DART somo la 15: parameter kwenye function za Dart
Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Dart function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function
Prameter zinatakiwa zifuate utaratibu:
Unapoweka parameter unaziweka kwenye mpangilio, hivyo hata wakati wa kuweka argument unatakiwa ufuate utaratibu huo huo. Mfano kama function ina parameter 2 ya umri na jinsia, basi wakati wa kuweka argument ifuate utaratibu ho huo. Pia unatakiwa kuzingatia na aina zake za data. Kama parameter inahitaji namba wewe unaweka string hapa utasababisha error.
import 'dart:io';
haloo(umri, jinsia){
print('umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
haloo(umri, jinsia);
}
Sasa hapo kama utachanganya mpangilio wa aprameter aina za data utaishia kupata error
Unaweza kuwa na default parameter
Default parameter ni parameter ambayo inakuwa umeshawekwa, hivyo mtumiaji wa program hana haja ya kujaza kitu. Kwa mfano katika program yetu ya hapo juu tunakwenda kuongeza parameter nyingine ambayo itaonyesha makazi. Tutaweka Tanzania kama default parameter
Ili uweze kuandika default parameter utaiweka ndani ya mabano {} utai declare kwa alama ya ( = ). Mfano {makazi = ‘Tanzania’}
import 'dart:io';
haloo(umri, jinsia, {makazi ='Tanzania'}){
print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi ${makazi}');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
haloo(umri, jinsia);
}
Pia unaweza kuweka parameter ambayo sio lazima ijazwe hivyo inakuwa ni optional. Parameter hii inaweza kuwa ni default parameter. Na endapo hutakuwa na default arameter yenyewe itabeba value null kumaanisha haina kitu. Kwa mfano hapo tunataka kuongeza parameter ya kuweka jina la mkoa. Hiyo ttaifanya sio lazima ijazwe yaani option.
Ili kuweka optional parameter tutaiweka ndani ya mabano [] kisha utaweka aina yake ya data ikifuatiwa na alama ya ? mfano [String? mkoa]
import 'dart:io';
haloo(int umri, String jinsia, [String? mkoa]){
print(' umri wako ni miaka ${umri} na jinsia yako ni $jinsia unaishi $mkoa');
}
void main(){
print('Andika umri wako');
int umri = int.parse(stdin.readLineSync()!);
print('Andika jinsia yako');
String jinsia = stdin.readLineSync()!;
print('Andika Mkoa unaoishi');
String mkoa = stdin.readLineSync()!;
...Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
DART somo la 4: Jinsi ya kuandika na kutumia variable kwenye Dart
Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable kwenye Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 11:break and continue statement kwenye Dat loop
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Dart loop za for loop na while loop.
Soma Zaidi...DART somo la 29: Dart encapsulation
Katika somo hili tutawenda kujifunza kuhusu encapsulatio kwenye Dart OOP na jinsi inavyoweza kutumika.
Soma Zaidi...DART somo la 41: concept ya generic kwenye dart
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu concept ya generics ili kuweza kufanya kazi na aina mbalimbali za data kwenye class.
Soma Zaidi...DART SOMO LA 16: String method zinazotumika kwneye Dart
Katika somo hili utakwenda kujfunza kuhusu String method zinazotumika kwenye Dart.
Soma Zaidi...DART somo la 10: while loop na do while loop kwenye Dart
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Dart.
Soma Zaidi...