Kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi
Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi, tunajua kabisa wakati wa hedhi damu inapaswa kuwa nyepesi na ya kawaida ila kuna wakati mwingine inakuwa na mabonge zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.
Sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.
1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba damu wakati wa hedhi inapaswa kuwa ya kawaida na isiwe na aina yoyote ya mabonge lakini kuna wakati unafika ambapo damu wakt wa hedhi inakuja ikiwa nzito na yenye mabonge mabonge mengi, hali hii usababishwa na mambo yafuatayo .
2. Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Kwenye via kama kuna Maambukizi hali hii utokea Maambukizi ha ya magonjwa ya ngono kama vile kaswende, kisonono na mengine kama hayo, na si Magonjwa ya ngono tu kuna maambukizi kwenye mlango wa kizazi nao pia usababisha damu kuja ikiwa nzito kwa hiyo kama hali hiyo ikitokea ni lazima kwenda kwenye vipimo ili kuangalia shida ni ipi na kutibiwa mara moja
3.Kuwepo kwa uvimbe kwenye mfuko wa uzazi na kwenye ovari, kama kuna uvimbe wowote uweza kusababisha mabonge mabonge ya damu wakati wa hedhi kwa hiyo ni lazima kufanya vipimo vya kwenye mfumo wa uzazi na kwenye ovary ili kuweza kutambua tatizo lililopo kwa Mama au dada yeyote mwenye tatizo kama hili
4.mabadiliko ya homoni.
Pengine utokea kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni ambazo zinahusika na kupandisha yai kutoka kwenye ovari, kuandaa mfuko wa uzazi, na kuaribu mfuko wa uzazi kama hakuna mimba katika hatua zote hizi kama kuna shida yoyote kwenye homoni na damu utoka kama mabonge mabonge na hali hii utokea mara chache inaweza kuwa kama miezi miwili na baadae uacha ila kama ni Maambukizi uendelea.
5.Kwa hiyo hali hii ikitokea mara kwa mara ni lazima kuchukua hatua za haraka ili kama ni Maambukizi yatibiwe mara moja ili kuzuia matatizo mengine kama vile utasa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 ai web app 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Wanaopasawa kutumia PEP
PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.
Soma Zaidi...Je endapo mama atafanya tendo la ndoa wiki moja kabla ya kuingia hedhi anaweza kupata ujauzito?
Zipo siku maalumu ambazo mwanamke hupata mimba. Siku hizi huzoeleka kwa jina la siku hatari. Je ungependa kufahamu mengi kuhusu siku hatari, endelea na makala hii.
Soma Zaidi...Uchunguzi wa Nimonia kwa mtoto na Tiba
Posti hii inahusu namna unavyoweza kumtambua mtoto mwenye Ugonjwa wa Nimonia na tiba anayopaswa kupata mtoto mwenye Nimonia
Soma Zaidi...Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kisukari wakati wa ujauzito.
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.
Soma Zaidi...Namna ya kumpima mtoto uzito
Posti hii inahusu namna ya kumpima mtoto uzito, ni njia ambayo utumika kujua uzito wake na maendeleo ya mtoto.
Soma Zaidi...