image

Maadili na malezi ya jamii

Maadili na malezi ya jamii

3. Maadili na malezi ya jamii



Qur-an, vile vile inatufunza mahusiano tunayotakiwa tuwe nayo ili kuondoa chuki na uadui na kupandikiza mapenzi miongoni mwa wanajamii kama tunavyojifunza katika sura zifuatazo:


Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yoyote ila Yeye tu. Na (ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee, (naye yuko) pamoja nawe, au wote wawili, basi usiwaambie hata Ah! Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa hishima (kabisa). Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa (njia ya kuwaonea) huruma na useme: "Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto." Mola wenu anajua sana yaliyo nyoyoni mwenu. Kama mkiwa wema (kwa wazee wenu daima; lakini mara moja mbili hivi mkapotea, basi atakusameheni) kwani Yeye ni Mwenye kuwaghufiria wenye kurejea (kwake). (17:23-25)



Na umpe jamaa (yako) haki yake, na maskini na msafiri aliyeharibikiwa, wala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu. Hakika watumiao kwa ubadhirifu ni ndugu wa mashetani (wanamfuata Shetani). Na Shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake. (1 7:26-2 7)


Na kama unajipurukusha nao (sasa hivi kwa kuwa huna kitu) lakini unatafuta rehema ya Mola wako (riziki) unayoitumai, basi sema nao maneno laini (ya kuwapa waadi ya kuwa ukipata utawapa). Wala usifanye mkono wako (kama) uliofungwa shingoni mwako, wala usiukunjue ovyo, utakuwa ni mwenye kulaumiwa (ukifanya hivyo) na kufilisika (ukiukunjua ovyo ovyo). (17:28-29)


Hakika Mola wako humkunjulia rikizi amtakaye na humdhikishia (amtakaye). Hakika Yeye kwa waja wake ni Mwenye kuwajua na kuwaona; (anajua yupi anayestahiki utajiri na yupi anayestahiki ufakiri). (17:30)


"Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa umasikini. Sisi ndio tunaowaruzuku wao na nyinyi (pia). Kwa yakini kuwauwa ni khatia kubwa. Wala msikaribie zinaa. Hakika hiyo (zinaa) ni uchafu (mkubwa) na ni njia mbaya (kabisa). (17:31-32)



Wala msiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha (kuuliwa) isipokuwa kwa haki. Na mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi tumempa nguvu mrithi wake. Basi (mrithi ) asifanye fujo katika kuua (kwa ajili ya huyo mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na sharia maadam anayo haki). (17:33)


Wala msiyakaribie (msiyaguse) mali ya yatima, isipokuwa kwa njia iliyo bora mpaka afike baleghe yake (huyo yatima akabidhiwe mwenyewe). Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi itaulizwa (Siku ya Kiama). Na timizeni kipimo mpimapo; na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni wema kwenu na bora mwishoni (kwake). (17:34-35)


Wala usifuate usiyo na ilimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio na macho na moyo; hivyo vyote vitaulizwa. Wala usitembee (usende) katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa milima. (Basi unajivuna nini). (1 7:36-3 7)



Haya yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako.(1 7:38)


Haya ni katika yale aliyokufunulia Mola wako katika hikima (zake). Wala usimueke pamoja na Mwenyezi Mungu, Mungu mwengine, usije kutupwa katika Jahanamu hali ya kuwa mwenye kulaumiwa (na) mwenye kufukuzwa (huku na huku). (1 7:39)
Aya hizi zinatufundisha kuwa ili tuweze kuishi vizuri katika jamii hatuna budi kushikamana na maamrisho kadhaa yaliyoainishwa na kujiepusha na makatazo kadhaa.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 549


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Maadili katika surat luqman
Soma Zaidi...

Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?
Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Muโ€™uminuun (23:1-11)
Soma Zaidi...

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu
Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu. Soma Zaidi...

Kujiepusha na maringo na majivuno
Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri. Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...

Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu. Soma Zaidi...

Dalili (Alama) za Qiyama
Soma Zaidi...

Lengo la kuletwa mitume
Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:โ€œKwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere.. Soma Zaidi...

Taqwa (Hofu ya kumuogopa Allah) ni popote ulipo
ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุฐูŽุฑูู‘ ุฌูู†ู’ุฏูŽุจู ุจู’ู†ู ุฌูู†ูŽุงุฏูŽุฉูŽุŒ ูˆูŽุฃูŽุจููŠ ุนูŽุจู’ุฏู ุงู„ุฑูŽู‘ุญู’ู…ูŽู†ู ู…ูุนูŽุงุฐู ุจู’ู†ู ุฌูŽุจูŽู„ู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ูู…ูŽุงุŒ ุนูŽู†ู’ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽ... Soma Zaidi...