picha

Namna ya kutunza nywele za mgonjwa

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza nywele za mgonjwa hasa kwa wagonjwa mahututi na wale wasiojiweza tunafanya hivyo ili tuweze kuwatoa kwenye hali ya usafi.

Namna ya kutunza nywele za mgonjwa ambaye hajiwezi.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mara nyingi tunakuwa na wagonjwa majumbani kwetu na tunashindwa kuwahudumia kwa sababu ya kutojua au pengine tunashindwa tuwahudumie namna gani kwa hiyo na nywele za mgonjwa zinapaswa kusafishwa kwa njia zifuatazo.

 

2.Kwanza kabisa unapaswa kumwambia mgonjwa nia na lengo la kumfanyia usafi kama mgonjwa anaweza kusikia na pia hakikisha kuwa hakuna Watu ambao hawahusiki ili mgonjwa aweze kujisikia huru  unaweza kuwa na msaidizi wako.

 

3.Ondoa nguo kwenye sehemu ya kichwa na weka nguo za kumwoshea Mgonjwa inaweza kuwa kanga au kitambaa chochote ambacho ukitoa unaweza kukiosha tena na weka mpira ili maji yasidondoke kwenye godoro na Mashuka mengine.

 

4.Msaidie mgonjwa aweze kusogeza kichwa chake juu ya kitanda ili kuweza kuwa karibu na beseni na hakikisha kichwa kipo kwenye beseni na wakati wa kumwosha nywele tumia maji ya moto .

 

5 Chukua maji kutoka kwenye beseni na mwekee mgonjwa na mwekee kwenye kichwa cha Mgonjwa na weka sabuni safisha nywele za mgonjwa na hakikisha kuwa zimetakata na pia chukua taulo safi upanguse nywele za mgonjwa na safisha sehemu ambapo mgonjwa alikuwepo na hakikisha mgonjwa nywele zake zimekuwa safi.

 

6.Mpake mafuta mgonjwa kwenye nywele zake na kama kuna mba unaweza kuweka dawa ili kuepuka hali ya kujikuna kama inawezekana unaweza kumsuka kama ni mwanamke.

 

7.Kwa hiyo baada ya kujua haya tuwafanyie usafi wa nywele wagonjwa na mtaweza kuona mabadiliko kwa sababu pengine hali ya mgonjwa uendelea kubwa mbaya kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kwa kumfanyia mgonjwa usafi anaweza kupata nafuu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1840

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Matokeo ya maumivu makali.

Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maumivu makali , kuna wakati mwingine mgonjwa anapata maumivu makali ya viungo na dawa mbalimbali uweza kutolewa kwa mgonjwa huyo lakini matokeo yake huwa ni kuendelea kwa maumivu kwa hiyo yafuatayo ni matokeo ya maumivu

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Soma Zaidi...
Namna ya kutumia vidonge vya ARV

Post hii inahusu zaidi matumizi ya vidonge vya ARV, ni vidonge vinavyotumiwa na wagonjwa waliopata ugonjwa wa Ukimwi

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu kizunguzungu

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kizungu Zungu ni tatizo ambalo utokea kwa watu mbalimbali na kwa sababu tofauti tofauti na pengine mtu akipata kizungu sehemu mbaya anaweza kusababisha majeraha au pengine kupata ulemavu

Soma Zaidi...
Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu

Soma Zaidi...
Namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Soma Zaidi...