Aina za vidonda
Posti hii inahusu zaidi Aina mbalimbali za vidonda kwenye mwili wa binadamu, ni vidonda ambavyo utokea kwenye mwili wa binadamu kwa Aina tofauti.
Aina za vidonda
1. Kuna vidonda visafi ambapo kwa kitaalamu huitwa (clean wound ) hii ni Aina ya vidonda ambavyo having wadudu au bakteria kwa kitaalamu hawa wadudu huitwa pathogens organism.tiba ya vidonda hivi ni kusafisha kila mara na Tabia ya vidonda hivi upona haraka sana kuliko Aina yoyote Ile ya vidonda, kwa hiyo watu wenye vidonda vya Aina hii hawapati sana shida katika kupona kwa sababu ya uharaka wa vidonda hivi kupona.
2.Aina nyingine ya vidonda ni vidonda vile ambavyo vina wadudu au bakteria vidonda hivi vidonda mara nyingi upatikana kwenye ajali, watu ambao Upata ajali huwa na vidonda vya Aina hii, vidonda hivi vikitumiwa kwa mda mwafaka upona haraka Ila visipotibiwa kwa mda mwafaka kwa Sababu ya uchafu unaokuwemo kwenye vidonda wadudu uongezeka kwa kiasi kikubwa na hatimaye kidonda uchukua mda mrefu kupona. Kwa hiyo hivi vidonda inabidi vipelekwe hospitalini haraka Ili kuweza kuzuia madhara makubwa yanayoweza kujitokeza kwa sababu ya kuongezeka kwa wadudu kwenye kidonda.
3. Vidonda ambavyo vina kiasi kikubwa Cha wadudu na uchafu vinakuwa mwingi sana, hii ni Aina ya kidonda ambayo unakuta seli pamoja na tisu vyote vimearibika kwenye sehemu ya kidonda.
Aina hii ya vidonda huitaji uangalifu sana kwa sababu ya hali yake na pia vinapaswa kutibiwa hospitalini kwa mda na mgonjwa anapaswa kupatiwa dawa za kutosha Ili kuponyesha Aina hii ya vidonda.
Aina hii ya vidonda usababisha na ajali au pengine na upungufu wa a kinga mwilini ambao usababisha seli kufa na tisu pia kufa wakati mwingine hivi vidonda vinaweza kuitwa vidonda ndugu kwa hiyo uchukua mda mwingi kupona.
Kwa wagojwa wa Mama hii kwanza wanatakiwa kuhojiwa kujua chanzo Cha kidonda na kwa wale wanaowahudumia wagonjwa wa namna hii wanapaswa kuwa makini iili kuepuka maambukizi ya Moja kwa Moja au ya baadae kwa sababu ya hali ya kidonda, kwa hiyo tunapaswa kuelimisha jamii kuhusu kuwepo kwa vidonda na pia kujua kuwa ni ugonjwa wa kawaida na unaweza kutibika. Na jamii zile ambazo wanaendelea kutibu vidonda hivi nyumbani waache maana vidonda vingine ni vikubwa na vinahitaji uangalizi zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 ai web app π5 Kitabu cha Afya π6 web hosting
Post zinazofanana:
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGβATWA NA NYOKA
Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.
Soma Zaidi...Ijue rangi za mkojo na maana zake katika mwili kuhsu afya yako
Posti hii inahusu zaidi rangi za mkojo na maana zake, hizi ni rangi ambazo uweza kutokea kwenye mkojo wa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa, chakula,na mtindo wa maisha inawezekana unywaji wa maji au kutokunywa maji.
Soma Zaidi...Utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyeaha
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyesha
Soma Zaidi...Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI
Somo hili linakwenda kukuletea mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI
Soma Zaidi...Njia za kupunguza uzito na kitambi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa pamoja na kitambi
Soma Zaidi...Njia za kushusha presha
Post hii inakwenda kukujulisha njia za kushusha presha iliyopanda.
Soma Zaidi...