DART somo la 15: parameter kwenye function za Dart
Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Dart function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function
Prameter zinatakiwa zifuate utaratibu:
Unapoweka parameter unaziweka kwenye mpangilio, hivyo hata wakati wa kuweka argument unatakiwa ufuate utaratibu huo huo. Mfano kama function ina parameter 2 ya umri na jinsia, basi wakati wa kuweka argument ifuate utaratibu ho huo. Pia unatakiwa kuzingatia na aina zake za data. Kama parameter inahitaji namba wewe unaweka string hapa utasababisha error.
import 'dart:io';
haloo(umri, jinsia){
print('umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
haloo(umri, jinsia);
}
Sasa hapo kama utachanganya mpangilio wa aprameter aina za data utaishia kupata error
Unaweza kuwa na default parameter
Default parameter ni parameter ambayo inakuwa umeshawekwa, hivyo mtumiaji wa program hana haja ya kujaza kitu. Kwa mfano katika program yetu ya hapo juu tunakwenda kuongeza parameter nyingine ambayo itaonyesha makazi. Tutaweka Tanzania kama default parameter
Ili uweze kuandika default parameter utaiweka ndani ya mabano {} utai declare kwa alama ya ( = ). Mfano {makazi = ‘Tanzania’}
import 'dart:io';
haloo(umri, jinsia, {makazi ='Tanzania'}){
print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi ${makazi}');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
haloo(umri, jinsia);
}
Pia unaweza kuweka parameter ambayo sio lazima ijazwe hivyo inakuwa ni optional. Parameter hii inaweza kuwa ni default parameter. Na endapo hutakuwa na default arameter yenyewe itabeba value null kumaanisha haina kitu. Kwa mfano hapo tunataka kuongeza parameter ya kuweka jina la mkoa. Hiyo ttaifanya sio lazima ijazwe yaani option.
Ili kuweka optional parameter tutaiweka ndani ya mabano [] kisha utaweka aina yake ya data ikifuatiwa na alama ya ? mfano [String? mkoa]
import 'dart:io';
haloo(int umri, String jinsia, [String? mkoa]){
print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi $mkoa');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
print('Andika Mkoa unaoishi');
String mkoa = stdin.readLineSync()!;
...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 ai web app 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
DART somola 42: Asynchronous programming
Katika somo hili tutakwenda kujifunza concept nyingine ya asynchronous programming.
Soma Zaidi...DART somo la 20: method zinazotumika kwenye map data type kwenye Dart
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye map data type
Soma Zaidi...DART somo la 24: Dart OOP maana ya Object Oriented Programming kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya OOP na faida zake. Pia utakwenda kujifunza kuhusu features za OOP.
Soma Zaidi...DART somo la 7: matumizi ya if, else, if else, else if kwenye Dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Soma Zaidi...DART somo la 37: Class interface
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class interface na inavyotofautiana na class abstract
Soma Zaidi...DART somo la 39: mixin kwenye dart
Katika somo hii utakwenda kujifunza kuhusu concept mixin na jinsi inavyoweza kutumika kwenye Dart.
Soma Zaidi...