Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu
Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.
Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu.
1. Dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu ugonjwa wa kifua kikuu, kwa kawaida kifua kikuu usababisha na bakteria anayeitwa mycobacterium tuberculosis ambaye uweza kutoka kwa mgonjwa kuingia kwa mtu mzima na kusababisha maambukizi kwa kupitia kwenye hewa,mate,makohozi na mambo kama hayo kwa hiyo ni vizuri kabisa kujihadhari na ugonjwa huu pia na matibabu yake uchukua mda mrefu na pia ugonjwa huu upenda kujirudia mara kwa mara.
2. Ugonjwa huu tunaweza kuutambua kupitia njia mbalimbali kama vile kuingia kwenye koo yaani kwa lugha ya kitaalamu ni X-ray, mgonjwa kukohoa zaidi ya wiki mbili, kuwepo kwa homa za mara kwa mara,kutokwa na jasho hasa wakati wa usiku, kukohoa makohozi yaliyochangamyikana na damu(haemoptysis) kupungua uzito kwa ghafla,kuvimba kwa lymph nodes za kwenye makwao, tumbo kujaa maji, kuwepo kwa shida wakati wa kupumua kuvimba kwenye jointi, hizo ni dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kifua kikuu baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kwenda hospitali kwa matibabu.
3.Dawa za kifua kikuu zimegawanyika kwenye makundi makuu mawili kuna kundi la kwanza ambapo mgonjwa anaanza kuzitumia kwanza na ndizo zilizopendekezwa na dawa hizi ni kama ifuatavyo.
- isoniazid(NH or H)
- Rifampin (RIF or R)
- Pyrazinamida(PZA or Z)
- Streptomycin (SM or S)
- Ethambutol (EMB or E)
Dawa hizo ndizo mgonjwa anapaswa kutumia kwa mara ya kwanza ambazo zinakuwa zimechanganywa na dawa zaidi ya moja na ikiwa dawa hizo hazikuweza kufanya kazi mgonjwa anaweza kuhamishiwa kwenye kundi la pili ambalo kwa kitaalamu huitwa second line ila kundi la kwanza huitwa first line.
4. Kama mgonjwa ameshindwa kutumia kundi la kwanza anaweza kutumia kundi la pili, kwa nini kundi la kwanza linagoma ? Kwa sababu ya maudhi madogo madogo yanakuwa na nguvu sana na kumsababishia mgonjwa matatizo makubwa zaidi ambayo yanaongeza zaidi ugonjwa. Kwa hiyo kama dawa za kundi la kwanza zimegoma mgonjwa anaweza kutumia dawa zifuatazo kwa ushauri wa daktari.
- Ethionamide
- Cycloserine
- Capreomysin
- Kanamycin
- Streptomycin
- Fluoroauinolones( Eg oflaxamin, moxifloxamine.
Pia dawa hizi zinakuwa kwenye mchanganyiko wa vidonge zaidi ya viwili ambavyo uweza kutengeneza dozi moja ya dawa
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 web hosting 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Ijue dawa ya sulphadoxine na pyrimethamine (sp)
Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.
Soma Zaidi...Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.
Soma Zaidi...Fahamu dawa za 5-fluorouracil,Tegafur na uracili
Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...Matibabu ya ugonjwa wa uti wa mgongo
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mgonjwa wa uti wa mgongo, kwa kawaida tunajua kuwa homa hii ya uti wa mgongo usababisha na wadudu mbalimbali kama vile bakteria, virus, fungasi, sumu mbalimbali kama vile madini ya lead na arseni, na vitu kama vile Mag
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi.
Soma Zaidi...Nani anapaswa kutumia vidonge vya zamiconal.
Posti hii inahusu zaidi watu ambao wana uwezo wa kutumia vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya watu au makundi yanayoweza kutumia vidonge hivi.
Soma Zaidi...