DAWA YA MAPUNYE
Matibabu ya mapunye inategemea ni wapi mapunjye yapo. Mapunye yanaweza kuota kichwani, mikononi, mgongoni na maeneo mengine. Pia matibabu yatategemea ni kiasi gani mmtgu ameathiriwa na hayo mapunye. Mapunye yanayweza kibiwa na dawa za kupaka kama losheni za fangasi na poda zake. Miongoni mwazo ni:-



Dawa ya mapunye ya kupaka:
1.Clorimazole
2.Miconazole
3.Terbinafine
4.Ketoconazole



Endamp dawa hisi hazitaweza kumaliza mapunye, daktari anaweza kukuandikia dawa za kumeza amasindano. Katu dawa hizi usimeze kiholela bila ya kupata ushauri wa daktari. Dozi ya dawa hizi inaweza kwisha ndani ya mwezi mmoja ama ikaendelea mpaka miezi mitatu. Dawa hizi za mapunye za kumeza ni pamoja na:-



Dawa ya mapunye ya kumeza.
1.Terbinafine. Dawa hii inaweza kunywewa ndani ya wiki nn4. hata hivyo inaweza kukuletea mabadiliko kwenye mwili wako kama kichefuchefu, kuhara, kukosa choo na ukurutu. Si lazima mabadiliko haya uyaone kuna wengine hawaoni chochote.



2.Griseofulvin. Dawa hii inaweza kutumiwa kuanzia wiki 8 mpaka 10. Pia inaweza lupatikana katika mtindo wa kupulizia. Nayo inaweza kulete mabadiliko kama kuhara, kutapika, kichefuchefu, maumivu ya kichwa na kukosa choo. Dawa hii sio salama kwa wajawazit, ama kama upo katika harakati za kubeba mimba ama kama unanyonyesha.



3.Itraconazole. Dawa hii humezwa ndani ya siku 7 mpaka 15. si nzuri dawa hii kutumiwa na watoto wadogo, wazee na walio na maradhi ya ini. Dawa hii pia inaweza kukuletea mabadiliko kama maumivu ya kichwa, kichefuchefu, kutapika, kuhara na kukosa choo.



Njia za kujilinda dhidi ya mapunye.
1.Osha mikono yako kila unapogusa punye
2.Osha nguozako za kuvaa, kutandika na kujifunika na taulo.
3.Oga kila unapotoka kufanya kazi
4.Kama upo karibu na wanyama kama mbwa na paka hakikisha wapo salama na mapunye.
5.Usishiriki nguo zako na mwenye mapunye.