picha

DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart

Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.

Nini maana ya variable?

Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6

 

Sheria za variable:

  1. Haitakiwi kuanza na special character
  2. Haitakiwi kuanza na namba
  3. Haitakiwi kuanza na underscore
  4. Variable ni case sensitivity kwa maana unatakiwa uzingatie matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Mfano Juma na juma ni majina mawili tofauti.

 

Jinsi ya kuandika variable:

Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value

Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-

  1. Kwa kutumia keyword var
  2. Kwa kutumia dynamic
  3. Kwa kutumia const
  4. Kwa final

 

  1. Utaanza na neno  var likifuatiwa na jina la variable. Kisha utaweka alama ya = iikifuatiwa na value (thamani) ya variable. Unapotumia var  dart yenyewe itaelewa aina ya data aina ya data itakayotumika.

 

Mfano

void main(){

 var web = 'bongoclass';

 print(web);

}

Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja

void main() {

String web = 'bongoclass';

print(web);

}

Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini

import 'dart:ffi';

void main() {

Int web = 'bongoclass';

print(web);

}

Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.

 

Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.

void main() {

int a, b, c;

a = 5;

b = 10;

c = 2;

print(a +b +c);

}

Hapo jibu ni 17

 

Pia unaweza kubadili value ya variable kwa kuitumia tena. Ila hakikisha type of data inabakia ile ile kama umetumia var.

void main() {

var x = 3;

x = 4;

 

print(x);

}


Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: DART Main: Masomo File: Download PDF Views 936

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 ai web app     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

DART somo la 17: method za namba zinazotumika kwenye dart

Katika somo hili utakwenda kuziona method za dart zinazotumika kwenye namba. pia utajifunzakuhusu math library

Soma Zaidi...
DART somo la 13: function kwenye dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni ya kziandika na matumizi yake.

Soma Zaidi...
DART somo la 21: Jinsi ya kutengeneza library kwenye Dart

Katika somo hili utajifunza kuhusu dart library. Pia tutakwend aktengeneza library yetu wennyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.

Soma Zaidi...
DART somo la 6: Dart operator na jinsi zinavyofanya kazi.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi zake na jinsi ya kuzitumia.

Soma Zaidi...
DART somo la 39: mixin kwenye dart

Katika somo hii utakwenda kujifunza kuhusu concept mixin na jinsi inavyoweza kutumika kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 31: inheritance kwenye DART OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu inheritance, na inavyoweza kutumika kwenye Dart OOP.

Soma Zaidi...