DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart
Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.
Nini maana ya variable?
Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6
Sheria za variable:
- Haitakiwi kuanza na special character
- Haitakiwi kuanza na namba
- Haitakiwi kuanza na underscore
- Variable ni case sensitivity kwa maana unatakiwa uzingatie matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Mfano Juma na juma ni majina mawili tofauti.
Jinsi ya kuandika variable:
Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value
Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-
- Kwa kutumia keyword var
- Kwa kutumia dynamic
- Kwa kutumia const
- Kwa final
- Utaanza na neno var likifuatiwa na jina la variable. Kisha utaweka alama ya = iikifuatiwa na value (thamani) ya variable. Unapotumia var dart yenyewe itaelewa aina ya data aina ya data itakayotumika.
Mfano
void main(){
var web = 'bongoclass';
print(web);
}
Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja
void main() {
String web = 'bongoclass';
print(web);
}
Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini
import 'dart:ffi';
void main() {
Int web = 'bongoclass';
print(web);
}
Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.
Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.
void main() {
int a, b, c;
a = 5;
b = 10;
c = 2;
print(a +b +c);
}
Hapo jibu ni 17
Pia unaweza kubadili value ya variable kwa kuitumia tena. Ila hakikisha type of data inabakia ile ile kama umetumia var.
void main() {
var x = 3;
x = 4;
print(x);
}
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 33 concept ya polymorphism
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya polymorphism.
Soma Zaidi...DART somo la 35: Enum kwenye Dart:
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu enum na inavyotumika kwenye Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 17: method za namba zinazotumika kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kuziona method za dart zinazotumika kwenye namba. pia utajifunzakuhusu math library
Soma Zaidi...DART somo la 29: Dart encapsulation
Katika somo hili tutawenda kujifunza kuhusu encapsulatio kwenye Dart OOP na jinsi inavyoweza kutumika.
Soma Zaidi...Dart somo la 25: DART OOP Nini maaan ya class na vipi utaweza kuitengeneza
Katika somo hili utajifunza maana ya class kwenye OOP paradigm, kisha utajifunza jinsi ya kutengeneza class.
Soma Zaidi...