image

Maamrisho ya kushikamana nayo

Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.

Maamrisho ya kushikamana nayo

(1) Maamrisho ya kushikamana nayo



Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo:
(i)Kumuabudu Allah (s.w) Peke yake
Kumuabudu Allah (s.w) peke yake ndilo jukumu la kwanza kwa Muumini na hasa ndio lengo la kuumbwa binaadamu (rejea Qur-an 51:56). Kumuabudu Allah (s.w), ni kumtii kwa unyenyekevu katika kukiendea kila kipengele cha maisha ya binafsi na ya jamii.



(ii)Kuwafanyia wema na kuwahurumia wazazi Ni wajibu kwa Waumini kuwafanyia wema wazazi wao. Kuwafanyia wema wazazi ni pamoja na kuwafanyia yafuatayo:
(a) Kuwatii katika yale yote yanayowafikiana na sharia ya
Allah (s.w).Wazazi watakapowaamrisha watoto wao
wafanye mambo ambayo ni kinyume na amri za Allah (s.w) na Mtume wake, hawatapaswa kuwatii, bali watoto waumini wanapaswa kuwakatalia hao wazazi wao kwa adabu na heshima kubwa kwa kuwajibu kwa upole na kwa kauli nzuri.



(b)Kuwaheshimu wazazi kwa kuongea nao kwa upole na kwa huruma. Pia ni pamoja na kujiepusha na kujibizana nao, hata tu kuwagunia au hata kuwapuuza kwa ishara.



(c)Kuwahurumia wazazi kwa kuwapa msaada wowote wanaohitajia kwa kadiri ya uwezo wao, ila tu msaada huo uzingatie mipaka ya Allah (s.w) na Mtume wake.



(d)Kuwausia wazazi wao kumcha Allah (s.w) na kuwaombea dua na msamaha kwa Allah (s.w) kama tunavyoelekezwa na Allah (s.w) katika Qur-an:


"Mola wetu nighufirie mimi na wazazi wangu na wale wote wanaoamini siku ya Hisabu". (14:41)


Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu na akamzaa kwa taabu. Na kubeba mimba yake hata kumwachisha ziwa; (uchache wake) ni miezi thalathini. Hata anapofikia baleghe yake na akawa mwenye umri wa miaka arubaini, (mtoto mwema) husema: - "Ee Mola wangu! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizonineemesha mimi na wazazi wangu na niwezeshe nifanye vitendo vizuri unavyovipenda, na unitengenezee watoto wangu; kwa yakini ninatubu kwako; na hakika mimi ni miongoni mwa waliosilimu (walionyenyekea)." (46:15)


(iii)Kutoa mali katika kuwasaidia wanaohitajia
Muumini anawajibika kutoa msaada wa mali na hali kuwapa wanaohitajia. Katika utaratibu wa kutoa msaada utaanza na jamaa zako wa karibu kisha ndio uwaangalie wahitaji wengine ikiwa ni pamoja na maskini, wasafiri walioharibikiwa na wengineo kama walivyoainishwa katika Qur-an (2:177), (4:36) na (51:19).Kama huna cha kutoa, angalau mliwaze huyo mwenye kuhitajia kwa kumpa maneno ya faraja na ya matumaini:


"Kauli njema na kusamehe ni bora kuliko sadaqa inayofuatishwa na udhia, na Mwenyezi Mungu ndiye Mkwasi na Mpole. (2:263)



(iv)Kutimiza vipimo
Waumini wanawajibika kuwa waadilifu wakati wa kuuziana kwa kukamilisha vipimo vya uzito, ujazo, urefu, n.k. Kufanya ujanja au ubabaishaji wowote katika vipimo ni katika makosa makubwa mbele ya Allah (s.w):


"Maangamizo yatawathubutikia wapunjao . Ambao wanapojipimia kwa watu hupokea (kipimo) kamili. Lakini wanapowapimia kwa (kipimo cha) vibaba au mizani (au vinginevyo) wao hupunguza. (83 1-3)


Je! Wao hawafikiri ya kwamba watafufuliwa; katika siku iliyo Kuu. (83:4-5)


Siku watakaposimama watu (wote) mbele ya Mola walimwengu wote?" (83:6)


(v) Kutimiza Ahadi
Ahadi ni deni ambalo linamlazimu Muumini kulilipa. Asiyetimiza ahadi kwa mujibu wa Qur-an (17:34) atakuwa ni mkosaji na siku ya Hukumu atasimamishwa kizimbani mbele ya Mahakama ya Allah (s.w) aulizwe juu ya ahadi aliyoivunja. Kuna aina mbili za ahadi; ahadi kuu na ahadi za kawaida.



Ahadi kuu ni ile iliyoichukua kila nafsi ya binaaadamu kuwa itamuabudu Allah (s.w) peke yake bila ya kumshirikisha na chochote. Rejea Qur-an (7:172-173). Waumini kila mara wanaikariri ahadi hii katika shahada na katika kila swala, hasa pale wanaposoma suratul-Faatiha na kuahidi "Wewe tu ndiye tunayekuabudu na Wewe tu ndiye tunayekuomba msaada". (1:5)



Ahadi za kawaida ni zile tunazoahidiana na binaadamu wenzetu katika kutekeleza mambo ya kheri. Ahadi za kufanya mambo maovu ni batili na hatuna budi kuzivunja pale tunapotanabahi.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 266


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kumuamini mwenyezi Mungu..
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah
Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio. Soma Zaidi...

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu. Soma Zaidi...

Elimu yenye manufaa
Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa) Soma Zaidi...

Maamrisho ya kushikamana nayo
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s. Soma Zaidi...

(c)Vipawa vya Mwanaadamu
Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine. Soma Zaidi...

โ€œAllah (s.w) humwingiza katika rahma zake amtakaye na kumwacha kupotea amtakayeโ€
Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini kutokana na vipawa alivyooewa na Allah
Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo Soma Zaidi...

ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽู†ูŽู‘ ุฑูŽุณููˆู„ูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ู…ูŽู†ู’ ูƒูŽุงู†ูŽ ูŠูุคู’ู…ูู†ู ุจูุงูŽู„ู„ูŽู‘ู‡ู ูˆูŽุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ู... Soma Zaidi...

Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI
โ€œKatika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s. Soma Zaidi...