picha

Dawa ya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za minyoo

DAWA YA MINYOOMinyoo ni wadudu aina ya parasite ambao wanaingia kwenye miili ya kiumbe hai kama wanyama na binadamu, na wanajipatia chakula chao humo na kuishi. Kwa binadamu kuna minyoo aiina nyingi sana inayo weza kuwaathiri. Ila zipo aina tatu ambazo zinaonekana ni zaidi kuathiri binadamu. Nazo ni kama:-

 

1.Minyoo aina ya Roundworms hawa wanaingia kwenye miili yetu kupitia vyakula tunavyokula ama vinywaji endapo hivyo vyakula ama vinywaji vitakuwa na mayai yao. Minyoo hawa wanataga na kuishi kwenye utumbo. Minyoo hawa ni pamoja na threadworm, ascaris, hookworm na trichuris.

 

2.Minyoo aina ya tapeworm, hawa hishi kwenye tumbo, mara nyingi tunaweza kuwapata minyoo hawa kwa kula chakula ambacho hakikupikwa ama hakikuwiva vyema kama nyama, mihogo mibichi n.k

 

3.Flukeworms, minyoo hawa huingia mwilini mwetu na kuishi kwenye damu, tumbo, mapafu ama kwenye ini. Unaweza kuwapata minyoo hawa kwa kuogelea ama kuoga kwenye maji yenye minyoo hawa. Mimnyoo hawa husababisha pia ugonjwa ujulikanao kama kichocho (schistosomiasis).

 

Ni dawa gani hutibu minyoo?Kwa ufupi tiba ya minyoo hutofautiana kulingana na aina ya minyoo na kiasi cha athari ndani ya mwili. Kwa kiasi kikubwa dawa aina ya  HYPERLINK "https://www.bongoclass.com/dawa/Mebendazole" Mebendazole imekuwa ikitumika kwa kiasi kikubwa sana maeneo mengi. Na hii ni kwa sababu dawa hii inatumika sana kutibu minyoo aina ya threadworm ambao minyoo hawa ndio wanaathiri watu zaidi. Pia inaweza kutibu aina nyinginyingi za minyoo. Dawa nyingine za kutibu minyoo ni:-

 

1.Levamisole2.Tiabendazole3.Ivermectin4.Niclosamide5.Praziquantel6.Albendazole7.Diethylcarbamazine

 

Dawa hizi zinafanyaje kazi?Yes hili ni swali zuri sana. Sasa inakupasa ujuwe namna ambavyo dawa hizi zitakusaidia kutibu minyoo. Dawa hizi zinafanya kazi kama ifuatavyo:-

 

A.Mebendazole, albendazole na tiabendazole hizi kuzuia minyoo isifyonze chakul (sugar) kutoka kwenye miili yetu. Hivyo wanaweza kufa kwa njaa. Ila dawa hii itauwa minyoo lakini sio mayai yao ambayo wameyataga tayari.

 

B.Praziquantel na ivermectin, dawa hizi husaidia kuwazubaisha minyoo kwenye utumbo, hivyo wanaweza kutolewa kwa njia ya haja kubwa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2238

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.

Soma Zaidi...
Fahamu Dawa itwayo Diazepam

Diazepam ni nini? Diazepam ni Dawa ambayo Huathiri kemikali kwenye ubongo ambazo zinaweza kukosa uwiano na kusababisha wasiwasi. Diazepam hutumiwa kutibu matatizo ya wasiwasi, dalili za kuacha pombe, au misuli. Diazepam wakati mwingine hutumiwa pamoja n

Soma Zaidi...
Dawa ya vidonda vya tumbo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya parental Artusnate dawa ya kutibu malaria sugu

Post hii inahusu zaidi dawa ya Parental Artusnate ni dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria sugu kama tutakavyoona hapo baadaye.

Soma Zaidi...