picha

DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart

Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.

Nini maana ya variable?

Variable ni jina ambalo hutumika kuhifadhia data kwenye program. Jina la variable huitwa identifier. Kwa mfano ukisema x = 6 yaani x ni sawa na 6. Hivyo tunasema x ni variable ambayo inahifadhi 6

 

Sheria za variable:

  1. Haitakiwi kuanza na special character
  2. Haitakiwi kuanza na namba
  3. Haitakiwi kuanza na underscore
  4. Variable ni case sensitivity kwa maana unatakiwa uzingatie matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Mfano Juma na juma ni majina mawili tofauti.

 

Jinsi ya kuandika variable:

Kwanza utaanza na jina la variable (identifier) ikifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value ya hiyo variable. Wakati mwingine utaanza na kutaja aina ya data ikifuatiwa na jina la vaiable likifuatiwa na alama ya (=) ikifuatiwa na value

Kwenye Dart kuna njia njingi za kuandika variable kuliko baadhi ya luga nyinginezo:-

  1. Kwa kutumia keyword var
  2. Kwa kutumia dynamic
  3. Kwa kutumia const
  4. Kwa final

 

  1. Utaanza na neno  var likifuatiwa na jina la variable. Kisha utaweka alama ya = iikifuatiwa na value (thamani) ya variable. Unapotumia var  dart yenyewe itaelewa aina ya data aina ya data itakayotumika.

 

Mfano

void main(){

 var web = 'bongoclass';

 print(web);

}

Wakati mwingine kwa sababu za ki usalama utahitaji aina maalumu ya data kwenye variable yako. Hapa utataja aina ya data moja kwa moja

void main() {

String web = 'bongoclass';

print(web);

}

Kama ukiweka aina nyingine iliyo tofauti, na ambayo umeitaja itakuletea error. Angalia mfano hapo chini

import 'dart:ffi';

void main() {

Int web = 'bongoclass';

print(web);

}

Hapo kuna error kwa sababu aina ya data nilio target ni int yaani namba lakini value nilioweka ni string.

 

Pia unaweza kutengeneza variable zaidi ya moja kwenye mstari mmoja kwa kutumia aina ya data moja. Angalia mfano hapo chini variable a, b na c ni int yaani namba. Zote nimezitengeneza kwa pamoja.

void main() {

int a, b, c;

a = 5;

b = 10;

c = 2;

print(a +b +c);

}

Hapo jibu ni 17

 

Pia unaweza kubadili value ya variable kwa kuitumia tena. Ila hakikisha type of data inabakia ile ile kama umetumia var.

void main() {

var x = 3;

x = 4;

 

print(x);

}


Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: DART Main: Masomo File: Download PDF Views 891

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 ai web app     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Dart somo la 26: DART OOP maana ya object, na jinsi ya kuitengeneza kwenye OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza Object pamoja na properties. Haa kwa ufupi tutakwenda kujifunza jinsi ya kutumia class.

Soma Zaidi...
DART somo la 11:break and continue statement kwenye Dat loop

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Dart loop za for loop na while loop.

Soma Zaidi...
DART somo la 21: Jinsi ya kutengeneza library kwenye Dart

Katika somo hili utajifunza kuhusu dart library. Pia tutakwend aktengeneza library yetu wennyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.

Soma Zaidi...
DART somo la 24: Dart OOP maana ya Object Oriented Programming kwenye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya OOP na faida zake. Pia utakwenda kujifunza kuhusu features za OOP.

Soma Zaidi...
DART somo la 22: Jinsi ya kutumia html library kwenye Dart

Katika somo hili tutakwenda kujifunz ajinsi ya kutumia library ya html kwenye Dart. somo hili litakupeleka kujifunza jinsi ya ku display dart output kwenye faili la html.

Soma Zaidi...
DART somo la 12: Kuchukuwa user input kwenye Dart

Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Dart kwa ajili ya kuongeza user interaction kwenye program.

Soma Zaidi...