image

DART somo la 27: DART OOP: maana ya constructor method na jinsi inavyotumika kwenye OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jins ya kutengeneza constructor method, pia utajifunza matumizi yake kwenye OOP.

Constructor method ni nini?

Hii ni method ambayo hutumika kutengeneza object moja kwa moja, ama kuweka property kwenye object moja kwa moja. Constructor method haina return  value. Pia jina ma construct method linatakiwa liwe sawa na jina la class husika.


 

Katika somo hili tutaendelea utumia kifano yetu ya somo lililopita il tupate kuelewa zaidi. Utaona tofauti ya kutumia constructor na kutokutumia.

 

Class gari

Kwanza tutatengeneza class gari kama tulivyoona katika somo lililopita.

class gari{

String? jina;

String? rangi;

int? matairi;

 

}

Baada ya hapo ndani ya class body tutatengeneza constructor method, ambayo itakuwa na jina sawa na jina la class.

class gari{

String? jina;

String? rangi;

int? matairi;

 

   gari(){

 

    }

}

 

Properties zetu tutazipitisha kama parameter kwenye constructor method.

class gari{

String? jina;

String? rangi;

int? matairi;

 

   gari(String jina, String rangi, int matairi){

 

    }

}

 

Sasa tunakwenda kutumia properties zetu kwenye construct function. Tunapotaka kutumia property ndani ya class tunatumia keyword this. Katika somo liliopita hatukutuia keyword this  ila tulitumia ina la class moja kwa moja ni kwa sababu tulitumia prpperty nje ya class.

 

class gari {

//properties

 String? jina;

 String? rangi;

 int? matairi;

 

 //method

 gari(String jina, String rangi, int matairi){

   print(" Tunauza gari aina ya ${jina}. Ina rangi ${rangi}. Ina matairi ${matairi}.");

 

   this.jina = jina;

   this.rangi = rangi;

   this.matairi = matairi;

 }

 

}

 

Hatuwa iliobaki ni kutengeneza object na kuweka property. Kwa mujibu wa somo lililopita tulitakiwa tufanye hivi:-

gari toyota = gari();

 toyota.jina = 'Toyota avalon';

 toyota.rangi = "Nyeusi mpauko";

 toyota.matairi = 4;


 

Ila kwa kuwa tmetumia constrct method, tutaweza kutengeneza object na kuweka value kwenye properties zake moja kwa moja kw akufanya hivi:-

gari toyota = gari( "Toyota Avalon", "nyeusi", 4);

Zingatia huo mpagilio naendana na mpangilio wa parameter kwenye construct method. Hivyo code zote zitaonekana hivi:-

class gari {

//properties

 String? jina;

 String? rangi;

 int? matairi;

 

 //method

 gari(String jina, String rangi, int matairi){

   print(" Tunauza gari aina ya ${jina}. Ina rangi ${rangi}. Ina matairi ${matairi}.");

 

   this.jina = jina;

   this.rangi = rangi;

   this.matairi = matairi;

 }

 

}

 

void main(){

 gari toyota = gari( "Toyota Avalon", "nyeusi", 4);

}

 

 

">...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 305


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

DART somo la 44: Jinsi ya ku install mysql kwenye program ya dart
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuunganisha databse na Dart. Pia utajifunza jinsi ya kuset environment kwenye kompyuta ili kuweza kutumia Dart sdk kwenye CMD. Soma Zaidi...

DART somo la 11:break and continue statement kwenye Dat loop
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Dart loop za for loop na while loop. Soma Zaidi...

DART - somo la 1: Kazi za dart programming na historia yake
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kazi za dart language. Pia nimekuandalia istoria fupi ya lugha ya DART. Soma Zaidi...

DART somo la 8: Matumizi ya switch case
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu switch case na jinsi inavyofanya kazi kwenye Dart. Soma Zaidi...

DART somo la 3: Aina za Data
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart. Soma Zaidi...

DART somo la 37: Class interface
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class interface na inavyotofautiana na class abstract Soma Zaidi...

DART somo la 41: concept ya generic kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya generics ili kuweza kufanya kazi na aina mbalimbali za data kwenye class. Soma Zaidi...

DART somo la 22: Jinsi ya kutumia html library kwenye Dart
Katika somo hili tutakwenda kujifunz ajinsi ya kutumia library ya html kwenye Dart. somo hili litakupeleka kujifunza jinsi ya ku display dart output kwenye faili la html. Soma Zaidi...

DART somo la 7: matumizi ya if, else, if else, else if kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement Soma Zaidi...

DART somo la 13: function kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni ya kziandika na matumizi yake. Soma Zaidi...

Dart somo la 25: DART OOP Nini maaan ya class na vipi utaweza kuitengeneza
Katika somo hili utajifunza maana ya class kwenye OOP paradigm, kisha utajifunza jinsi ya kutengeneza class. Soma Zaidi...

DART somo la 24: Jinsi ya kutengeneza faili, folda na kuingiza data
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika data kwenye faili. Kwanza utajifunza kutengeneza folda, kisha faili na kuweka data, kisha utajifunza kufuta fali. Soma Zaidi...