picha

DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart

Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.

Nini maana ya variable?

Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6

 

Sheria za variable:

  1. Haitakiwi kuanza na special character
  2. Haitakiwi kuanza na namba
  3. Haitakiwi kuanza na underscore
  4. Variable ni case sensitivity kwa maana unatakiwa uzingatie matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Mfano Juma na juma ni majina mawili tofauti.

 

Jinsi ya kuandika variable:

Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value

Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-

  1. Kwa kutumia keyword var
  2. Kwa kutumia dynamic
  3. Kwa kutumia const
  4. Kwa final

 

  1. Utaanza na neno  var likifuatiwa na jina la variable. Kisha utaweka alama ya = iikifuatiwa na value (thamani) ya variable. Unapotumia var  dart yenyewe itaelewa aina ya data aina ya data itakayotumika.

 

Mfano

void main(){

 var web = 'bongoclass';

 print(web);

}

Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja

void main() {

String web = 'bongoclass';

print(web);

}

Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini

import 'dart:ffi';

void main() {

Int web = 'bongoclass';

print(web);

}

Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.

 

Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.

void main() {

int a, b, c;

a = 5;

b = 10;

c = 2;

print(a +b +c);

}

Hapo jibu ni 17

 

Pia unaweza kubadili value ya variable ">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-11-18 Topic: DART Main: ICT File: Download PDF Views 803

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

DART somo la 6: Dart operator na jinsi zinavyofanya kazi.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi zake na jinsi ya kuzitumia.

Soma Zaidi...
DART somo la 24: Dart OOP maana ya Object Oriented Programming kwenye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya OOP na faida zake. Pia utakwenda kujifunza kuhusu features za OOP.

Soma Zaidi...
DART somo la 2: syntax za dart

Katika somo hili tutatkwenda kuziona baadhi ya xyntax yaani kanunu za uandishi wa code za dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 28: Named constructor na constant constructor kwenye OOP

Ka tika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya named constructor na constant constructor kwenye Object Oriented Programming.

Soma Zaidi...
DART somo la 20: method zinazotumika kwenye map data type kwenye Dart

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye map data type

Soma Zaidi...
DART somo la 33 concept ya polymorphism

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya polymorphism.

Soma Zaidi...
DART somo la 35: Enum kwenye Dart:

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu enum na inavyotumika kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 36: Abstract class kweye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu abstract class na abstract method kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART SOMO LA 16: String method zinazotumika kwneye Dart

Katika somo hili utakwenda kujfunza kuhusu String method zinazotumika kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 11:break and continue statement kwenye Dat loop

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Dart loop za for loop na while loop.

Soma Zaidi...