Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz

Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito.

1.Kuwapatia wajawazito neti pindi wanapoanza mahudhurio ya kliniki.

Hii ni mojawapo ya njia ambayo inafanya kila mahali nchini ambapo kila mwanamke mwenye mimba akija kuanza mahudhurio ya kliniki anapewa neti ili aweze kulala ndani yake wakati wa usiku na kuzuia mbu wanaoeneza Malaria wasimpate akilala ndani ya neti, kw hiyo akina Mama wale wazembe wa kuhudhuria kliniki mnapaswa kwenda ili kuepukana na Ugonjwa wa Malaria.

 

2.Pia kuna watu wenye mila potofu wakipewa neti badala ya kuitumia wakati wa kulala wanaitumia kufugia kuku na kufunika mazao ili yasiliwe na wadudu kwa hiyo elimu ni ya msingi kwa jamii ili kuepuka vitu vya namna hivyo na wanaofanya mambo kama haya wanapaswa kuchukuliwa na sheria kwa sababu hizi neti ni bajeti ya serikali.

 

3.Na njia nyingine ni kutoa dawa za SP kila mwezi pale ambapo Mama anakuja kwenye mahudhurio ya kliniki. Kila mwezi kwenye vituo vyote akina Mama upewa dawa za SP lengo ni kuzuia wadudu wanasababisha malaria kutofikia mtoto, maana dawa hizi ukaa karibu na plasenta ikitokea mdudu amefika uweza kuuawa na hawezi kupata Malaria, kwa hiyo akina Mama wanaoanza kliniki wakiwa na miezi sita hawapati dawa hizi kwa wakati kwa hiyo wanaweza kuwa katika hatari ya kupata Maambukizi.

 

4.Kuna baadhi ya mila na desturi za watu wakipewa dawa hizo uleta visingizio wakidai watatumia wakiwa njiani eti zinawasumbua na wakienda nyumbani hawatumii wanatumia madawa ya kienyeji hali hii usababisha mama kujifungua mtoto mfu au mimba kutoka, kwa hiyo hakina Mama jaribu kujali maisha yenu na watoto pia nenda kliniki kwa wakati, tumia kila dawa ipasavyo na nakuhakikishia utajifungua salama achana na mila na desturi za zamani maisha yamebadilika kuna magonjwa mengi na vitu vingi kwa hiyo okoa maisha yako na mtoto wako.

 

5.Njia nyingine ni kupima Malaria kwa wajawazito pindi tu wanapoanza mahudhurio ya kliniki, hii inatumika kila sehemu ambapo wanawake wanapoanza kliniki kati ya vipimo vinavyopikwa na Malaria nayo imo kwa kuft hivyo ni kutafuta njia ili kutokomeza ugonjwa huu. Kwa hiyo akina Mama wale wazembe wa kuhudhuria kliniki Malaria ipo na inaweza kumshika mjamzito na kusababisha madhara makubwa kama vile mimba kutoka na kuzaa mtoto mfu, kwa hiyo acha uvivu nenda kliniki

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/02/08/Tuesday - 09:59:27 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 630

Post zifazofanana:-

Hati.a ya kijana mchonganishi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili. Soma Zaidi...

Athari ya kutotibu maambukizi ya kwenye kibofu cha mkojo
Post hii inahusu zaidi athari za kutotibu maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo, nimatazito yanayoweza kutokea iwapo ugonjwa huu hautatibika. Soma Zaidi...

Haki za raia katika dola ya kiislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kazi ya Dawa ya salbutamol
Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma. Soma Zaidi...

Je fangasi ikikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa ina madhara gani?
Je umeshawaho kujiuliza maswali mengi kihusu fangasi?. Huyu hapa ni mmoja katika waulizaji waliopata kuuliza rundo la maswali haya. Soma post hii kuona nini ameuliza Soma Zaidi...

Sunnah za funga ya ramadhan
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ugonjwa wa UTI
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI Soma Zaidi...

Kutoa zakat
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Tahadhari za ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI Soma Zaidi...

Vyanzo vya sumu mwilini.
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa sumu mwilini, kwa sababu kuna wakati mwingine tunapata magonjwa na matatizo mbalimbali ya ki afya tunaangaika huku na huko kumbe sababu kubwa ni kuwepo kwa sumu mwilini na vyanzo vya sumu hiyo ni kama ifuatavy Soma Zaidi...

Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo. Soma Zaidi...