picha

Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake

Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo

Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake

KUHARIBIKA KWA UJAUZITO



Kitendo cha kuharibika kwa ujauzito kitaalamu hutambulika kama spontaneous abortion. Ni kutoka kwa ujauzito ndani ya wiki 20 za mwanzo. Tafiti zinaonesha kuwa yapata asilimilia 50 ya mimba hutoka yaani nusu ya mimba zinazotugwa hutoka. Wengiwao hupatwa tu na ha;I ya kukosa siku zao bila ya kujuwa kama walikuwa na ujauzito na wengine wanajigundua. Pia tafiti zinaonyesha kuwa yapata asilimia 15 mpaka 25 ya mimba ambazo zimejulikana hutoka. Hata hivyo mimba nyingine hutoka siki chache tu baada ya kuingia. Sasa ni kwa nini mimba hutoka? Makala hii inakwenda kukupa elimu juu ya kutoka kwa mimba, dalili zake na sababu zake.


Dalili za kutoka kwa ujauzito
1.Kutokwa na damu ambayo inawza kuongezeka kadiri muda unavyoenda.
2.Maumivu ya tumbo
3.Kupata uchovu
4.Maumivu makali ya mgongo
5.Kupatwa na homa iliyochanganyikana na moja ya dalili zilizotajwa hapo juu.


6.Sababu za kutoka ujauzitoMaumivu ya chango kupitiliza

Mimba nyingi hutoka kwa sababu kuna matatizo kwenye genetics za mtoto na si kosa la mama ama la baba. Hii ni kutokana na maumbile ya mtoto kuwa na shida katika ufanyikaji. Sababu nyingine za kutokwa na ujauzito ni:-
1.Maambukizi, watu waishio na baadhi ya maambukizi kama PID ama HIV wanaweza kuwa hatarini.
2.Kuwa na maradhi kama kisukari ama maradhi katika tezi ya thyroid
3.Matatizo katika homoni
4.Mfumo wa kinga kuondoa mimba
5.Shughuli na maumbile ya mama
6.Mfuko wa mimba kuwa na matatizo


Pia mwanamke anaweza kuwa na nafasi kubwa ya kutokwa na ujauzito kama:-
1-Atakuwa na umri wa zaidi ya miaka 35
2-Ana maradhi kama kisukari au maradhi ya tezi ya thyroid
3-Kama ana kawaida ya kutokwa na ujauzito zaidi ya mara tatu.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2419

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.

Soma Zaidi...
Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri

Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba

Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.

Soma Zaidi...
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Soma Zaidi...