kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka
Dawa ya fangasi uumeni
Fangasi wanaweza kuathiri watu wa marika yeto, pia kuathiri maeneo mengi ya mwili. Lakini hapa nitakuletea fangasi wanaoathiri uume, sababu zao, dalili zao na dawa inayotumika kutibu fangasi hawa wa kwenye uume.
Dalili za fangasi wa kwenye uume
1.Upele na ukurutu kwenye uume
2.Vidoadoa vyeupe kwenye uume
3.Uume kuwa na umajimaji kwenye ngozi yake
4.Kwa ambao hawajatahiriwa kutakuwa na uchafu mweume kwenye ngozi ya govi
5.Miwasho kwenye uume na kuhisi kuunguwa
Nini sababu ya fangasi hawa wa kwenye uume?
Fangasi wa kwenye uume husababishwa na aina ya fangasi inayojulikana kama candida. fangasi hawa wanapenda sana maeneo yenye majimaji. Hususan sehemu za siri ambapo ndipo panakuwa na majimaji mengi. Fangasi hawa wanaweza kuambukizwa kwa kupitia ngono. Usafi wa sehemu za siri ukawa ni mbovu hali inaweza kuwa mbaya zaidi.
Watu walio hatarini kupata fangasi wa uumeni
1.Watu walio na Uchafu wa mwili hasa sehemu za siri
2.Watu walio na kisukari
3.Watu wenye viribatumbo (kitambi)
4.Watu wenye kinga dhaifu kama waathirika wa VVU ama walioanza matibabu ya saratani
5.Watu ambao hawajatahiriwa
Dawa zinazotumika kutibu fangasi wa uumeni
Fangasi hawa wanaweza tu kutibiwa kwa dawa za fangasi za kupaka yaani za losheni kama:-
1.Miconazole (lotrimin AF, Ceruex, Desenex, Ting Antifungal)
2.Imidazole (canesten, Selezen)
3.Clotrimazole (Lotrimin AF, Anti-Fungal, Cruex, Desenex, Lotrimin AF Ringworm)
Pia endapo hali itaendelea, mgonjwa anaweza kutumia dawa za kumeza, baada ya kupata ushauri kwa daktari. Dawa hizi ni kama:-
1.Fluconazole (Diflucan) hii ni ya kumeza pia hutumika pamoja na ya kupaka inayoitwa hydrocortisone cream. Tiba hii hasa ni kwa wale ambao hali imekuwa mbaya sana (balanitis).
TIBA MBADALA ZA KUTIBU FANGASI WA UUMENI
1.Mafuta ya majani ya chai
2.Kitunguu thaumu
3.Siki ya epo
4.Mafuta ya nazi
5.Mafuta ya karafuu
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi, ama tuachie maoni yako hapo chini.
Umeionaje Makala hii.. ?
Digoxin ni nini? Digoxin inatokana na majani ya mmea wa digitalis. Digoxin husaidia kufanya mapigo ya moyo kuwa na nguvu na kwa mdundo wa kawaida zaidi. Digoxin hutumiwa kutibu kushindwa kwa moyo. Digoxin pia hutumiwa kutibu mpapatiko wa atiria, ugonjw
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...