Soma Zaidi...Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ushauri kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, kabisa ya kubeba mimba akina Mama na wachumba wanapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi watu ambao wana uwezo wa kutumia vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya watu au makundi yanayoweza kutumia vidonge hivi.
Soma Zaidi...