Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.
1. Pyrantel pamoate ni aina mojawapo ya dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo ukaa kwenye utumbo mdogo yaani kwa kitaalamu kwenye intestinal nematode hiyo ndiyo kazi yake na pia inaweza kufanya kazi kama dawa za Albendazole na mebendazole kwa sababu ya kupambana na aina ya minyoo inayotibiwa na na dawa hizo ambayo ni hookworm na pinworn.
2. Dawa hii pia ipo kwenye mfumo wa vidonge na pia utafunwa na kumezwa bila maji na pia utumika kabla ya kula kitu chochote ili kuweza kukabiliana vizuri na minyoo ambayo iko tumboni, kwa matumizi yake au namna ya kutumia ni kwa kadiri ya maagizo ya daktari au mtaalamu wa afya.
3. Pia dawa hii utumika kwa watu wote wakubwa na wadogo isipokuwa watoto wadogo chini ya miaka miwili na akina Mama wajawazito wenye mimba changa hawapaswi kutumia dawa hii kwa kuepukana na mimba kutoka, kwa hiyo wajawazito wanapaswa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya hasa wakiwa kliniki na sio kununua dawa na kutumia kwa sababu wanaweza kujiletea matatizo makubwa.
4. Pia dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika, kizunguzungu, kuchoka mara kwa mara kwa watumiaji wa dawa za pyrantel pamoate wakiona dalili kama hizi ni vema kabisa kufahamu kwamba ni matokeo ya dawa na pia hali ikiwa mbaya ni vema kabisa kuwaona wataalamu wa afya.
5. Pia jamii inapaswa kuelewa kwamba dawa hii haitumiki kiholela ni kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya na kujua matumizi yake, endapo ikitumika visivyo inaweza kuleta matokeo mabaya kwa watumiaji hasa wajawazito na watoto chini ya miaka miwili, kwa hiyo kwa upande wa wajawazito ni vizuri kufuata masharti ya kliniki hasa mimba ikiwa changa katika matumizi ya dawa na pia mtoto anapaswa kupelekwa kliniki ikitokea kama anaumwa ili apewe dawa zake.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya fluconazole ni dawa ya kutibu fangasi za aina au za sehemu mbalimbali,
Soma Zaidi...MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya carvedilo katika matibabu ya magonjwa, ni mojawapo ya dawa kwenye kundi la beta blockers na pia uhusika katika matibabu ya magonjwa ya moyo kama nyingine.
Soma Zaidi...Post hii inahusu dawa ya kaoline katika kutibu au kuzuia kuharisha ni dawa ambayo imependekezwa kutumiwa hasa kwa wale walioshindwa kutumia dawa ya loperamide.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Soma Zaidi...