Zijue sababu za kupoteza fahamu.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.
Sababu za kupoteza fahamu.
1. Kupata mshutuko.
Kupata mshutuko ni sababu mojawapo ya kumfanya mtu kupoteza fahamu, vitu kama vile habari mbaya ya kuondokewa na mpendwa yeyote katika jamii, magonjwa mbalimbali nayo usababisha mshutuko,kuona vitu vya kutisha, mawazo nayo usababisha mshutuko na kutoelewana katika familia na mambo mengine kama hayo uweza kumfanya mtu ashutuke na kupoteza fahamu.
2. Kupigwa na kitu kichwani.
Kupigwa na kitu kichwani usababisha kupoteza fahamu kwa sababu kwenye kichwa Kuna ogani ya muhimu ambayo ni ubongo, ubongo ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo ubongo ukishutuliwa tu mtu upoteza fahamu kwa hiyo tunapaswa kumpatia mgonjwa aliyepoteza fahamu mda wa kupumzika Ili ubongo uweze kutulia na kufanya kazi yake kama kawaida.
3. Mshutuko wa Moyo.
Pia mshutuko wa Moyo usababisha mtu kupoteza fahamu kwa sababu tunajua kuwa kazi kuu ya moyo ni kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa hiyo na kazi ya damu ni kubwa mno kwenye mwili, kwa hiyo basi moyo ukishutuliwa tu mfumo ushindwa kufanya kazi yake kwa Kawaida na mtu upoteza fahamu, hali hii uweza kurudisha kwa kuamsha moyo ulioshutuluwa na mgonjwa urudia hali yake ya kawaida.
4. Kula au kulishwa sumu.
Kula au kulishwa sumu ni mojawapo ya sababu ya kupoteza fahamu kwa sababu sumu inapoingia kwenye mfumo wa damu ufanya damu yote kuwa sumu na kazi yake ya kawaida ushindwa kufanyika vizuri na baadae mtu upoteza fahamu na hali hii inaweza kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu na pengine watu utumia Tiba asili kupunguza sumu kwenye mwili kama vile kumpatia mgonjwa mkojo na Tiba mbalimbali za asili na mgonjwa anaweza kupona.
5. Kiwango Cha sukari kushuka.
Kiwango Cha sukari kikishuka usababisha mgonjwa kupoteza fahamu kwa sababu tunajua kabisa kazi ya sukari mwilini ni kuongeza nguvu, kwa hiyo mwili ukiishiwa nguvu kila mfumo kwenye mwili uhishiwa nguvu hatimaye mtu hupoteza fahamu.kwa hiyo tatizo hili linaweza kutibiwa kwa kumpatia mgonjwa vyakula vyenye sukari kama vile soda, chai au kama mgonjwa Yuko hospitalin anaweza kupewa maji yanayoongeza sukari mwilini.
6. Kutumia kiasi kikubwa Cha Pombe au madawa ya kulevya.
Watumiaji wa madawa ya kulevya na Pombe uadhiri kiwango Cha kazi ya Neva system kwa kutumia vitu hivi kwa mda mrefu kwa hiyo na wakati mwingine Pombe umaliza kiwango Cha sukari mwilni na baadae mtu hupoteza fahamu kwa sababu wengine wanatumia Pombe na madawa ya kulevya bila chakula hatimaye wanapoteza fahamu, hao tunaweza kuwasaidia kwa kuwashauri na kubadilisha mtindo wa maisha Ili kuepusha madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwenye maisha yao
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Mkojo wa kawaida
Posti hii inahusu zaidi mkojo wa kawaida kwa kila mwanadamu na unavyopaswakuwa, mkojo wa kawaida kwa binadamu huwa na sifa zifuatazo.
Soma Zaidi...Vipi kuhusu kibofu kukaza sana na unapokula unahisi kama tumbo kujaa zaidi je hii nidall yamimba?
Dalili za mimba zinaweza kuwa tata sana kuzijua mpaka upate vipimo. Kwa mfano unaweza kupatwa na maumivu yakibofu. Je unadhani nayo ni dalili ya mimba?
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPANDWA NA PRESHA
Presha ya kupanda hutokea pale kipimo kinaposoma zaidi ya 120/80mm Hg.
Soma Zaidi...Mambo yanayoathiri Uponyaji was jeraha.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kuadhiri Uponyaji wa jeraha.jeraha huleta maumivu makali sana, vilevile Uvimbe, kutoa usaha. Pia jeraha hutofautiana katika kupona kwa mtu mzima na Mtoto.
Soma Zaidi...Namna ya kumhudumia mtu aliyeingongwa na nyoka
Posti hii inahusu njia na namna ya kumhudumia aliyeingiwa na nyoka. Nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na mtu akifinywa na nyoka asipohudumiwa anaweza kupata ulemavu au kupoteza maisha
Soma Zaidi...