DART somo la 3: Aina za Data
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart.
Dart ni kama lugha nyinginezo za kompyuta, karibia aina za data zinazotumuka kwenye dart ni sawa katika language nyinginezo. Aina hizo za data ni :-
- Namba
- String
- Boolean
- Lists
- Map
- Runes
- Namba ni aina za data ambazo ni namba tu.
Namaba zinaweza kuwa ni int yaani namba nzima ama double yaani namba zenye desimali.
void main(){
print(2);
print(1.5);
}
- String
Hizi ni data zilizo katika mfumo wa mchanganyiko wa herufi, namba, na alama za uandishi. String huandikwa ndani ya alama za funga na fungua semi mbili (“) ama moja (‘). Jambo la kuzingatia ni kuwa utakayoa anza nayo ndio umalizie nayo. Yaani ukitumia (“) mwanzo basi na mwisho utumie (“)
void main(){
print("bongoclass");
print('info@example.com');
print("#@?");
}
Pia unaweza kuunganisha string zaidi ya moja yaani kufanya concatnation. Kuna njia 3 ambazo hutumika kuunganisa string zaidi ya moja. Njia hizo ni kama
- Kwa kutumia alama ya kujumlisha +
- Kwa kutenganisha string mbili kwa kuacha nafasi kati yao
- Kwa kutumia interpolation yaani unaunganisha string na variable.
void main(){
//concatnation kwa kutumia +
print("karibu "+"Bongoclass");
//kwa kucha nafasi kati ya string mbili
print('karibu ' 'Bongoclass');
//kufanya interpolation
//x ni variable. Tutajifunza zaidi kwenye somo lijalo
var x = 'bongoclass';
print('karibu ${x}');
}
Kwenye string unaweza ku break line kwa kutumia back slash () ikifuatiwa na herufi n hii ni sawa na matumizi ya <br> kwenye html
void main(){
print(' karibu bongoclass upate kujifunza');
}
Kuna changamoto nyingine angalia mfano huu
void main(){
print("mama anauza ng'ombe");
}
Hapa utaona hakuna error. Ila sasa wacha tutumia single quotation mark (‘)
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
Hapo kwenye neno ng’ombe hiyo alama ya apostroph (‘) haiwezi kuendana na hizo funga semi. Hivyo kutatua tatizo hilo tutatumia back slash 2WD ().
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
DART somo la 41: concept ya generic kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya generics ili kuweza kufanya kazi na aina mbalimbali za data kwenye class.
Soma Zaidi...DART somo la 34: Static variable kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static property na jinsi ambavyo inavyotumika.
Soma Zaidi...DART somo la 19: method zinazotumika kwenye set data type kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja na method ambazo hufanya kazi kwenye set.
Soma Zaidi...DART somo la 8: Matumizi ya switch case
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu switch case na jinsi inavyofanya kazi kwenye Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 33 concept ya polymorphism
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya polymorphism.
Soma Zaidi...DART somo la 6: Dart operator na jinsi zinavyofanya kazi.
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi zake na jinsi ya kuzitumia.
Soma Zaidi...