DART somo la 3: Aina za Data
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart.
Dart ni kama lugha nyinginezo za kompyuta, karibia aina za data zinazotumuka kwenye dart ni sawa katika language nyinginezo. Aina hizo za data ni :-
- Namba
- String
- Boolean
- Lists
- Map
- Runes
- Namba ni aina za data ambazo ni namba tu.
Namaba zinaweza kuwa ni int yaani namba nzima ama double yaani namba zenye desimali.
void main(){
print(2);
print(1.5);
}
- String
Hizi ni data zilizo katika mfumo wa mchanganyiko wa herufi, namba, na alama za uandishi. String huandikwa ndani ya alama za funga na fungua semi mbili (“) ama moja (‘). Jambo la kuzingatia ni kuwa utakayoa anza nayo ndio umalizie nayo. Yaani ukitumia (“) mwanzo basi na mwisho utumie (“)
void main(){
print("bongoclass");
print('info@example.com');
print("#@?");
}
Pia unaweza kuunganisha string zaidi ya moja yaani kufanya concatnation. Kuna njia 3 ambazo hutumika kuunganisa string zaidi ya moja. Njia hizo ni kama
- Kwa kutumia alama ya kujumlisha +
- Kwa kutenganisha string mbili kwa kuacha nafasi kati yao
- Kwa kutumia interpolation yaani unaunganisha string na variable.
void main(){
//concatnation kwa kutumia +
print("karibu "+"Bongoclass");
//kwa kucha nafasi kati ya string mbili
print('karibu ' 'Bongoclass');
//kufanya interpolation
//x ni variable. Tutajifunza zaidi kwenye somo lijalo
var x = 'bongoclass';
print('karibu ${x}');
}
Kwenye string unaweza ku break line kwa kutumia back slash () ikifuatiwa na herufi n hii ni sawa na matumizi ya <br> kwenye html
void main(){
print(' karibu bongoclass upate kujifunza');
}
Kuna changamoto nyingine angalia mfano huu
void main(){
print("mama anauza ng'ombe");
}
Hapa utaona hakuna error. Ila sasa wacha tutumia single quotation mark (‘)
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
Hapo kwenye neno ng’ombe hiyo alama ya apostroph (‘) haiwezi kuendana na hizo funga semi. Hivyo kutatua tatizo hilo tutatumia back slash 2WD ().
void main(){
print('mama anauza ng'ombe');
}
...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
DART somo la 13: function kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni ya kziandika na matumizi yake.
Soma Zaidi...DART somo la 31: inheritance kwenye DART OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu inheritance, na inavyoweza kutumika kwenye Dart OOP.
Soma Zaidi...DART somola 42: Asynchronous programming
Katika somo hili tutakwenda kujifunza concept nyingine ya asynchronous programming.
Soma Zaidi...DART somo la 45: Jinai ys kutuma mysql database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya mysql kwenye Dart. hakikisha umeelewa vyema na kutekeleza yalioelekezwa kutoka kwenye somo lililopita.
Soma Zaidi...DART somo la 43: Stream kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda ujifunz akuhusu concept ya stream kwenye Dart. pia ttaona kwa namna gani strean inaweza kutofautiana na future wakati zote mbili zipo kwenye asychronous programming.
Soma Zaidi...DART somo la 24: Jinsi ya kutengeneza faili, folda na kuingiza data
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika data kwenye faili. Kwanza utajifunza kutengeneza folda, kisha faili na kuweka data, kisha utajifunza kufuta fali.
Soma Zaidi...