Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu
Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.
Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu.
1. Dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu ugonjwa wa kifua kikuu, kwa kawaida kifua kikuu usababisha na bakteria anayeitwa mycobacterium tuberculosis ambaye uweza kutoka kwa mgonjwa kuingia kwa mtu mzima na kusababisha maambukizi kwa kupitia kwenye hewa,mate,makohozi na mambo kama hayo kwa hiyo ni vizuri kabisa kujihadhari na ugonjwa huu pia na matibabu yake uchukua mda mrefu na pia ugonjwa huu upenda kujirudia mara kwa mara.
2. Ugonjwa huu tunaweza kuutambua kupitia njia mbalimbali kama vile kuingia kwenye koo yaani kwa lugha ya kitaalamu ni X-ray, mgonjwa kukohoa zaidi ya wiki mbili, kuwepo kwa homa za mara kwa mara,kutokwa na jasho hasa wakati wa usiku, kukohoa makohozi yaliyochangamyikana na damu(haemoptysis) kupungua uzito kwa ghafla,kuvimba kwa lymph nodes za kwenye makwao, tumbo kujaa maji, kuwepo kwa shida wakati wa kupumua kuvimba kwenye jointi, hizo ni dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kifua kikuu baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kwenda hospitali kwa matibabu.
3.Dawa za kifua kikuu zimegawanyika kwenye makundi makuu mawili kuna kundi la kwanza ambapo mgonjwa anaanza kuzitumia kwanza na ndizo zilizopendekezwa na dawa hizi ni kama ifuatavyo.
- isoniazid(NH or H)
- Rifampin (RIF or R)
- Pyrazinamida(PZA or Z)
- Streptomycin (SM or S)
- Ethambutol (EMB or E)
Dawa hizo ndizo mgonjwa anapaswa kutumia kwa mara ya kwanza ambazo zinakuwa zimechanganywa na dawa zaidi ya moja na ikiwa dawa hizo hazikuweza kufanya kazi mgonjwa anaweza kuhamishiwa kwenye kundi la pili ambalo kwa kitaalamu huitwa second line ila kundi la kwanza huitwa first line.
4. Kama mgonjwa ameshindwa kutumia kundi la kwanza anaweza kutumia kundi la pili, kwa nini kundi la kwanza linagoma ? Kwa sababu ya maudhi madogo madogo yanakuwa na nguvu sana na kumsababishia mgonjwa matatizo makubwa zaidi ambayo yanaongeza zaidi ugonjwa. Kwa hiyo kama dawa za kundi la kwanza zimegoma mgonjwa anaweza kutumia dawa zifuatazo kwa ushauri wa daktari.
- Ethionamide
- Cycloserine
- Capreomysin
- Kanamycin
- Streptomycin
- Fluoroauinolones( Eg oflaxamin, moxifloxamine.
Pia dawa hizi zinakuwa kwenye mchanganyiko wa vidonge zaidi ya viwili ambavyo uweza kutengeneza dozi moja ya dawa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Matibabu ya ugonjwa wa uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mgonjwa wa uti wa mgongo, kwa kawaida tunajua kuwa homa hii ya uti wa mgongo usababisha na wadudu mbalimbali kama vile bakteria, virus, fungasi, sumu mbalimbali kama vile madini ya lead na arseni, na vitu kama vile Mag
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.
Soma Zaidi...Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital
Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.
Soma Zaidi...dawa ya minyoo, dalili za minyoo na sababu na vyanzo vya minyoo
MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.
Soma Zaidi...Dawa ya chango na maumivu ya hedhi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi
Soma Zaidi...Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.
Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.
Soma Zaidi...