hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi
DAWA YA FANGASI
Fangasi ni katika magonjwa yanayoathiri watu wengi sana. Fangasi wanaweza kuathiri ngozi, nywele na kucha. Unaweza kujitibu fangasi kwa kwenda duka la dawa na kununua dawa bila ya kuhitaji usimamizi maalumu wa daktari ila hii ni kwa dawa za fangasi za kupaka. Za kunywa na sindano hakikisha unapata ushauri wa daktari kwanza. Kumbuka matibabu ya fangasi yanategemea aina ya fangasi wanaokusumbuwa.
Aina za fangasi
1.Fangasi wa kwenye kucha
2. Fangasi wa Mapunye
3. Fangasi aina ya candida
4. Fangasi wa Mdomoni na kooni
5. Fangasi wa kwenye uke
6. Fangasi wanaoshambulia mfumo wa damu na ogran kama moyo, figo n.k
7. Fangasi aina ya Blastomyces
8. Fangasi wa sehemu za siri
Aina za dawa za kitubu fangasi.
Dawa za kutibu fangasi nazo zimegawanyika kama:-
1.Dawa za kupaka na kupulizia
2.Dawa za kumeza majimaji na vidonge
3.Sindano
4.Dawa za kuweka ili zimumunyike, hizi sana huwekwa kwenye uke.
Orodha ya dawa za fangasi
1.Clotrimazole
2.Econazole
3.Miconazole
4.Terbinafine
5.Fluconazole
6.Ketokonazole
7.Amphotericin
Kazi za dawa za fangasi.
Dawa hizi zina kazi kuu 2 nazo ni:-
1.Kuuwa fangasi
2.Kuzuia fangasi kuzaliana na kukuwa.
Athari zinazoweza kutokea wakati wa kutumia dawa za fangasi.
Haya ni matokea yanayoweza kutokea unapoanza kutumia dawa hizi. Si jambo la kuogopa.
1.Miwasho
2.Kujihisi ovyoovyo
3.Kuharisha
4.Ukurutu
5.Unaweza kupata aleji
Umeionaje Makala hii.. ?
Zipo dawa nyingi ambazo hufahamika katika kutibu fangasi kwenye mdomo ama kinywa. Miongoni mwa dawa hizo hapa nitakuletea baadhi yao. kama wewe pia unasumbuliwa na fangasi wa mdomo basi post hii itakusaidi sana.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na maumivu ya hedhi
Soma Zaidi...Maumivu ya mgongo hutokea sana kwa wajawazito. Ijapokuwa ni hali ya usumbufu sana ila hakikisha hautumii madawa kiholela kutoka maduka ya dawa ama miti shamba. Kwani ukikisea kidogobinawezabhatarisha afya ya mtoto
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo
Soma Zaidi...Digoxin ni nini? Digoxin inatokana na majani ya mmea wa digitalis. Digoxin husaidia kufanya mapigo ya moyo kuwa na nguvu na kwa mdundo wa kawaida zaidi. Digoxin hutumiwa kutibu kushindwa kwa moyo. Digoxin pia hutumiwa kutibu mpapatiko wa atiria, ugonjw
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya theophylline ni dawa inayofanya kazi kwenye mfumo wa upumuaji.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya paracetamol katika kutuliza maumivu, ni Aina ya dawa ambayo utumiwa sana katika kutuliza maumivu kwa wagonjwa.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...