Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.
Nini maana ya variable?
Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6
Sheria za variable:
Jinsi ya kuandika variable:
Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value
Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-
Mfano
void main(){
var web = 'bongoclass';
print(web);
}
Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja
void main() {
String web = 'bongoclass';
print(web);
}
Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini
import 'dart:ffi';
void main() {
Int web = 'bongoclass';
print(web);
}
Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.
Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.
void main() {
int a, b, c;
a = 5;
b = 10;
c = 2;
print(a +b +c);
}
Hapo jibu ni 17
Pia unaweza kubadili value ya variable kwa kuitumia tena. Ila hakikisha type of data inabakia ile ile kama umetumia var.
void main() {
var x = 3;
x = 4;
print(x);
}
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi zake na jinsi ya kuzitumia.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Soma Zaidi...Katika somo hili tutatkwenda kuziona baadhi ya xyntax yaani kanunu za uandishi wa code za dart.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya class kwenye OOP paradigm, kisha utajifunza jinsi ya kutengeneza class.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya OOP na faida zake. Pia utakwenda kujifunza kuhusu features za OOP.
Soma Zaidi...Katika somo hiliutakwenda kujifunza aina nyingine ya constructor ambayo hutumika kwenye Dart. aina hiyo ni factory constructory.
Soma Zaidi...