picha

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama




Mtume (s.a.w) pia ametutajia dalili kubwa za kukaribia kwa siku ya Mwisho. Dalili hizo zinapatikana katika Qur’an na Hadith kama inavyobainishwa hapa chini:“Na kitakapokaribia Kiyama, tutawatolea mnyama kutoka ardhini atawaeleza (watu) kwa kuwa watu walikuwa hawaziamini aya zetu” (27:82)“Mpaka watakapofunguliwa Ya’juj na Ma’juj nao wataporomoka kwa kasi, na ikakaribia ahadi ya kweli kufunguliwa, hesabu na malipo, basi wakati huo macho ya makafiriyatatokeza mno juu ” (21:96 – 97)
Katika hadith aliyoipokea Imam Ahmad, na kusimuliwa na Khudhaifa Ibn Usaid Al – Ghifaar (r.a) amesema; Alitutokea Mtume (s.aw) kutoka chumbani kwake na sisi tukikumbushana jambo la kiyama, Mtume (s.a.w) akasema: Hakitosimama Kiyama mpaka muone alama kumi,



1. Kuchomoza jua Magharibi



2. Kutokea moshi mkubwa utakaochafua mazingira (pollution)



3. Mnyama atatokeza na kuwasemesha watu (27:82)



4. Kufunguliwa Ya’juj na Ma’juj (21:96 97)



5. Kurudi kwa Issa mwana wa Maryam



6.Kuja kwa Masih Dajal (False Messayah)



7.Kutoka Moto (Volcano) katika pango la Aden ukiwaendesha watu



8.Dunia kugawika mapande matatu (Three Blocks); Pande la Mashariki (Eastern Block)



9.Pande la Magharibi na (western block)



10.Bara Arab (Mashariki ya kati - Middle East)
Kwa hakika Qur’an imetaja dalili nyingi mno, Rejea Suratul qiyaamah (75:6 – 9) na nyinginezo nyingi zilizotajwa katika hadith mbali mbali.
Kuamini siku ya mwisho ni kuamini kuwa kuna maisha ya milele baada ya maisha haya ya hapa duniani. Kwa mujibu wa mafundisho ya Qur-an, maisha hayo yatakuwa na hatua kuu nne zifu atazo:



(i)kutokwa na roho



(ii)Maisha ya kaburini - Barzakh.



(iii)Kufufuka na kuhudhurishwa mbele ya Allah (s.w) na kuhesabiwa.



(iv)Maisha ya kukaa Peponi milele kwa watu wema au kukaa motoni kwa watu waovu.Aidha kwa kuzingatia matukio yatakayotokea katika hatua nne za maisha yajayo,





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 9324

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 web hosting     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...
Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.

Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.

Soma Zaidi...
Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

عَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَيْضًا قَالَ: " بَيْنَمَا نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ذَاتَ يَوْمٍ، إذْ ?...

Soma Zaidi...