DART somo la 15: parameter kwenye function za Dart
Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Dart function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function
Prameter zinatakiwa zifuate utaratibu:
Unapoweka parameter unaziweka kwenye mpangilio, hivyo hata wakati wa kuweka argument unatakiwa ufuate utaratibu huo huo. Mfano kama function ina parameter 2 ya umri na jinsia, basi wakati wa kuweka argument ifuate utaratibu ho huo. Pia unatakiwa kuzingatia na aina zake za data. Kama parameter inahitaji namba wewe unaweka string hapa utasababisha error.
import 'dart:io';
haloo(umri, jinsia){
print('umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
haloo(umri, jinsia);
}
Sasa hapo kama utachanganya mpangilio wa aprameter aina za data utaishia kupata error
Unaweza kuwa na default parameter
Default parameter ni parameter ambayo inakuwa umeshawekwa, hivyo mtumiaji wa program hana haja ya kujaza kitu. Kwa mfano katika program yetu ya hapo juu tunakwenda kuongeza parameter nyingine ambayo itaonyesha makazi. Tutaweka Tanzania kama default parameter
Ili uweze kuandika default parameter utaiweka ndani ya mabano {} utai declare kwa alama ya ( = ). Mfano {makazi = ‘Tanzania’}
import 'dart:io';
haloo(umri, jinsia, {makazi ='Tanzania'}){
print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi ${makazi}');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
haloo(umri, jinsia);
}
Pia unaweza kuweka parameter ambayo sio lazima ijazwe hivyo inakuwa ni optional. Parameter hii inaweza kuwa ni default parameter. Na endapo hutakuwa na default arameter yenyewe itabeba value null kumaanisha haina kitu. Kwa mfano hapo tunataka kuongeza parameter ya kuweka jina la mkoa. Hiyo ttaifanya sio lazima ijazwe yaani option.
Ili kuweka optional parameter tutaiweka ndani ya mabano [] kisha utaweka aina yake ya data ikifuatiwa na alama ya ? mfano [String? mkoa]
import 'dart:io';
haloo(int umri, String jinsia, [String? mkoa]){
print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi $mkoa');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
print('Andika Mkoa unaoishi');
String mkoa = stdin.readLineSync()!;
...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 29: Dart encapsulation
Katika somo hili tutawenda kujifunza kuhusu encapsulatio kwenye Dart OOP na jinsi inavyoweza kutumika.
Soma Zaidi...DART somo la 45: Jinai ys kutuma mysql database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya mysql kwenye Dart. hakikisha umeelewa vyema na kutekeleza yalioelekezwa kutoka kwenye somo lililopita.
Soma Zaidi...DART somo la 28: Named constructor na constant constructor kwenye OOP
Ka tika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya named constructor na constant constructor kwenye Object Oriented Programming.
Soma Zaidi...DART somo la 27: DART OOP: maana ya constructor method na jinsi inavyotumika kwenye OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jins ya kutengeneza constructor method, pia utajifunza matumizi yake kwenye OOP.
Soma Zaidi...DART somo la 41: concept ya generic kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya generics ili kuweza kufanya kazi na aina mbalimbali za data kwenye class.
Soma Zaidi...