picha

DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart

Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.

Nini maana ya variable?

Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6

 

Sheria za variable:

  1. Haitakiwi kuanza na special character
  2. Haitakiwi kuanza na namba
  3. Haitakiwi kuanza na underscore
  4. Variable ni case sensitivity kwa maana unatakiwa uzingatie matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Mfano Juma na juma ni majina mawili tofauti.

 

Jinsi ya kuandika variable:

Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value

Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-

  1. Kwa kutumia keyword var
  2. Kwa kutumia dynamic
  3. Kwa kutumia const
  4. Kwa final

 

  1. Utaanza na neno  var likifuatiwa na jina la variable. Kisha utaweka alama ya = iikifuatiwa na value (thamani) ya variable. Unapotumia var  dart yenyewe itaelewa aina ya data aina ya data itakayotumika.

 

Mfano

void main(){

 var web = 'bongoclass';

 print(web);

}

Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja

void main() {

String web = 'bongoclass';

print(web);

}

Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini

import 'dart:ffi';

void main() {

Int web = 'bongoclass';

print(web);

}

Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.

 

Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.

void main() {

int a, b, c;

a = 5;

b = 10;

c = 2;

print(a +b +c);

}

Hapo jibu ni 17

 

Pia unaweza kubadili value ya variable kwa kuitumia tena. Ila hakikisha type of data inabakia ile ile kama umetumia var.

void main() {

var x = 3;

x = 4;

 

print(x);

}


Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: DART Main: Masomo File: Download PDF Views 1084

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

DART somo la 13: function kwenye dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni ya kziandika na matumizi yake.

Soma Zaidi...
DART somo la 30 :Jinsi ya kutengeneza setter na geter kwenye OOP

Katika somo hili tutakwenda kujifunza zaidi kuhusu method za getter na setter. Tutakwenda kuona hasa zinavyotumika na zinavyotengenezwa.

Soma Zaidi...
DART SOMO LA 16: String method zinazotumika kwneye Dart

Katika somo hili utakwenda kujfunza kuhusu String method zinazotumika kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 11:break and continue statement kwenye Dat loop

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Dart loop za for loop na while loop.

Soma Zaidi...
DART somola 42: Asynchronous programming

Katika somo hili tutakwenda kujifunza concept nyingine ya asynchronous programming.

Soma Zaidi...
DART somo la 22: Jinsi ya kutumia html library kwenye Dart

Katika somo hili tutakwenda kujifunz ajinsi ya kutumia library ya html kwenye Dart. somo hili litakupeleka kujifunza jinsi ya ku display dart output kwenye faili la html.

Soma Zaidi...