picha

Zijue sababu za kupoteza fahamu.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.

Sababu za kupoteza fahamu.

1. Kupata mshutuko.

Kupata mshutuko ni sababu mojawapo ya kumfanya mtu kupoteza fahamu, vitu kama vile habari mbaya ya kuondokewa na mpendwa yeyote katika jamii, magonjwa mbalimbali nayo usababisha mshutuko,kuona vitu vya kutisha, mawazo nayo usababisha mshutuko na kutoelewana katika familia na mambo mengine kama hayo uweza kumfanya mtu ashutuke na kupoteza fahamu.

 

2. Kupigwa na kitu kichwani.

Kupigwa na kitu kichwani usababisha kupoteza fahamu kwa sababu kwenye kichwa Kuna ogani ya muhimu ambayo ni ubongo, ubongo ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo ubongo ukishutuliwa tu mtu upoteza fahamu kwa hiyo tunapaswa kumpatia mgonjwa aliyepoteza fahamu mda wa kupumzika Ili ubongo uweze kutulia na kufanya kazi yake kama kawaida.

 

3. Mshutuko wa Moyo.

Pia mshutuko wa Moyo usababisha mtu kupoteza fahamu kwa sababu tunajua kuwa kazi kuu ya moyo ni kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa hiyo na kazi ya damu ni kubwa mno kwenye mwili, kwa hiyo basi moyo ukishutuliwa tu  mfumo ushindwa kufanya kazi yake kwa Kawaida na mtu upoteza fahamu, hali hii uweza kurudisha kwa kuamsha moyo ulioshutuluwa na mgonjwa urudia hali yake ya kawaida.

 

4. Kula au kulishwa sumu.

Kula au kulishwa sumu ni mojawapo ya sababu ya kupoteza fahamu kwa sababu sumu inapoingia kwenye mfumo wa damu ufanya damu yote kuwa sumu na kazi yake ya  kawaida ushindwa kufanyika vizuri na baadae mtu upoteza fahamu na hali hii inaweza kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu na pengine watu utumia Tiba asili kupunguza sumu kwenye mwili kama vile kumpatia mgonjwa mkojo na Tiba mbalimbali za asili na mgonjwa anaweza kupona.

 

5. Kiwango Cha sukari kushuka.

Kiwango Cha sukari kikishuka usababisha mgonjwa kupoteza fahamu kwa sababu tunajua kabisa kazi ya sukari mwilini ni kuongeza nguvu, kwa hiyo mwili ukiishiwa nguvu kila mfumo kwenye mwili uhishiwa nguvu hatimaye mtu hupoteza fahamu.kwa hiyo tatizo hili linaweza kutibiwa kwa kumpatia mgonjwa vyakula vyenye sukari kama vile soda, chai au kama mgonjwa Yuko hospitalin anaweza kupewa maji yanayoongeza sukari mwilini.

 

6. Kutumia kiasi kikubwa Cha Pombe au madawa ya kulevya.

Watumiaji wa madawa ya kulevya na Pombe uadhiri kiwango Cha kazi ya Neva system kwa kutumia vitu hivi kwa mda mrefu kwa hiyo na wakati mwingine Pombe umaliza kiwango Cha sukari mwilni na baadae mtu hupoteza fahamu kwa sababu wengine wanatumia Pombe na madawa ya kulevya bila chakula hatimaye wanapoteza fahamu, hao tunaweza kuwasaidia kwa kuwashauri na kubadilisha mtindo wa maisha Ili kuepusha madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwenye maisha yao

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/12/25/Saturday - 06:03:36 pm Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 3567

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Umuhimu wa asidi iliyokwenye tumbo( kwa kitaalamu huitwa HCL)

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix.

Soma Zaidi...
Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo

Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k

Soma Zaidi...
Zijue dalili za upungufu wa maji mwilini

Posti hii inaelezea kuhusiana na upungufu wa maji mwilini

Soma Zaidi...
Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI

Somo hili linakwenda kukuletea Mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI

Soma Zaidi...
Vipi utaepuka maumivu ya kichwa ya mara kwa mara?

maumivu ya kichwa ni moja ya dalili za kiafya ambazo huashiria hali isiyo ya kawaida. hata hivyo maumivu ya kichwa yanaweza kutokea hata kama sio mgonjwa. Hapa nitakuletea sababu zinazopelekea kuumwa na kichwa mara kwa mara.Maumivu

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda

Soma Zaidi...
Nna swali mimi nimefanya Romance na mtu ambaye sijampima kbsa sasa naogopa anaeza kuwa mgonjwa na mm nkaupata

Muulizaji anauliza he kula denda, ama kumbusu ama kufanya romance na muathirika was HIV na wewe uta ambukizwa?

Soma Zaidi...
Faida za chanjo

Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...