Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate

Post hii inahusu zaidi dawa ya pyrantel pamoate ni dawa ambayo usaidia kutibu minyoo ambayo kwa kawaida ukaa kwenye utumbo mdogo.

Fahamu kuhusu dawa ya pyrantel pamoate.

1. Pyrantel pamoate ni aina mojawapo ya dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo ukaa kwenye utumbo mdogo yaani kwa kitaalamu kwenye intestinal nematode hiyo ndiyo kazi yake na pia inaweza kufanya kazi kama dawa za Albendazole na mebendazole kwa sababu ya kupambana na aina ya minyoo inayotibiwa na na dawa hizo ambayo ni hookworm na pinworn.

 

2. Dawa hii pia ipo kwenye mfumo wa vidonge na pia utafunwa na kumezwa bila maji na pia utumika kabla ya kula kitu chochote ili kuweza kukabiliana vizuri na minyoo ambayo iko tumboni, kwa matumizi yake au namna ya kutumia ni kwa kadiri ya maagizo ya daktari au mtaalamu wa afya.

 

3. Pia dawa hii utumika kwa watu wote wakubwa na wadogo isipokuwa watoto wadogo chini ya miaka miwili na akina Mama wajawazito wenye mimba changa hawapaswi kutumia dawa hii kwa kuepukana na mimba kutoka, kwa hiyo wajawazito wanapaswa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya hasa wakiwa kliniki na sio kununua dawa na kutumia kwa sababu wanaweza kujiletea matatizo makubwa.

 

4. Pia dawa hii huwa na maudhi madogo madogo kama vile maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo, kichefuchefu na kutapika, kizunguzungu, kuchoka mara kwa mara kwa watumiaji wa dawa za pyrantel pamoate wakiona dalili kama hizi ni vema kabisa kufahamu kwamba ni matokeo ya dawa na pia hali ikiwa mbaya ni vema kabisa kuwaona wataalamu wa afya.

 

5. Pia jamii inapaswa kuelewa kwamba dawa hii haitumiki kiholela ni kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya na kujua matumizi yake, endapo ikitumika visivyo inaweza kuleta matokeo mabaya kwa watumiaji hasa wajawazito na watoto chini ya miaka miwili, kwa hiyo kwa upande wa wajawazito ni vizuri kufuata masharti ya kliniki hasa mimba ikiwa changa katika matumizi ya dawa na pia mtoto anapaswa kupelekwa kliniki ikitokea kama anaumwa ili apewe dawa zake.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1050

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 web hosting    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ushauri kabla ya kubeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi ushauri kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, kabisa ya kubeba mimba akina Mama na wachumba wanapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)

Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin,

Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi uumeni

kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka

Soma Zaidi...
Kazi ya Dawa ya salbutamol

Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.

Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye ngu

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu kiungulia

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya mucolytic dawa ya kutibu kikohozi

Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto.

Soma Zaidi...
Dawa ya Panadol au paracetamol katika kutuliza maumivu

Posti hii inahusu zaidi kazi ya paracetamol katika kutuliza maumivu, ni Aina ya dawa ambayo utumiwa sana katika kutuliza maumivu kwa wagonjwa.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu minyoo

Zijuwe aina za minyoo na tiba yake. Dawa 5 za kutibu minyoo ya aina zote

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kuzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya cloxacillin ambayo Iko kwenye kundi mojawapo la penicillin ambalo uzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria.

Soma Zaidi...