DART somo la 3: Aina za Data
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart.
Dart ni kama lugha nyinginezo za kompyuta, karibia aina za data zinazotumuka kwenye dart ni sawa katika language nyinginezo. Aina hizo za data ni :-
- Namba
- String
- Boolean
- Lists
- Map
- Runes
- Namba ni aina za data ambazo ni namba tu.
Namaba zinaweza kuwa ni int yaani namba nzima ama double yaani namba zenye desimali.
void main(){
print(2);
print(1.5);
}
- String
Hizi ni data zilizo katika mfumo wa mchanganyiko wa herufi, namba, na alama za uandishi. String huandikwa ndani ya alama za funga na fungua semi mbili (“) ama moja (‘). Jambo la kuzingatia ni kuwa utakayoa anza nayo ndio umalizie nayo. Yaani ukitumia (“) mwanzo basi na mwisho utumie (“)
void main(){
print("bongoclass");
print('info@example.com');
print("#@?");
}
Pia unaweza kuunganisha string zaidi ya moja yaani kufanya concatnation. Kuna njia 3 ambazo hutumika kuunganisa string zaidi ya moja. Njia hizo ni kama
- Kwa kutumia alama ya kujumlisha +
- Kwa kutenganisha string mbili kwa kuacha nafasi kati yao
- Kwa kutumia interpolation yaani unaunganisha string na variable.
void main(){
//concatnation kwa kutumia +
print("karibu "+"Bongoclass");
//kwa kucha nafasi kati ya string mbili
print('karibu ' 'Bongoclass');
//kufanya interpolation
//x ni variable. Tutajifunza zaidi kwenye somo lijalo
var x = 'bongoclass';
print('karibu ${x}');
}
Kwenye string unaweza ku break line kwa kutumia back slash () ikifuatiwa na herufi n hii ni sawa na matumizi ya <br> kwenye html
void main(){
print(' karibu bongoclass upate kujifunza');
}
Kuna changamoto nyingine angalia mfano huu
void main(){
print("mama anauza ng'ombe");
}
Hapa utaona hakuna error. Ila sasa wacha tutumia single quotation mark (‘)
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
Hapo kwenye neno ng’ombe hiyo alama ya apostroph (‘) haiwezi kuendana na hizo funga semi. Hivyo kutatua tatizo hilo tutatumia back slash 2WD ().
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
DART somo la 36: Abstract class kweye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu abstract class na abstract method kwenye Dart.
Soma Zaidi...Dart somo la 26: DART OOP maana ya object, na jinsi ya kuitengeneza kwenye OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza Object pamoja na properties. Haa kwa ufupi tutakwenda kujifunza jinsi ya kutumia class.
Soma Zaidi...DART somo la 34: Static variable kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static property na jinsi ambavyo inavyotumika.
Soma Zaidi...Dart somo la 25: DART OOP Nini maaan ya class na vipi utaweza kuitengeneza
Katika somo hili utajifunza maana ya class kwenye OOP paradigm, kisha utajifunza jinsi ya kutengeneza class.
Soma Zaidi...DART somo la 24: Dart OOP maana ya Object Oriented Programming kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya OOP na faida zake. Pia utakwenda kujifunza kuhusu features za OOP.
Soma Zaidi...DART somo la 7: matumizi ya if, else, if else, else if kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Soma Zaidi...