Qur-an, vile vile inatufunza mahusiano tunayotakiwa tuwe nayo ili kuondoa chuki na uadui na kupandikiza mapenzi miongoni mwa wanajamii kama tunavyojifunza katika sura zifuatazo:
Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yoyote ila Yeye tu. Na (ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee, (naye yuko) pamoja nawe, au wote wawili, basi usiwaambie hata Ah! Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa hishima (kabisa). Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa (njia ya kuwaonea) huruma na useme: "Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto." Mola wenu anajua sana yaliyo nyoyoni mwenu. Kama mkiwa wema (kwa wazee wenu daima; lakini mara moja mbili hivi mkapotea, basi atakusameheni) kwani Yeye ni Mwenye kuwaghufiria wenye kurejea (kwake). (17:23-25)
Na umpe jamaa (yako) haki yake, na maskini na msafiri aliyeharibikiwa, wala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu. Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu wa mashetani (wanamfuata Shetani). Na Shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake. (1 7:26-2 7)
Na kama unajipurukusha nao (sasa hivi kwa kuwa huna kitu) lakini unatafuta rehema ya Mola wako (riziki) unayoitumai, basi sema nao maneno laini (ya kuwapa waadi ya kuwa ukipata utawapa). Wala usifanye mkono wako (kama) uliofungwa shingoni mwako, wala usiukunjue ovyo, utakuwa ni mwenye kulaumiwa (ukifanya hivyo) na kufilisika (ukiukunjua ovyo ovyo). (17:28-29)
Hakika Mola wako humkunjulia rikizi amtakaye na humdhikishia (amtakaye). Hakika Yeye kwa waja wake ni Mwenye kuwajua na kuwaona; (anajua yupi anayestahiki utajiri na yupi anayestahiki ufakiri). (17:30)
"Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa umasikini. Sisi ndio tunaowaruzuku wao na nyinyi (pia). Kwa yakini kuwauwa ni khatia kubwa. Wala msikaribie zinaa. Hakika hiyo (zinaa) ni uchafu (mkubwa) na ni njia mbaya (kabisa). (17:31-32)
Wala msiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha (kuuliwa) isipokuwa kwa haki. Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi tumempa nguvu mrithi wake. Basi (mrithi ) asifanye fujo katika kuua (kwa ajili ya huyo mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na sharia maadam anayo haki). (17:33)
Wala msiyakaribie (msiyaguse) mali ya yatima, isipokuwa kwa njia iliyo bora mpaka afike baleghe yake (huyo yatima akabidhiwe mwenyewe). Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi itaulizwa (Siku ya Kiama). Na timizeni kipimo mpimapo; na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni wema kwenu na bora mwishoni (kwake). (17:34-35)
Wala usifuate usiyo na ilimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio na macho na moyo; hivyo vyote vitaulizwa. Wala usitembee (usende) katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa milima. (Basi unajivuna nini). (1 7:36-3 7)
Haya yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako.(1 7:38)
Haya ni katika yale aliyokufunulia Mola wako katika hikima (zake). Wala usimueke pamoja na Mwenyezi Mungu, Mungu mwengine, usije kutupwa katika Jahanamu hali ya kuwa mwenye kulaumiwa (na) mwenye kufukuzwa (huku na huku). (1 7:39)
Aya hizi zinatufundisha kuwa ili tuweze kuishi vizuri katika jamii hatuna budi kushikamana na maamrisho kadhaa yaliyoainishwa na kujiepusha na makatazo kadhaa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:1 Kumuamini Allah (s.
Soma Zaidi...Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.
Soma Zaidi...Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali.
Soma Zaidi...Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi.
Soma Zaidi...Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.
Soma Zaidi...Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.
Soma Zaidi...