Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Download Post hii hapa

Muumini wa kweli huishi katika kila kipengele cha maisha yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w), na hii kama ifuatavyo;

 

  1. Kupata ukombozi kutokana na utumwa wa aina zote;

Huu hupatikana baada ya mtu kuwa huru na kuishi kwa kufuata taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w) pekee.

Rejea Qur’an (12:39).

 

       (ii)  Mwanaadamu huwa mwadilifu katika utendaji wa maisha yake ya kila siku;

Muumini wa kweli hufanya mema na kuepuka maovu bila hata ya kusimamiwa au      kuonekana na watu, kwa kujua kuwa mjuzi pekee ni Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Qur’an (50:16).

 

        (iii)  Humfanya mwanaadamu kuwa mpole, mvumilivu na mwenye huruma;

Mwanaadamu huwa mpole hasa kwa wenye shida na matatizo na pia kuwa na subra anapofikwa na mitihani na kujiepusha na kibri, majivuno na kujiona.

Rejea Qur’an (6:165).

 

     (iv)  Humfanya mja kuwa jasiri katika kusimamia haki, uadilifu na usawa katika jamii;

Muumini wa kweli huwa shujaa katika kupambana na dhulma na ukandamizaji wa aina yeyote na kupigania haki bila kumchelea mtu yeyote.

Rejea Qur’an (4:74), (5:45) na (9:111).

 

        (v)  Humfanya mja kuwa na mtazamo mpana na sahihi juu ya maisha;

Muumini wa kweli kamwe hawi na fikra na mtazamo finyu katika kuyaendea maisha yake ya kila siku kwa kujua lengo, thamani na nafasi yake juu ya maisha ya Akhera.

Rejea Qur’an (15:9).

 

        (vi) Humuwezesha mja kuwa mwenye kukinai na kutosheka;

Muumini wa kweli hutosheka na kuridhika na kile alichokadiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w) iwe kwa kupungukiwa au kuzidishiwa, yote kwake anashukuru.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2320

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kuamini siku ya mwisho
Kuamini siku ya mwisho

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.
Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.

Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kula mali ya Yatima
Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah
Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah

Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu

Soma Zaidi...
Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?
Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?

Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida

Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?

Soma Zaidi...