CHANGAMOTO ZA UJAUZITO


image


Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu


CHANGAMOTO ZA UAJAUZITO NA DALILI ZENYE KUENDELEA:

Ni vyema sana kutambuwa hili, kwani itakusaidia katika klujuwa changamioto za ujauzito. Katika dalili hizi za ujauzito zipo ambazo nio zenye kuendelea. Na katika kuendelea hko wengi katika wajawazito wanapatwa na changamoto kadhaa. Hapa nitakueleza nini cha kufanya.

 

1.KichefuchefuKichefuchefu kinaweza huweza kuchelewa kujitokeza lakioni kinaweza kuwa ni chenye kuendelea. Kwa baadhi ya wanawake kinaweza kwenda mpka miezi kadhaa mbele, ila kwa wengi kinaweza kukata kufikia wiki ya 28. Hii ni changamoto kwakweli kwa wajawazito. Maana kichefuchefu kinaweza lumkoseshea amani wakati mwingine.hali ya kutema mate, kuhisi kutapika ama kichefuchefu kwa ujumla huwasumbua wajawazito. Wataalamu wanaeleza kuwa hasa chanzo cha kichefuchefu ni mabadiliko ya homoni mwilini. Na huwenda pia kuna sababu nyingine.

 

Kama utakuwa unasumbuliwa na hali hii fanya hivi. Epuka kukaa maeneo yenye joto sana. Epuka kunywa maji wakati unakula. Tumia tangawizi, kwenye chai ama tafuna. Unaweza kuiweka kama unga ama vipande vidogovidogo. Unaweza kutumia bigjii maalumu kwa ajili ya wajawazito.

 

2.Maumivu ya tumbo:Kwa wajawazito maumivu ya tumbo mara kwa mara ni hali ya kawaida na yenye kuendelea. Maumivu haya yanaweza kuchukuwa muda mchache na kuondoka. Pia ni yenye kuvumilika yaani mwanamke anaweza kuendelea kufanya shughuli zake. Ila endapo yatakuwa ni makali sana kutovumilika inaweza kuashiria kuna shida kwenye afya ya mwanamke huyu. Ni vyema kufika kituo cha afya kupata ufafanuzi wa hali.

 

Katika hali ya maumiovu haya ya tumbo mwanamke anaweza kutumia dawa za kupunguza maumivu. Pia zipo tiba mbadala kupunguza maumivu. Ila mwanamke awe makini sana maana anaweza kuingia katika hatari endapo atatumia dawa kiholela.

 

3.Kutokwa na damu:Kama ilivyo dalili nyingine huendelea basi si jambo ;la kushangaza kwa mwanamke mjamzito kujikuta nguo yake ya ndani kuwa na vitone vya damu. Damu hii si yenye kuchuruzika ama yenye kutoka kwa wingi kama damu ya hedhi. Endapo mjamzito atakuwa anatokwa na damu nyingi eidha iambatane na maumivu makali ya tumbo ama isiambatane ni vyema awahi kituo cha afya kupata uthibitisho juu ya mabadiliko hayo. Maana wakati mwingimne damu inaweza kuashiria shida katika ujauzito.

 

4.Mabadiliko katika hisia, matakwa na matamanio katika vyakula na vitu vingine.Haswa mwanamke anaweza kujishangaa mwenyewe inakuweje hali hii. Mwanamke anaweza kuona kuwa nachukia vitui ama kuna watu anawachukia ghafla. Wakati huo huo anaweza kupenda mtu flani sana. Pia kuna wakati atakuwa anachukia baadhi ya vyakula na vitu vingine. Yaani kwa ufupi ni mabadiliko tu katika saikolojia yake. Huu si ugonjwa hivyo hali hii isimpe mawazo saana mwanamke. Watu walio karibu na wajawazito wawe makini pia maana wanaweza kufanya makosa makubwa kama kumpiga na vinginevyo.

 

5.Kuvimba ama kujaa kwa uso na miguu.Yes hii ni changamoto kwa kweli. Hii haiwapati wenye mimba ya miezi ya mwanzo, hali hii hutokea wakati mimba imesha komaa miezi ya mbeleni. Kuvimba ama kujaa kwa uso na miguu kwa wajawazito sio jambao la ajabu. Hali huweza kukaa sawa atakapojifungua. Kama mwanamke anasumbuliwa na hali hii, ahakikishe anapumzika katika maeneo yenye utulivu na yaliyopa yaani aepuke kukaa maeneo yenye joto. Pia aepuke kubvaa nguo za kabana. Aepuke kukaa chini katika mkao mmoja kwa muda mrefu.

 

6.Kuenda haja ndogo mara kwa mara.Hii ji changanmoto hasa kwa wale ambao ndio ujauzito wao wa kwanza.Hapa pia kuna wajawazito wanajitahidi kujizuia eti wapunguze kuenda haja ndigo. Hii sio sawa kabisa. Mjamzito anatakiwa anaposikia haja kakaitoe wala asihofu kitu huu si ugonjwa na ni kawaida kabisa. Kwa kuwa moyo wake umeongeza utendaji wa kazi hivyo uchujwaji wa damu ni mkubwa. Kwa maendeleo mema ya afya yake na afya ya ujauzito wake, mjamzito asihofu kitu, aende tu haja.



Sponsored Posts


  πŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       πŸ‘‰    2 Maktaba ya vitabu       πŸ‘‰    3 Hadiythi za alif lela u lela       πŸ‘‰    4 Magonjwa na afya       πŸ‘‰    5 Mafunzo ya php       πŸ‘‰    6 Jifunze fiqh    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?
Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito. Soma Zaidi...

image Madhara ya fangasi ukeni
Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke. Soma Zaidi...

image Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako. Soma Zaidi...

image Njia za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha kwa sababu kuna familia nyingi zinakosa watoto sio kwa sababu ni tasa ila kuna njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Napenda kuuliza mke wangu anamuda wa wiki moja . tumbo na maziwa vinauma je dalili hizo zinawekuwa ni ujauzito...?
Maumivu ya tumbo kwa mjamzito huweza kuanaa kuonekana mwanzoni kabisa mwaujauzito, ndani ya mwezi mmoja. Ikabidi si dalili pekee ya kuwa ni mjamzito. Soma Zaidi...

image Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...

image Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza Soma Zaidi...

image Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea
Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu. Soma Zaidi...

image Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

image Dalili za uvimbe kwenye kizazi
Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi. Soma Zaidi...