picha

Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria

Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali.

Kazi za Artesunate katika kutibu Malaria kali.

1.Artusnate ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi katika kutibu Malaria ambayo ni kali na dawa hii umetumiwa na watu wengi na wamefanikiwa kupona kwa kiwango kikubwa sana. 

 

Dawa hii utumika ndani ya Msaa ishilini na manne Ili kuendelea kuangalia maendeleo ya mgonjwa mgonjwa upewa anapofika tu, na baada ya masaa Kumi na mbili baadae anapewa dose ya mwisho ndani ya maasaa ishilini na manne, na mgonjwa akimaliza dozi hii anaongezeka na dozi ya Mseto Ili kuweza kumalizika wadudu waliobaki.

 

2.Dalili ambazo uonekana kwa mgonjwa na kuamua kumpatia dawa hii ni kama ifuatavyo, mgonjwa anakuwa amelegea sana kwa mwili mzima,  mgonjwa kwa wakati mwingine anakuwa amezimi kabisa na hajui kinachoendelea, pengine Tabia ya Mgonjwa ubadilika kwa sababu wakati mwingine Malaria uingia kichwani na kumfanya mgonjwa kuanza kuongea maneno  yoyote yanayomjia kichwani, wagonjwa wengine huwa na degedege hasa kwa watoto wadogo ambao ushambuliwa sana na Malaria na kuwafanya wapate degedege pengine hali hiii inaweza kujitokeza hata kwa watu wazima.

 

3. Dalili nyingine kwa mgonjwa mwenye maambukizi ya Malaria kali ni Pamoja na kukosa hewa au mgonjwa anapumua vibaya, mwili mzima wa Mgonjwa ubadilika na kuwa na rangi ya njano hii nikwa sababu ya kuharibika kwa seli kwa sababu ya maambukizi, wakati mwingine mgonjwa anakuwa anatapika kila kitu anachokuli, kama ni kwa mtoto anashindwa kunyonya na kula kitu chochote  kwa hiyo mtu Mwenye dalili hizo anapaswa kuty artusnate Maana ndiyo dawa ya Malaria inayoweza kutibu Malaria sugu kwa hiyo tunapaswa kutumia dawa hii kwa kuona dalili hizi kubwa za Malaria.

 

4.Dawa hii ya Artusnate unapokuwa inatumika uweza kuleta maudhi mbalimbali au matokeo mbalimbali kwa mgonjwa ambayo mgonjwa hasiogope ni kawaida kama vile kutapika, kuishiwa nguvu kwa mgonjwa, maumivu ya kichwa au wakati mwingine Homa kupanda kusiko kwa kawaida hii ni kawaida kwa Mgonjwa kwa hiyo mgonjwa akiwa anatumia dawa hii anapaswa kula na kunywa sana Maana dawa hii ufanya kazi vizuri okiwa mgonjwa anakuwa na kunywa vizuri.

 

Kwa hiyo katika matibabu tuzingatie sana chakula, Maana dawa ufanya kazi vizuri kuliko kama mgonjwa ameshiba.

 

Angalisho: baada ya kutumia dawa hii ya Artusnate mgonjwa inabidi aongezewa dawa nyingine ya kutibu kutibu Malaria ya kawaida kama vile Mseto,ACT na SP

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 2817

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya hydralazine katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya hydralazine katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii imetoka kwenye kundi la vasodilators, na pia usaidia sana kwenye matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Theophylline katika kutibi mfumo wa upumuaji

Post hii inahusu zaidi dawa ya theophylline ni dawa inayofanya kazi kwenye mfumo wa upumuaji.

Soma Zaidi...
Faida za dawa za NMN

Posti hii inahusu zaidi faida za dawa za NMN maana yake ni Nicotinamide mononucleotide ni dawa ambazo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali kama vile.

Soma Zaidi...
Ijue Dawa ya lignocaine

Posti hii inahusu zaidi dawa ya lignocaine kama mojawapo ya Dawa ambayo utumika wakati wa upasuaji.

Soma Zaidi...
Dawa ya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za minyoo

Soma Zaidi...
Fahamu Dawa inayotibu minyoo iitwayo albenza (albendazole)

Albenza (albendazole) hutumika kutibu magonjwa ya minyoo ya ndani ikiwa ni pamoja na maambukizi ya minyoo ya tegu. Albenza inafanya kazi kukomesha kuenea kwa maambukizo ya minyoo kwenye chanzo, na kukata chanzo chao cha nishati, na hivyo kuzuia kuenea k

Soma Zaidi...