DART somo la 3: Aina za Data

DART somo la 3: Aina za Data

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart.

Dart ni kama lugha nyinginezo za kompyuta, karibia aina za data zinazotumuka kwenye dart ni sawa katika language nyinginezo. Aina hizo za data ni :-

  1. Namba
  2. String
  3. Boolean
  4. Lists
  5. Map
  6. Runes

 

  1. Namba ni aina za data ambazo ni namba tu. 

Namaba zinaweza kuwa ni int yaani namba nzima ama double yaani namba zenye desimali.

void main(){

 print(2);

 print(1.5);

}

  1. String

Hizi ni data zilizo katika mfumo wa mchanganyiko wa herufi, namba, na alama za uandishi. String huandikwa ndani ya alama za funga na fungua semi mbili (“) ama moja (). Jambo la kuzingatia ni kuwa utakayoa anza nayo ndio umalizie nayo. Yaani ukitumia (“) mwanzo basi na mwisho utumie (“)

void main(){

 print("bongoclass");

 print('info@example.com');

 print("#@?");

}

Pia unaweza kuunganisha string zaidi ya moja yaani kufanya concatnation. Kuna njia 3 ambazo hutumika kuunganisa string zaidi ya moja. Njia hizo ni kama

  1. Kwa kutumia alama ya kujumlisha +
  2. Kwa kutenganisha string mbili kwa kuacha nafasi kati yao
  3. Kwa kutumia interpolation yaani unaunganisha string na variable.

void main(){

 //concatnation kwa kutumia +

 print("karibu "+"Bongoclass");

 //kwa kucha nafasi kati ya string mbili

 print('karibu ' 'Bongoclass');

 //kufanya interpolation

 //x ni variable. Tutajifunza zaidi kwenye somo lijalo

 var x = 'bongoclass';

 print('karibu ${x}');

}

Kwenye string unaweza ku break line kwa kutumia back slash () ikifuatiwa na herufi n hii ni sawa na matumizi ya <br> kwenye html

 

void main(){

print(' karibu bongoclass upate kujifunza');

}

Kuna changamoto nyingine angalia mfano huu

void main(){

print("mama anauza ng'ombe");

}

Hapa utaona hakuna error. Ila sasa wacha tutumia single quotation mark (‘)

void main(){

print('mama anauza ng'ombe');

}

Hapo kwenye neno ng’ombe hiyo alama ya apostroph (‘) haiwezi kuendana na hizo funga semi. Hivyo kutatua tatizo hilo tutatumia back slash 2WD ().

void main(){

print('mama anauza ng'ombe');

}

 

...
Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: DART Main: Masomo File: Download PDF Views: 1739

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

DART somo la 23: Jinsi ya kusoma mafaili kwa kutumia Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma na kuandika faili kwa kutumia Dart programming.

Soma Zaidi...
DART somo la 31: inheritance kwenye DART OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu inheritance, na inavyoweza kutumika kwenye Dart OOP.

Soma Zaidi...
DART somo la 45: Jinai ys kutuma mysql database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya mysql kwenye Dart. hakikisha umeelewa vyema na kutekeleza yalioelekezwa kutoka kwenye somo lililopita.

Soma Zaidi...
DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 19: method zinazotumika kwenye set data type kwenye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja na method ambazo hufanya kazi kwenye set.

Soma Zaidi...
DART somo la 43: Stream kwenye Dart

Katika somo hili utakwenda ujifunz akuhusu concept ya stream kwenye Dart. pia ttaona kwa namna gani strean inaweza kutofautiana na future wakati zote mbili zipo kwenye asychronous programming.

Soma Zaidi...