picha

DART somo la 15: parameter kwenye function za Dart

Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Dart function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function

Prameter zinatakiwa zifuate utaratibu:

Unapoweka parameter unaziweka kwenye mpangilio, hivyo hata wakati wa kuweka argument unatakiwa ufuate utaratibu huo huo. Mfano kama function ina parameter 2 ya umri na jinsia, basi wakati wa kuweka argument ifuate utaratibu ho huo. Pia unatakiwa kuzingatia na aina zake za data. Kama parameter inahitaji namba wewe unaweka string hapa utasababisha error.

 

import 'dart:io';

haloo(umri, jinsia){

 print('umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia');

}

 

void main(){

 print('Andika umri wako');

 int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);

 print('Andika jinsia yako');

 String jinsia = stdin.readLineSync()!;

 haloo(umri, jinsia);

}

Sasa hapo kama utachanganya mpangilio wa aprameter aina za data utaishia kupata error


 

Unaweza kuwa na default parameter

Default parameter ni parameter ambayo inakuwa umeshawekwa, hivyo mtumiaji wa program hana haja ya kujaza kitu. Kwa mfano katika program yetu ya hapo juu tunakwenda kuongeza parameter nyingine ambayo itaonyesha makazi. Tutaweka Tanzania kama default parameter

 

Ili uweze kuandika default parameter utaiweka ndani ya mabano {} utai declare kwa alama ya ( = ). Mfano {makazi = ‘Tanzania’}

 

import 'dart:io';

haloo(umri, jinsia, {makazi ='Tanzania'}){

 print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi ${makazi}');

}

 

void main(){

 print('Andika umri wako');

 int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);

 print('Andika jinsia yako');

 String jinsia = stdin.readLineSync()!;

 haloo(umri, jinsia);

}

 

Pia unaweza kuweka parameter ambayo sio lazima ijazwe hivyo inakuwa ni optional. Parameter hii inaweza kuwa ni default parameter. Na endapo hutakuwa na default arameter yenyewe itabeba value null kumaanisha haina kitu. Kwa mfano hapo tunataka kuongeza parameter ya kuweka jina la mkoa. Hiyo ttaifanya sio lazima ijazwe yaani option.

 

Ili kuweka optional parameter tutaiweka ndani ya mabano [] kisha utaweka aina yake ya data ikifuatiwa na alama ya ? mfano [String? mkoa]

import 'dart:io';

haloo(int umri, String jinsia, [String? mkoa]){

 print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi $mkoa');

}

 

void main(){

 print('Andika umri wako');

 int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);

 print('Andika jinsia yako');

 String jinsia = stdin.readLineSync()!;

 print('Andika Mkoa u">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-11-24 Topic: DART Main: ICT File: Download PDF Views 981

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 ai web app    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

DART SOMO LA 14: Aina za function kwenye Dart

Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la function. Hapa tutakwenda kuona aina za function.

Soma Zaidi...
DART somo la 22: Jinsi ya kutumia html library kwenye Dart

Katika somo hili tutakwenda kujifunz ajinsi ya kutumia library ya html kwenye Dart. somo hili litakupeleka kujifunza jinsi ya ku display dart output kwenye faili la html.

Soma Zaidi...
DART somo la 13: function kwenye dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni ya kziandika na matumizi yake.

Soma Zaidi...
DART somo la 44: Jinsi ya ku install mysql kwenye program ya dart

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuunganisha databse na Dart. Pia utajifunza jinsi ya kuset environment kwenye kompyuta ili kuweza kutumia Dart sdk kwenye CMD.

Soma Zaidi...
DART somo la 32: Inheritance kwenye construct method:

Katika masomo yaliopita tumesha jifunza jinsi inheritance inavyokuwa, ila hatujaona kwa namna gani utaweza ku inherit constructor method. Somo hili litashughulika na swla hilo.

Soma Zaidi...
DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 34: Static variable kwenye Dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static property na jinsi ambavyo inavyotumika.

Soma Zaidi...
DART somo la 41: concept ya generic kwenye dart

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya generics ili kuweza kufanya kazi na aina mbalimbali za data kwenye class.

Soma Zaidi...
DART somo la 35: Enum kwenye Dart:

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu enum na inavyotumika kwenye Dart.

Soma Zaidi...
DART somo la 24: Jinsi ya kutengeneza faili, folda na kuingiza data

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika data kwenye faili. Kwanza utajifunza kutengeneza folda, kisha faili na kuweka data, kisha utajifunza kufuta fali.

Soma Zaidi...