Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Muumini wa kweli huishi katika kila kipengele cha maisha yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w), na hii kama ifuatavyo;

 

  1. Kupata ukombozi kutokana na utumwa wa aina zote;

Huu hupatikana baada ya mtu kuwa huru na kuishi kwa kufuata taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w) pekee.

Rejea Qur’an (12:39).

 

       (ii)  Mwanaadamu huwa mwadilifu katika utendaji wa maisha yake ya kila siku;

Muumini wa kweli hufanya mema na kuepuka maovu bila hata ya kusimamiwa au      kuonekana na watu, kwa kujua kuwa mjuzi pekee ni Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Qur’an (50:16).

 

        (iii)  Humfanya mwanaadamu kuwa mpole, mvumilivu na mwenye huruma;

Mwanaadamu huwa mpole hasa kwa wenye shida na matatizo na pia kuwa na subra anapofikwa na mitihani na kujiepusha na kibri, majivuno na kujiona.

Rejea Qur’an (6:165).

 

     (iv)  Humfanya mja kuwa jasiri katika kusimamia haki, uadilifu na usawa katika jamii;

Muumini wa kweli huwa shujaa katika kupambana na dhulma na ukandamizaji wa aina yeyote na kupigania haki bila kumchelea mtu yeyote.

Rejea Qur’an (4:74), (5:45) na (9:111).

 

        (v)  Humfanya mja kuwa na mtazamo mpana na sahihi juu ya maisha;

Muumini wa kweli kamwe hawi na fikra na mtazamo finyu katika kuyaendea maisha yake ya kila siku kwa kujua lengo, thamani na nafasi yake juu ya maisha ya Akhera.

Rejea Qur’an (15:9).

 

        (vi) Humuwezesha mja kuwa mwenye kukinai na kutosheka;

Muumini wa kweli hutosheka na kuridhika na kile alichokadiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w) iwe kwa kupungukiwa au kuzidishiwa, yote kwake anashukuru.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2657

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Njia ambazo Allah hufundisha wanadamu elimu mbalimbali

Ni kipi chanzo cha Elimu, na ni kwa namna gani Allah hufundisha Elimu kwa wanadamu?

Soma Zaidi...
Mazingatio kabla ya kuosha maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku

Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.

Soma Zaidi...