Nitakujuza dalili za UTI na dawa za kutibu UTI. Pia tutaona njia za kujikinga na UTI pamoja na dalili za UTI
Dawa ya UTI na UTI iliyo sugu
Kama ulishawahi kujiuliza masalikama chanzo cha UTI, sababu zake, njia za kukabiliana na uti vipi uti inaenezwa na ni zipi dawa zake. Makala hii ni kwa ajili yako, nimeiandaa kwa ufupi na kwa ufanisi kiasi cha kuweza kukuridhisha kwa majibu ya maswali yako. Kama utakuwa na mawazo zaidi, tuachie maoni yako hapo chini.
Ugonjwa wa UTI ni nini?
UTI ni kifupisho cha maneno Urinary Track Infection. Ni maambukishi na mashambulizi ya bakteria aina ya E.coil katika mfumo wa mkojo. Mwanzoni bakteria huingia kwenye kibofu, figo ama sehemu yeyote kwenye mfumo wa mkojo. Kisha bakteria huyu anaanza kushambulia na kuathiri mfumo huu na ndipo dalili za UTI huanza kuonekana kama maumivu wakati wa kukojoa. Dalili za uti huonekana kuanzia siku 3 mpaka 8 toka kuambukizwa.
Ni zipi sababu za UTI
Sababu kuu za ugonjwa wa UTI ni bakteria aina ya E.coil. Bakteria huyu huishi kwenye utumbo. Sasa endapoa atapata njia kutoka kwenye utumbo kupitia haja kubwa na akaingi kwenye mfumo wa mkojo hasa hasa kwa wanawake anasababisha UTI. Pia bakteria wanaoishi kwenye uke, mkundu na kuzunguka sehemu za siri wanaweza rahisi kupata njia na kuingia kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha uti. Pia UTI inaweza kusababishwa na baadhi ya magonjwa ya ngono kama gonorrhea, chlamydia na mengine.
Ugonjwa wa uti unaenezwa vipi?
Mtu ataweza kupata UTI kama atafanya chochote ambacho kitaletwa bakteria wanaoishi kwenye utumbo kwenye kwenye nia ya mkojo. Kwa mfano kama wakati wa kuchamba alichamba kwa kuelekea mbele kisha bakteria waliotoka kupitia haja kubwa wakafikia kwenye uume ama uuke, hawa wataingi ndani na kusababisha uti. Si kawaida sana uti kuambukizwa kupitia ngono lakini inaweza kutokea. Na ndio maana inashauriwa ukakojoe baada ya kufanya ngono.
Pia maeneo ya chooni mtu anaweza kupata UTI ila pia hii hutokea mara chache sana na ni kwa wanawake ama kwa wale ambao wanajisaidi kwenye vyoo vya kukaa na si kucuchuchumaa ama kusimama hata hivyo si ahisi kwani lamda kama choo ni kichafu ndipo utapata UTI. Hata hivyo watu hawa wapo hatarini zaidi kupata UTI
1.Kama ulishawahi kupata UTI
2.Kama una kisikari
3.Kama una kiriba tumbo
4.Kama unatumia baadhi ya njia za kidhibiti uzazi kama spermicides au diaphrahm
5.Kama una vijiwe kwenye figo au kibofu na vijiwe hivi vikawa vinazuia mkojo kutoka kwa urahisi.
6.Kama ni mjamzito
Ni zipi dalili za UTI?
1.Maumivu wakati wa kukojoa na wakati mwingine yanafanana na kuhisi kuunguwa
2.Mkojo kuwa mchafu kkama wa mawingi ivi na unatowa harufu kali sana
3.Pia mgonjwa anaweza kuona damu ama kama usaha kwenye mkojo
4.Maumivu chini ya tumbo na mgongo
5.Homa
6.Kupatwa na baridi na hatimaye utetemeka
7.Kichefuchefu
8.Kutapika
9.Kuhisi uchovu sana.
NJIA ZA KUJIKINGA NA UTI
1.Kunywa maji mengi na ya kutosha
2.Dhibiti kisukari kama na kisukari
3.Punguza kula vitu vyenye sukari kwa wingi
4.Unapochamba jifute kuelekea nyuma
5.Punguza michepuko
6.Kojoa baada ya kushiriki tendo la ndoa
7.Kojoa pindi unapohisi mkojo
8.usitumie kondomu isiyo na vilainishi
Dawa ya uti
1.Amoxicillin/augmentin
2.Cetriaxone(rocephin)
3.Trimethoprim/sulfamethoxazole
4.Cephalexin
5.Ciprofloxacin (cipro)
6.Fosfomycin
7.Levofloxacin
8.Nitrofurantoin (mecrodantin)
Dawa kama ciprofloxacin na levofloxacin hutumika kutibu UTI sugu, hivyo si vyema kutumiwa kwa uti ya kawaida. Hata hivyo kabla ya kutumia dawa hizi hakikisha unapata ushauri wa daktari kwanza.
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa za fangasi na matumizi yake kwa kutumia dawa ya fluconazole kama dawa mojawapo ya fangasi.
Soma Zaidi...Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa.
Soma Zaidi...kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.
Soma Zaidi...