DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart
Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.
Nini maana ya variable?
Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6
Sheria za variable:
- Haitakiwi kuanza na special character
- Haitakiwi kuanza na namba
- Haitakiwi kuanza na underscore
- Variable ni case sensitivity kwa maana unatakiwa uzingatie matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Mfano Juma na juma ni majina mawili tofauti.
Jinsi ya kuandika variable:
Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value
Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-
- Kwa kutumia keyword var
- Kwa kutumia dynamic
- Kwa kutumia const
- Kwa final
- Utaanza na neno var likifuatiwa na jina la variable. Kisha utaweka alama ya = iikifuatiwa na value (thamani) ya variable. Unapotumia var dart yenyewe itaelewa aina ya data aina ya data itakayotumika.
Mfano
void main(){
var web = 'bongoclass';
print(web);
}
Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja
void main() {
String web = 'bongoclass';
print(web);
}
Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini
import 'dart:ffi';
void main() {
Int web = 'bongoclass';
print(web);
}
Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.
Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.
void main() {
int a, b, c;
a = 5;
b = 10;
c = 2;
print(a +b +c);
}
Hapo jibu ni 17
Pia unaweza kubadili value ya variable kwa kuitumia tena. Ila hakikisha type of data inabakia ile ile kama umetumia var.
void main() {
var x = 3;
x = 4;
print(x);
}
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
DART SOMO LA 16: String method zinazotumika kwneye Dart
Katika somo hili utakwenda kujfunza kuhusu String method zinazotumika kwenye Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 7: matumizi ya if, else, if else, else if kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Soma Zaidi...DART somo la 6: Dart operator na jinsi zinavyofanya kazi.
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi zake na jinsi ya kuzitumia.
Soma Zaidi...DART somo la 31: inheritance kwenye DART OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu inheritance, na inavyoweza kutumika kwenye Dart OOP.
Soma Zaidi...DART somo la 20: method zinazotumika kwenye map data type kwenye Dart
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye map data type
Soma Zaidi...DART somo la 45: Jinai ys kutuma mysql database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya mysql kwenye Dart. hakikisha umeelewa vyema na kutekeleza yalioelekezwa kutoka kwenye somo lililopita.
Soma Zaidi...