Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Muumini wa kweli huishi katika kila kipengele cha maisha yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w), na hii kama ifuatavyo;

 

  1. Kupata ukombozi kutokana na utumwa wa aina zote;

Huu hupatikana baada ya mtu kuwa huru na kuishi kwa kufuata taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w) pekee.

Rejea Qur’an (12:39).

 

       (ii)  Mwanaadamu huwa mwadilifu katika utendaji wa maisha yake ya kila siku;

Muumini wa kweli hufanya mema na kuepuka maovu bila hata ya kusimamiwa au      kuonekana na watu, kwa kujua kuwa mjuzi pekee ni Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Qur’an (50:16).

 

        (iii)  Humfanya mwanaadamu kuwa mpole, mvumilivu na mwenye huruma;

Mwanaadamu huwa mpole hasa kwa wenye shida na matatizo na pia kuwa na subra anapofikwa na mitihani na kujiepusha na kibri, majivuno na kujiona.

Rejea Qur’an (6:165).

 

     (iv)  Humfanya mja kuwa jasiri katika kusimamia haki, uadilifu na usawa katika jamii;

Muumini wa kweli huwa shujaa katika kupambana na dhulma na ukandamizaji wa aina yeyote na kupigania haki bila kumchelea mtu yeyote.

Rejea Qur’an (4:74), (5:45) na (9:111).

 

        (v)  Humfanya mja kuwa na mtazamo mpana na sahihi juu ya maisha;

Muumini wa kweli kamwe hawi na fikra na mtazamo finyu katika kuyaendea maisha yake ya kila siku kwa kujua lengo, thamani na nafasi yake juu ya maisha ya Akhera.

Rejea Qur’an (15:9).

 

        (vi) Humuwezesha mja kuwa mwenye kukinai na kutosheka;

Muumini wa kweli hutosheka na kuridhika na kile alichokadiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w) iwe kwa kupungukiwa au kuzidishiwa, yote kwake anashukuru.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2358

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Mtazamo wa uislamu juu ya dini

Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Mafundisho ya Mitume

Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s.

Soma Zaidi...
KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida

Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri

Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera.

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...