Namna ugonjwa wa herpes simplex unavyosambaa.

Posti hii inahusu zaidi namna ya ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Namna ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

1.Ugonjwa huu wa herpes simplex unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana pasipokutumia kondomu kwa hiyo wakati wa kujamiiana ni lazima kutumia kinga ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu ambao hauna tiba.

 

2.vile vile ugonjwa huu unaweza kusambaa kwa kupigana busu kwa wapenzi na wale wenye utamaduni wa kufanya hivyo, kwa hiyo tunapaswa kuwa makini katika kupigana busu kwa kuangalia kwanza kama kuna dalili na wagonjwa wanapaswa kuwa wazi kama wana ugonjwa huu.

 

3.Pia Ugonjwa huu unasambaa kwa kutumia vifaa ambavyo vimetumiwa na mtu mwenye Ugonjwa huu ikiwa virus wamebaki kwa hiyo tunapaswa kuosha vizuri vyombo vyetu kama tunafikiria au tunajua kuna mtu ana matatizo hayo na ametumia vyombo hivyo, kwa hiyo hatupaswi kuwatenga wagonjwa wenye matatizo ya aina hii ila tuwahudumie na kuwa makini.

 

4.Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua kwa hiyo mama anapaswa kujifungulia hospitalini ili kuepuka Maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto na pia akina Mama wakati wa ujauzito wanapaswa kupima afya zao ili kuepukana kuwaambukiza watoto wao.

 

5.Baada ya kujua njia zinazotumika kuambukiza ugonjwa huu ni lazima kubwa makini na kujikinga ili kuepuka kusambaza ugonjwa huu kwa sababu unasababishwa na virusi kwa hiyo kupona kwake na majaliwa ya Mwenyezi Mungu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1253

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa Pumu, dalili zake na njia za kujilinda dhidi ya Pumu.

Pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu kitaalamu huitwa bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na michubuko sugu mwilini kwenye mirija yake ya kupitisha hewa. Hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija

Soma Zaidi...
Njia za kujikinga na UTI

Somo hili linakwenda kukuletea njia za kujikinga na UTI

Soma Zaidi...
Njia za kutumia Ili kuepuka tatizo la kupungua kwa damu

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa tatizo na kuishiwa damu, kuishiwa damu ni tatizo linolowakumba watu wengi na kusababisha matatizo mengi

Soma Zaidi...
Ajali ya jicho

Post hii inahusu zaidi ajali ya jicho na visababishi vyake, ajali ya jicho ni pale jicho linavyoingiliwa na uchafu na vitu vingine ambavyo havistahili kuwa kwenye jicho

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu kazi za ini.

Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa wajawazito na wanaonyonyesha

Post hii inahusu umuhimu wa kupima virus vya ukimwi kwa mama wajawazito na wanaonyonyesha. Ni hatua ya kupima Mama akiwa mjamzito na wakati wa kunyonyesha ili kuepuka hatari ya kumwambikiza mtoto

Soma Zaidi...
Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.

Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.

Soma Zaidi...
Choo kisichokuwa cha kawaida

Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Upungufu wa damu mwilini

Post inaenda kuzungumzia kuhusiana na upungufu wa damu mwilini ambapo tutaona SABABU na dalili zake lakin upungufu wa damu mwilini hujulikana Kama ANEMIA.

Soma Zaidi...
Matokeo ya maambukizi kwenye milija na ovari

Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maambukizi kwenye milija na ovari, ni matokeo apatayo mtu mwenye maambukizi kwenye milija na ovari.

Soma Zaidi...