Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.

Dawa za kutibu magonjwa ya moyo.

1. Kwanza kabisa kabla hatujaanza kuchambua dawa moja baada ya nyingine tunapaswa kufahamu kabisa kuhusu magonjwa ya moyo, ambapo kwa lugha ya kitaalamu magonjwa ya moyo huitwa cardiac failure , magonjwa ya moyo ni hali ambayo utokea kama moyo umeshindwa kufanya kazi yake vizuri kwa mfano moyo kushindwa kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

2. Kwa kawaida kuna dalili mbalimbali ambazo zinaweza kujitokeza kama moyo haufanyi kazi vizuri na dalili hizi ni pamoja na uchovu wa mara kwa mara, kushindwa kupumua vizuri, na wakati mwingine kifua kubana , kukonda kusiko kwa kawaida hata kama mgonjwa anakuwa anatumia chakula na dalili nyingine zinaweza kujitokeza kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mwingine.

 

3. Kutokana na kuwepo kwa magonjwa ya moyo kuna dawa mbalimbali ambazo utumika kutibu magonjwa ya moyo na lengo la dawa hizi ni kuhakikisha kwamba moyo unafanya kazi yake ipasavyo na kuhakikisha kwamba maumivu mbalimbali hayatokei kwa mgonjwa na pia dawa hizo zinatofautiana kutoka kwa dawa moja kwenda kwa nyingine kadri ya tatizo lilivyo.

 

4. Kuna dawa za moyo ambazo usaidia kama presha iko juu kitendo hiki kwa kitaalamu huitwa high blood pressure, hali hiyo uitwa magonjwa ya moyo kwa sababu kuna kipindi moyo unatumia nguvu kubwa kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili, hali hii ya moyo kutumia nguvu kusukuma damu utokea kwasababu ya mishipa ya damu kuwa nyembamba na kusababisha damu kutoweza kufika sehemu mbalimbali za mwili kusababisha moyo kutumia nguvu hali inayosababisha shinikizo la damu. Kwa hiyo kuna dawa za kutibu hali hiyo ya shinikizo la damu.

 

5. Pia kuna dawa za moyo ambazo usaidia kwenye matibabu ya kupambana  na shinikizo kali la damu ambalo usababisha kiharusi, kwa kitaalamu huitwa stroke na myocardial infarction, kwa kawaida tunafahamu kwamba iwapo shinikizo la damu limekuwa sugu usababisha kiharusi ,kwa hiyo pia tutaweza kuona dawa za kutibu hali hiyo.

 

6 pia kuna dawa vile vile ambazo usaidia kutibu hali ya presha kuwa chini, kuna  kipindi baada ya presha kubaki kwenye hali yake ya kawaida yenyewe inashuka hali inayosababisha matatizo kwa mgonjwa kama matibabu hayajatolewa, kwa hiyo tutaweza kuona dawa za kutibu hali hiyo.

 

7. Pamoja na kujua aina mbalimbali za magonjwa ya moyo tutaona jinsi dawa zinazotumika kutibu magonjwa ya moyo jinsi zinavyofanya kazi , kwanza dawa hizi uondoa chumvi kwenye moyo na maji yaliyozalishwa kwenye moyo  na kusababisha moyo kuwa kawaida na kuweza kufanya kazi vizuri,kwa hiyo ili moyo ufanye kazi unahitaji chumvi na maji sawia  yaani viwe vya kawaida, kwa hiyo maji yakiwa mengi kuzidi na chumvi ikizidi kwenye moyo ni hatari sana.

 

8. Pia dawa hizo usaidia kupandisha presha kama imeshuka na kuiweka kwenye hali ya kawaida, dawa ambayo kwa kawaida utumika uhakikisha kwamba presha hatishuki ovyo ovyo.

 

9. Pia dawa hizo upanua mishipa ya damu kama ni midogo na kusababisha damu kuweza kupita vizuri na kwenda kwenye sehemu mbalimbali za mwili na kushusha presha na ikiwa ya kawaida.

 

10. Baada ya kufahamu kazi za dawa hizi za magonjwa ya moyo na kufahamu magonjwa mbalimbali ya moyo ni vizuri kufahamu kwamba kila ugonjwa wa moyo huwa na dawa zake maalum ambazo utumika kutibu ugonjwa huo kwa hiyo ni vizuri kabisa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya.

 

11. Kwa hiyo baada ya kufahamu tofauti za magonjwa ya moyo ni vizuri kupima kwanza ili kufahamu kwamba upo kwenye kundi gani na kupewa dawa kadri ya tatizo.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1802

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Faida za dawa za NMN

Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazopunguza maumivu

Post hii inahusu zaidi dawa zinazofanya kazi ya kupunguza maumivu kwa kawaida dawa hizi ufanya kazi kwa kupitia kwenye mfumo wa fahamu.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo

Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya haloperidol katika matibabu ya akili

Post hii inahusu dawa ya haloperidol katika matibabu ya magonjwa ya akili, ni mojawapo ya dawa ambayo utumiwa na wagonjwa ambao wamechananyikiwa.

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...
IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE

Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.

Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye ngu

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya maumivu aina ya indomethacin

Post hii inahusu zaidi dawa ya kutibu au kutuliza maumivu, kwa majina huiitwa indomethacin ni dawa inayotumika kutuliza maumivu ya Kawaida.

Soma Zaidi...
dawa ya minyoo, dalili za minyoo na sababu na vyanzo vya minyoo

MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...