image

Fahamu dawa za 5-fluorouracil,Tegafur na uracili

Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.

Fahamu kuhusu dawa za 5- fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa,

1. Hizi ni dawa ambazo upatikana kwenye kundi la antimetabolite, dawa hizi usaidia kupambana na kansa za kwenye matiti, kansa ya damu ,kansa za kwenye kizazi na aina nyingine kadri ya wataalamu wa afya, dawa hizi ufanya kazi ya ya kuingilia nuclear ambayo kwa kitaalamu huitwa DNA na kuhakikisha kwamba seli ambazo hazihiitajiki zinaacha kabisa kuendelea kuzalishwa na kukomaa kabisa.

 

2. Kwa matumizi ya dawa hizi za 5-fluoro uracili, Tegafur na uracili usaidia kuondoa kabisa au kufubaisha zile seli za kansa ambazo zilikuwa zimekwisha zalishwa tayari na kuhakikisha kwamba zinapungua kabisa na haziendelei kuzalishwa , kwa watumiaji wazuri wa dawa na wale waliowahi kuanza matibabu hasa wa kansa ngazi ya kwanza na ya pili,wanaweza kupona ugonjwa huu.

 

3. Katika matumizi ya dawa hizi mgonjwa anapaswa kula mlo kamili na pia kula wingi wa matunda kwa sababu dawa hizi zina tabia ya kumaliza mgonjwa nguvu na pia kumbuka kuna baadhi ya seli ambazo tayari zimeshaanza kushambuliwa,na zingine zimeharibiwa na dawa kwa sababu kama dawa inatumika haijarishi aina ya seli  bali ufyeka seli zote, kwa hiyo kwa mgonjwa huyu matunda na mlo kamili ni lazima.

 

4. Vile vile dawa hizi zina maudhui madogo madogo ambayo ujitokeza na maudhi haya utofautiana kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda mwingine,na maudhi hayo ni kama vile vidonda kwenye midomo, kichefuchefu na kutapika,uchofu na kuishiwa nguvu, hamu ya kula kuwa ndogo hali ambayo usababisha mgonjwa kukonda kwa hiyo uangalizi wa mgonjwa huyu ni lazima hasa kwa upande wa chakula kwa sababu uchagua vyakula kwa hiyo anapaswa kupewa vyakula anavyovipenda.

 

5. Na kwa matumizi ya mda mrefu dawa hizi  usababisha nywele kuondoka na kubadilika kusiko kwa kawaida vile  vile kwa matumizi ya dawa hizi mgonjwa anaweza pia kuwa na viupele kwenye ngozi kwa hivyo usafi ni kawaida kwa mgonjwa huyu ili kuweza kuepukana na vi upele na kama mgonjwa yuko kwenye umri wa kuzaa anaweza kuwa mgumba kwa matumizi ya dawa hizi kwa mda mrefu na pengine hamu ya tendo la ndoa kupungua,

 

6. Kwa sababu ya kuwepo kwa maudhi madogo madogo pengine maudhui haya yanaweza kugeuka kuwa kama ugonjwa kwa hiyo matibabu ya matokeo ya dawa nayo yanatakiwa kwa mfano kama mgonjwa hana hamu ya kula ni vizuri kupewa dawa ya hamu ya kula, au kama mgonjwa anaharisha na kutapika ni vizuri kabisa kupewa dawa za kutapika na kuharisha au kama mgonjwa ana shida ya kuwa na choo kigumu ni vizuri kuwepo kwa dawa za kusaidia tatizo hilo, kwa hiyo matibabu ya matokeo ya dawa ni lazima ili kuweza kuhakikisha mgonjwa anaendelea vizuri.

 

7. Vile vile kama maudhui yamekuwa na matokeo mabaya ni vizuri kumbadilishia mgonjwa dawa na kumpatia dawa ambayo atatumia bila shida au kwa kuwepo maudhi madogo madogo ambayo hayamletei shida, pamoja na kuwepo kwa maudhi hayo pia dawa hizi hazipatiswi kutumiwa na watu ambao wana aleji au mzio wa 5-fluorouracil, Tegafur na uracili , kwa sababu kuna dawa nyingine ambazo wanaweza kutumia ili kuweza kuendelea na matibabu.

 

8. Vile vile dawa hizi hazitumiki kiholela zinapaswa kutumika kwa utaratibu wa wataalamu wa afya na pia wagonjwa wa kansa ni vizuri kabisa kupewa uangalizi wa karibu kwa hiyo sio vizuri kabisa kumeza dawa hizi kiholela.

 

9. Vile vile jamii inapaswa kufahamu kwamba ugonjwa huu wa kansa ya matiti,kansa ya kizazi na pia kansa  ya damu zinatibika kabisa kwa kutumia dawa hizi za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili, kitu cha kwanza cha kufahamu ni kwamba mgonjwa anapaswa kufuata utaratibu wote wakati wa matibabu na pia kutunzwa vizuri na kupewa chakula cha kutosha na vilevile mgonjwa anapaswa kuwahi matibabu mapema kabisa , yaani kuanza matibabu kwenye ngazi ya kwanza na ya pili na pia mgonjwa akiongezea na matunzo pamoja na kumtia moyo kwa upande wa kansa ngazi ya kwanza na ya pili mgonjwa anaweza kupona .

 

10. Vile vile jamii inapaswa kuelezwa wazi kwamba kwa wagonjwa wanaoanza dawa wamechelewa wakiwa kwenye ngazi ya tatu na ya nne ni vigumu kupona haraka na kwa sababu ya kuwepo kwa matokeo ya dawa ambayo pengine ni makali kama kuharisha na kutapika , kupungua kwa seli mwilini na matokeo mengine kama tulivyoona hapo nyuma.kwa hiyo w agonjwa wa ngazi ya tatu na ya nne kupona kwao ni vigumu na kwa hivyo baadhi yetu wakiona dalili yoyote ambayo siyo ya kawaida ni vizuri, kama vile na uvumbe ambayo hayaeleweki ni vizuri kabisa kuwahi hospitali ili kama ni kansa matibabu yaanze mapema.

 

11. Vile vile jamii inapaswa kuachana na mila na desturi za kuogopa ugonjwa huu wa kansa na kwa wakati mwingine wengine wanafikia kiwango cha kuwatelekeza wagonjwa wao hospitalini  na kwa wakati mwingine wakihofia kuambukizwa na ugonjwa huo na wengine wanafikia kiwango cha kuamini kwamba mtu ambaye ana kansa hawezi kupona , kwa hiyo wafahamu kwamba wagonjwa wa kansa wakiwahi matibabu wanaweza kupona kabisa na kurudia hali zao za kawaida, ila shida watu wanashindwa kuwahi matibabu hali inayoendelea kuleta shida zaidi.

 

12. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa hudumia wagonjwa wa kansa na kuepuka na tabia ya kuwatenga kwa sababu kansa haijathibitishwa kwamba inaenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine na kwa hiyo wagonjwa wanapaswa kuwekwa kutunzwa vizuri na kuwekwa kwenye hali ya kawaida kwani ni kama ugonjwa mwingine.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 545


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria
Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.
Post hii inahusu zaidi dawa aina ya ketoconazole ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye koo. Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu. Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi. Soma Zaidi...

Dawa inaitwa koflame ukitumia inashida kwa mama mjamzito? Maumivu ya mgongo na nyonga zinasumbua
Maumivu ya mgongo hutokea sana kwa wajawazito. Ijapokuwa ni hali ya usumbufu sana ila hakikisha hautumii madawa kiholela kutoka maduka ya dawa ama miti shamba. Kwani ukikisea kidogobinawezabhatarisha afya ya mtoto Soma Zaidi...

Fahamu Dawa inayotibu minyoo iitwayo albenza (albendazole)
Albenza (albendazole) hutumika kutibu magonjwa ya minyoo ya ndani ikiwa ni pamoja na maambukizi ya minyoo ya tegu. Albenza inafanya kazi kukomesha kuenea kwa maambukizo ya minyoo kwenye chanzo, na kukata chanzo chao cha nishati, na hivyo kuzuia kuenea k Soma Zaidi...

Tiba mbadala za vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya ALU au kwa lugha nyingine ni dawa ya mseto
Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida. Soma Zaidi...

Dawa za kutibu ugonjwa wa macho
Somo Hili linakwenda kukuletea dawa za kutibu ugonjwa wa macho Soma Zaidi...

Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital
Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa. Soma Zaidi...

Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo
Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya Acetohexamide
Post hii inahusu zaidi dawa ya Acetohexamide kwa matibabu ya sukari, kama tulivyoona katika post iliyopita kwamba kuna kipindi ambacho kongosho linatoa insulini lakini seli haziko tayari kupokea hiyo insulini. Soma Zaidi...