DART somo la 13: function kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni ya kziandika na matumizi yake.
Function ni nini?
Function ni kifungu cha code (block of code) ambacho hufanya kazi maalumu. Function inaweza kufanya kazi kwa kujirudia rudia bila ya kikomo kila itakapoitwa. Function husaidia kutokurudiarudia kuandika code.
Mambo ya kuzingatia:
- Function hutumika zaidi ya mara moja
- Function haifanyikazi mpaka iitwe
- Function inakuwa na parameter
Jinsi ya kuandika function
- Function ambayo haihitaji ku return value
Returntype name (){
Code
}
Hapo utaona kwanz aunaanza return type hii itafahamisha kuwa function yako ita rudisha data amba laa. Kama haitarudisha data tutaweka void. Baada ya return type inayofuata na name yaani jina la hiyo function, kisha utaweka mabano () ndani ya haya mabano tutakuja kuweka parameter. Kisha utaweka mabano {} ndani ya haya mabano ndipo utaweka code ambazo unataka zifanye kazi. Wacha tuone mifano huwenda ukaelewa zaidi:-
Mfano 1:
Tunatengeneza program ya kuandika neno bongoclass mara 10. Kwanza tuatatengeneza hiyo fnction ambayo ita print nrno bongoclass
void bongo(){
print('Bongoclass');
}
Kisha tutaiita (call) hiyo funcyion kwenye main().
bongo(){
print('Bongoclass');
}
void main(){
bongo(;
}
Sasa kama tutaiita mara 10 itaprint hilo neno mara 10
void bongo(){
print('Bongoclass');
}
void main(){
for(int x = 0; x<10; x++){
bongo();
}
}
Jinsi ya kuweka parameter kwenye function
Tuchukulie mfano kama huu wa mwanzo. Tunataka mtumiaji aweze kuandika kwenye we anataka neno bongoclass litokee mara ngapi. Kwa mfano akitaka litokee mara 6 ataandika 6 kwenye user input kisha function yetu itafanya kazi husika.
Sasa katika hali hiyo tutahitaji kuweka variable ambayo itawakilisha hiyo 6 atakayowekamtu. Hiyo variable ndio parameter kwa mfano tutaiita idadi. Na hiyo namba 6 atakayoinginza mtu huitwa argument. Kwa ufup tunasema parameter ni jina ila argument ni value yenyewe.
Parameter zinaweza kuwa option, default ama required. Tutakwenda kuziona kadiri somo linavyoenda.wacha tuone mfano ambao mtumiaji ataweka argument na program kutoa majibu
import 'dart:io';
void bongo(idadi){
for(int x = 0; x<idadi; x++){
print('Bongoclass');
}
}
void main(){
print('ANDIKA IDADI');
int idadi = int.parse(stdin.readLineSync()!);
bongo(idadi);
}
Kuna kitu hapa tunataka kujifunza kwanza. Ukiangalia hapo utaona variable tumeitengenezea nje ya function.int idadi = int.parse(stdin.readLineSync()!);
Sasa kama utaiweka kwenye function utaona kuna error
import 'dart:io';
void bongo(idadi){
int idadi = int.parse(stdin.readLineSync()!);
for(int x = 0; x<idadi; x++){
print('Bongoclass');
}
}
void main(){
print('ANDIKA IDADI');
bongo(idadi);
}
Sasa ili kutatua tatizo itatibidi mixin hii ni njia ambayo hutumika kufanya class iweze kufanya kazi zaidi na zaidi. Lakini h...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
DART somola 42: Asynchronous programming
Katika somo hili tutakwenda kujifunza concept nyingine ya asynchronous programming.
Soma Zaidi...DART somo la 20: method zinazotumika kwenye map data type kwenye Dart
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye map data type
Soma Zaidi...DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 43: Stream kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda ujifunz akuhusu concept ya stream kwenye Dart. pia ttaona kwa namna gani strean inaweza kutofautiana na future wakati zote mbili zipo kwenye asychronous programming.
Soma Zaidi...DART somo la 27: DART OOP: maana ya constructor method na jinsi inavyotumika kwenye OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jins ya kutengeneza constructor method, pia utajifunza matumizi yake kwenye OOP.
Soma Zaidi...DART somo la 29: Dart encapsulation
Katika somo hili tutawenda kujifunza kuhusu encapsulatio kwenye Dart OOP na jinsi inavyoweza kutumika.
Soma Zaidi...