picha

Zijue sababu za kupoteza fahamu.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.

Sababu za kupoteza fahamu.

1. Kupata mshutuko.

Kupata mshutuko ni sababu mojawapo ya kumfanya mtu kupoteza fahamu, vitu kama vile habari mbaya ya kuondokewa na mpendwa yeyote katika jamii, magonjwa mbalimbali nayo usababisha mshutuko,kuona vitu vya kutisha, mawazo nayo usababisha mshutuko na kutoelewana katika familia na mambo mengine kama hayo uweza kumfanya mtu ashutuke na kupoteza fahamu.

 

2. Kupigwa na kitu kichwani.

Kupigwa na kitu kichwani usababisha kupoteza fahamu kwa sababu kwenye kichwa Kuna ogani ya muhimu ambayo ni ubongo, ubongo ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo ubongo ukishutuliwa tu mtu upoteza fahamu kwa hiyo tunapaswa kumpatia mgonjwa aliyepoteza fahamu mda wa kupumzika Ili ubongo uweze kutulia na kufanya kazi yake kama kawaida.

 

3. Mshutuko wa Moyo.

Pia mshutuko wa Moyo usababisha mtu kupoteza fahamu kwa sababu tunajua kuwa kazi kuu ya moyo ni kusukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili kwa hiyo na kazi ya damu ni kubwa mno kwenye mwili, kwa hiyo basi moyo ukishutuliwa tu  mfumo ushindwa kufanya kazi yake kwa Kawaida na mtu upoteza fahamu, hali hii uweza kurudisha kwa kuamsha moyo ulioshutuluwa na mgonjwa urudia hali yake ya kawaida.

 

4. Kula au kulishwa sumu.

Kula au kulishwa sumu ni mojawapo ya sababu ya kupoteza fahamu kwa sababu sumu inapoingia kwenye mfumo wa damu ufanya damu yote kuwa sumu na kazi yake ya  kawaida ushindwa kufanyika vizuri na baadae mtu upoteza fahamu na hali hii inaweza kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu na pengine watu utumia Tiba asili kupunguza sumu kwenye mwili kama vile kumpatia mgonjwa mkojo na Tiba mbalimbali za asili na mgonjwa anaweza kupona.

 

5. Kiwango Cha sukari kushuka.

Kiwango Cha sukari kikishuka usababisha mgonjwa kupoteza fahamu kwa sababu tunajua kabisa kazi ya sukari mwilini ni kuongeza nguvu, kwa hiyo mwili ukiishiwa nguvu kila mfumo kwenye mwili uhishiwa nguvu hatimaye mtu hupoteza fahamu.kwa hiyo tatizo hili linaweza kutibiwa kwa kumpatia mgonjwa vyakula vyenye sukari kama vile soda, chai au kama mgonjwa Yuko hospitalin anaweza kupewa maji yanayoongeza sukari mwilini.

 

6. Kutumia kiasi kikubwa Cha Pombe au madawa ya kulevya.

Watumiaji wa madawa ya kulevya na Pombe uadhiri kiwango Cha kazi ya Neva system kwa kutumia vitu hivi kwa mda mrefu kwa hiyo na wakati mwingine Pombe umaliza kiwango Cha sukari mwilni na baadae mtu hupoteza fahamu kwa sababu wengine wanatumia Pombe na madawa ya kulevya bila chakula hatimaye wanapoteza fahamu, hao tunaweza kuwasaidia kwa kuwashauri na kubadilisha mtindo wa maisha Ili kuepusha madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwenye maisha yao

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 3961

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa wajawazito na wanaonyonyesha

Post hii inahusu umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama wajawazito na wanaonyonyesha. Ni hatua ya kupima Mama akiwa mjamzito na wakati wa kunyonyesha ili kuepuka hatari ya kumwambikiza mtoto

Soma Zaidi...
Madhara ya kuchelewa kutibu tatizo la kiafya

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa mwenye uchafu kwenye sikio.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio.

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia, hii ni chanjo inayozuia hasa hasa Magonjwa ya mfumo wa hewa kwa hiyo nayo upewa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Soma Zaidi...
Namna ya kusaidia vijana wakati wa kubarehe

Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia vijana wakati wa kubarehe, ni njia za kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa na mwelekeo ,

Soma Zaidi...
Namna ya kumhudumia mtu aliyeingongwa na nyoka

Posti hii inahusu njia na namna ya kumhudumia aliyeingiwa na nyoka. Nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na mtu akifinywa na nyoka asipohudumiwa anaweza kupata ulemavu au kupoteza maisha

Soma Zaidi...