image

Fahamu kuhusu dawa ya propranolol ambayo hutibu magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya propranolol katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii ipo kwenye kundi la beta blockers na ufanya Kazi mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo.

Fahamu kuhusu dawa ya propranolol.

1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba hii ni dawa inayotokana na kundi la beta blockers, aina hii ya dawa ya propranolol usaidia kama kuna dalili yoyote ya kuganda damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili hasa kwenye ubongo, tunafahamu kabisa kwamba kama kuna tatizo kwenye moyo usafirishaji wa damu huwa ni wa shida hali inayosababisha damu kutofika katika sehemu mbalimbali au pengine mzunguko wa damu kusimama kabisa au pengine damu kuganda, kwa hiyo kama kuna tatizo la damu kwenye ubongo dawa hii usaidia sana.

 

2. Dawa hii ufanya kazi ya kuhakikisha kwamba kuna damu ya kutosha kwenye ubongo kwa kupita kwenye system ya mzunguko wa damu uliopo kwenye ubongo na kuhakikisha kwamba damu inasafirishwa vya kutosha na shughuli za kwenye ubongo zinakuwa sawa kabisa, tunafahamu kwamba kuwepo kwa chumvi nyingi kwenye mfumo wa mzunguko wa damu ni tatizo kwa hiyo na dawa hii upunguza kiwango cha chumvi kwenye mfumo wa damu na hali huwa kawaida tu.

 

3. Pamoja na kazi nzuri ya dawa hii kuna wakati maudhi madogo madogo utokea hasa kwa watumiaji wa mda mrefu na wale wanaoanza kutumia dawa hii, maudhui hayo ni pamoja na mapigo ya moyo kuwa ya chini sana, macho kuwa makavu bila ya maji maji au pengine yanakuwepo kidogo, nywele zinaisha au zinanyonyoka kama wale watumiaji wa mionzi, kichefuchefu na kutapika, udhaifu wa mwili na uchovu wa mara kwa mara.

 

4. Kama maudhi haya ni kidogo kwa wanaoanza kutumia dawa wavumilie kwa sababu uisha taratibu na baadae mwili uweza kuzoea dawa na kama maudhi haya yakiendelea na kuleta matatizo makubwa kama kutapika mara kwa mara uchovu unaokufanya hata usifanye kazi yoyote nywele kuisha karibu zote kichwani, ongea na wataalamu wa afya ili uweze kubadilishiwa dawa kadri ya tatizo la mgonjwa, kwa sababu maudhui madogo madogo mengine yanaweza kufanya mtumiaji wa dawa kupata matatizo badala ya kupona.

 

5. Vile vile watumiaji wa dawa hii wanaweza kuwa na matatizo kwenye ngozi na wengine wanaweza kuona kwamba ni kama aleji hivi yaani kwa watumiaji hasa wale wa mwanzoni wanaweza kuwa na vipengele vidogo vidogo kwenye miili yao, kuwashwa na kujikuna hali inayosababisha mgonjwa pengine kuwa na wasiwasi, na pengine vidonda hivyo vinaweza kueneza mwili mzima na kuwepo kwa maji maji, kwa hiyo hali hiyo ikiendelea ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kutibu hivyo vidonda huku mgonjwa akiendelea na dawa lakini hali hiyo ikijitokeza mara kwa mara ni vizuri kubadilishiwa dawa.

 

6. Vile vile dawa hii ya propranolol ina tabia ya kusababisha kuwepo kwa shida wakati wa upumuaji kwa hiyo utakuta mtumiaji wa dawa anapumua kama mtu mwenye pumu hasa kwa wanaoanza, kwa hiyo ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya endapo hali hii inaendelea kila mara ila kwa watumiaji wa dawa wa mwanzoni hali hii uwepo na baadae upitea lakini ikiendelea ni vizuri kabisa kubadilishiwa dawa.

 

7. Katika matumizi ya dawa hii ya propranolol usababisha kubadilisha kiwango cha sukari mwilini, ndio maana kwa wagonjwa wa matatizo ya moyo wanapaswa kupima sukari mara kwa mara,kwa sababu katika matumizi ya dawa nyingine umaliza sukari mwilini hasa dawa hii ya propranolol ina tabia hiyo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kwa watumiaji wa dawa hii ya propranolol wale vyakula vyenye sukari kabla na baada ya kutumia au ikiwezekana  kupima sukari mara kwa mara ili kupunguza tatizo la kuishiwa na sukari na pia kupima sukari mara kwa mara ni lazima kabisa.

 

8. Pia watumiaji wa dawa hii ya propranolol mara nyingi miguu yao na mikono huwa ya baridi hasa kwa watumiaji wa mwanzoni na baadae hali huwa ya kawaida, kwa hiyo watumiaji wakihisi hali hiyo hawapaswi kuogopa bali waone ni hali ya kawaida tu,na pengine wanapata shida wakati wa kulala, pengine usingizi hawaupati au wanasinzia wanashutuka shutuka shutuka au kwa wakati mwingine wanakuwa wanajigeuza sana wakati wa kulala kwa ujumla wanakuwa na maangaiko wakati wa kusinzia.

 

9. Kwa wale ambao hawasinzii kabisa na kwa mda mrefu wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya ili waweze kubadilishiwa dawa mara moja kwa sababu kitendo cha kukosa usingizi ni kibaya mno na uweza kuleta matatizo makubwa zaidi kuliko yaliyokuwepo,na sio kwa usingizi tu ila maudhi madogo madogo yakiwa ya mda mrefu ni vizuri kuyariport na kupata msaada mapema kuliko kuongeza matatizo.

 

10. Pia dawa hii ya propranolol inawezekana kuleta matatizo kwenye misuli ambayo kwa kitaalamu huitwa muscle cramp au kwa wakati mwingine miguu kulegea na pengine kuchoka baada ya kutembea kwa mda mfupi, au kwa wakati mwingine uzito kuongezeka ghafla unakuta mtu amenenepeana ghafla na hapo misuli umelemewa na kwa hiyo kutembea huwa shida kwa sababu mtumiaji wa dawa uchoka mara kwa mara na kuwepo na maumivu kwenye sehemu mbalimbali za mwili hasa kwenye jointi.

 

11. Kwa hiyo tunaona dawa hii ya propranolol ina maudhi madogo madogo mengi hasa kwa watumiaji wa mwanzo endapo maudhi haya hayatatibika mapema yanaweza kuleta magonjwa au matatizo zaidi kwa watumiaji kwa hiyo ni vizuri kabisa ikitokea hali imebadilika kwa watumiaji ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kuepukana na matatizo makubwa zaidi, na pia dawa hizi hazitumiki kiholela bali ni kwa ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya,kwa sababu ukitumia kiholela unaweza kujikuta kwenye matatizo makubwa zaidi.

 

12. Pia dawa hii inapaswa kutumiwa na watu mbalimbali kadri ya wataalamu wa afya ila kwa wale wenye matatizo kwenye ubongo wanapaswa kuitumia chini ya uangalizi maalumu,na wale wanaoanguka kifafa wanapaswa kuitumia kwa uangalifu maalum.

 

13. Vile vile napenda kutoa angalizo kidogo kwa wagonjwa wa kisukari na vilevile wana magonjwa ya moyo na wanatumia dawa hii ya propranolol, kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba dawa hii inatabia ya kupunguza kiwango cha sukari mwilini na kwa wale hasa wenye sukari ya kushuka  kabla ya kutumia dawa hii ya propranolol wanapaswa kupima sukari na kuona iko kwa kiasi gani na wakiona iko chini wasitumie dawa hii wahakikishe kwamba sukari inakuwa kwenye hali ya kawaida, na pia wahakikishe kwamba wanakula vyakula vyenye wingi wa sukari na wale na kushiba, na wakiona matumizi ya dawa hii ni shida kwao kwa sababu ya hali yao ya sukari ni vizuri wakabadilishiwa dawa.

 

14. Pia napenda kutoa angalizo tena kwa wale wenye matatizo ya kupumua, hasa wenye pumu na matatizo mengine kama hayo na pia wanatumia dawa hizi ya propranolol wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya ili waweze kubadilishiwa dawa kwa sababu kama dawa yenyewe inaleta tatizo la kupumua vipi ikiongezea na tatizo la asili la mgonjwa na hapo hali inaweza kuwa mbaya zaidi, waone wataalamu wa afya kama tatizo linaleta shida.

 

15. Pia na wagonjwa wa akili na wenyewe wanapaswa kuwa kwenye uangalizi zaidi kwa sababu dawa hii inaleta tatizo la kuwaza na kuwasababishia watumiaji kutokuwa na hali ya kawaida vipi kama mtu ana magonjwa ya akili na akiongezea na dawa hii hali huwa mbaya zaidi na kuleta madhara yadiyotarajiwa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1663


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Fahamu dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi. Soma Zaidi...

Fahamu dawa ambazo uchangia kupungua kwa nguvu za kiume
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali ambazo uchangia katika kupunguza nguvu za kiume , hii ni kwa sababu ya wataalamu mbalimbali wanavyosema Soma Zaidi...

IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE
Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake. Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya ibuprofen katika kutuliza maumivu
Post hii inahusu zaidi dawa ibuprofen katika kutuliza maumivu, ni aina mojawapo ya dawa na yenyewe ufanya kazi kama aspirin na paracetamol Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto. Soma Zaidi...

Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo
Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya mebendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya mebendazole ni dawa ambayo utumika kutibu minyoo ambayo utokea kwa watoto na watu wazima. Soma Zaidi...

Matibabu ya ugonjwa wa uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mgonjwa wa uti wa mgongo, kwa kawaida tunajua kuwa homa hii ya uti wa mgongo usababisha na wadudu mbalimbali kama vile bakteria, virus, fungasi, sumu mbalimbali kama vile madini ya lead na arseni, na vitu kama vile Mag Soma Zaidi...

Dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria
Posti hii inahusu zaidi dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ,ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi kwa matibabu ya ugonjwa wa Malaria. Soma Zaidi...

Fahamu tiba ya jino
Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo Soma Zaidi...

Fahamu dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo. Soma Zaidi...

Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa
Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli. Soma Zaidi...