picha

Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu

Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.

Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu.

1. Dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu ugonjwa wa kifua kikuu, kwa kawaida kifua kikuu usababisha na bakteria anayeitwa mycobacterium tuberculosis ambaye uweza kutoka kwa mgonjwa kuingia kwa mtu mzima na kusababisha maambukizi kwa kupitia kwenye hewa,mate,makohozi na mambo kama hayo kwa hiyo ni vizuri kabisa kujihadhari na ugonjwa huu pia na matibabu yake uchukua mda mrefu na pia ugonjwa huu upenda kujirudia mara kwa mara.

 

 

 

 

2. Ugonjwa huu tunaweza kuutambua kupitia njia mbalimbali kama vile kuingia kwenye koo yaani kwa lugha ya kitaalamu ni X-ray, mgonjwa kukohoa zaidi ya wiki mbili, kuwepo kwa homa za mara kwa mara,kutokwa na jasho hasa wakati wa usiku, kukohoa makohozi yaliyochangamyikana na damu(haemoptysis) kupungua uzito kwa ghafla,kuvimba kwa lymph nodes za kwenye makwao, tumbo kujaa maji, kuwepo kwa shida wakati wa kupumua kuvimba kwenye jointi, hizo ni dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kifua kikuu baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kwenda hospitali kwa matibabu.

3.Dawa za kifua kikuu zimegawanyika kwenye makundi makuu mawili kuna kundi la kwanza ambapo mgonjwa anaanza kuzitumia kwanza na ndizo zilizopendekezwa na dawa hizi ni kama ifuatavyo.

Dawa hizo ndizo mgonjwa anapaswa kutumia kwa mara ya kwanza ambazo zinakuwa zimechanganywa na dawa zaidi ya moja na ikiwa dawa hizo hazikuweza kufanya kazi mgonjwa anaweza kuhamishiwa kwenye kundi la pili ambalo kwa kitaalamu huitwa second line ila kundi la kwanza huitwa first line.

 

 

 

 

4. Kama mgonjwa ameshindwa kutumia kundi la kwanza anaweza kutumia kundi la pili, kwa nini kundi la kwanza linagoma ? Kwa sababu ya maudhi madogo madogo yanakuwa na nguvu sana na kumsababishia mgonjwa matatizo makubwa zaidi ambayo yanaongeza zaidi ugonjwa. Kwa hiyo kama dawa za kundi la kwanza zimegoma mgonjwa anaweza kutumia dawa zifuatazo kwa ushauri wa daktari.

Pia dawa hizi zinakuwa kwenye mchanganyiko wa  vidonge zaidi ya viwili ambavyo uweza kutengeneza dozi moja ya dawa

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 1790

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Miungurumo haiishi tumboni nikishika upande wa kushoto wa tumbo kuna maumivu kwa mbali je mm nitumie dawa gan kuondoa tatizo hilo

Kukawa na gesi tumboni kunaweza kuwa ni dalili ya shida kwenye afya, hasa katika mfumo wa chakula. Hali itakuwa sio nzuri endapo utakosea hamu ya kula na kuhisivkushiba muda wowote.

Soma Zaidi...
Dawa ya fangasi uumeni

kama unasumbuliwa na fangasi uumeni, nitakujuza dawa yake, sababu za fangasi uumeni, matibabu yake na njia za kuwaepuka

Soma Zaidi...
Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.

Soma Zaidi...
Dawa za mapunye

Somo Hili linakwenda kukuletea dawa za maounye

Soma Zaidi...
Dawa ya chango na maumivu ya hedhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya chango na dawa ya maumivu ya hedhi

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha

Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...