DART somo la 3: Aina za Data
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart.
Dart ni kama lugha nyinginezo za kompyuta, karibia aina za data zinazotumuka kwenye dart ni sawa katika language nyinginezo. Aina hizo za data ni :-
- Namba
- String
- Boolean
- Lists
- Map
- Runes
- Namba ni aina za data ambazo ni namba tu.
Namaba zinaweza kuwa ni int yaani namba nzima ama double yaani namba zenye desimali.
void main(){
print(2);
print(1.5);
}
- String
Hizi ni data zilizo katika mfumo wa mchanganyiko wa herufi, namba, na alama za uandishi. String huandikwa ndani ya alama za funga na fungua semi mbili (“) ama moja (‘). Jambo la kuzingatia ni kuwa utakayoa anza nayo ndio umalizie nayo. Yaani ukitumia (“) mwanzo basi na mwisho utumie (“)
void main(){
print("bongoclass");
print('info@example.com');
print("#@?");
}
Pia unaweza kuunganisha string zaidi ya moja yaani kufanya concatnation. Kuna njia 3 ambazo hutumika kuunganisa string zaidi ya moja. Njia hizo ni kama
- Kwa kutumia alama ya kujumlisha +
- Kwa kutenganisha string mbili kwa kuacha nafasi kati yao
- Kwa kutumia interpolation yaani unaunganisha string na variable.
void main(){
//concatnation kwa kutumia +
print("karibu "+"Bongoclass");
//kwa kucha nafasi kati ya string mbili
print('karibu ' 'Bongoclass');
//kufanya interpolation
//x ni variable. Tutajifunza zaidi kwenye somo lijalo
var x = 'bongoclass';
print('karibu ${x}');
}
Kwenye string unaweza ku break line kwa kutumia back slash () ikifuatiwa na herufi n hii ni sawa na matumizi ya <br> kwenye html
void main(){
print(' karibu bongoclass upate kujifunza');
}
Kuna changamoto nyingine angalia mfano huu
void main(){
print("mama anauza ng'ombe");
}
Hapa utaona hakuna error. Ila sasa wacha tutumia single quotation mark (‘)
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
Hapo kwenye neno ng’ombe hiyo alama ya apostroph (‘) haiwezi kuendana na hizo funga semi. Hivyo kutatua tatizo hilo tutatumia back slash 2WD ().
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
DART somo la 17: method za namba zinazotumika kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kuziona method za dart zinazotumika kwenye namba. pia utajifunzakuhusu math library
Soma Zaidi...DART somo la 19: method zinazotumika kwenye set data type kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja na method ambazo hufanya kazi kwenye set.
Soma Zaidi...DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kula majani ya kunde
Leo tutajifunza kuhusu majani ya kunde — mboga za kijani zinazotokana na mmea wa kunde (beans). Wengi hula mbegu za kunde pekee, wakisahau kuwa hata majani yake yana virutubisho vya thamani kubwa kwa mwili. Tutazungumzia vitamini, madini, na faida mbalimbali za kiafya zinazopatikana katika majani haya.
Soma Zaidi...Dart somo la 26: DART OOP maana ya object, na jinsi ya kuitengeneza kwenye OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza Object pamoja na properties. Haa kwa ufupi tutakwenda kujifunza jinsi ya kutumia class.
Soma Zaidi...DART somo la 21: Jinsi ya kutengeneza library kwenye Dart
Katika somo hili utajifunza kuhusu dart library. Pia tutakwend aktengeneza library yetu wennyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.
Soma Zaidi...