Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz
Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito.
1.Kuwapatia wajawazito neti pindi wanapoanza mahudhurio ya kliniki.
Hii ni mojawapo ya njia ambayo inafanya kila mahali nchini ambapo kila mwanamke mwenye mimba akija kuanza mahudhurio ya kliniki anapewa neti ili aweze kulala ndani yake wakati wa usiku na kuzuia mbu wanaoeneza Malaria wasimpate akilala ndani ya neti, kw hiyo akina Mama wale wazembe wa kuhudhuria kliniki mnapaswa kwenda ili kuepukana na Ugonjwa wa Malaria.
2.Pia kuna watu wenye mila potofu wakipewa neti badala ya kuitumia wakati wa kulala wanaitumia kufugia kuku na kufunika mazao ili yasiliwe na wadudu kwa hiyo elimu ni ya msingi kwa jamii ili kuepuka vitu vya namna hivyo na wanaofanya mambo kama haya wanapaswa kuchukuliwa na sheria kwa sababu hizi neti ni bajeti ya serikali.
3.Na njia nyingine ni kutoa dawa za SP kila mwezi pale ambapo Mama anakuja kwenye mahudhurio ya kliniki. Kila mwezi kwenye vituo vyote akina Mama upewa dawa za SP lengo ni kuzuia wadudu wanasababisha malaria kutofikia mtoto, maana dawa hizi ukaa karibu na plasenta ikitokea mdudu amefika uweza kuuawa na hawezi kupata Malaria, kwa hiyo akina Mama wanaoanza kliniki wakiwa na miezi sita hawapati dawa hizi kwa wakati kwa hiyo wanaweza kuwa katika hatari ya kupata Maambukizi.
4.Kuna baadhi ya mila na desturi za watu wakipewa dawa hizo uleta visingizio wakidai watatumia wakiwa njiani eti zinawasumbua na wakienda nyumbani hawatumii wanatumia madawa ya kienyeji hali hii usababisha mama kujifungua mtoto mfu au mimba kutoka, kwa hiyo hakina Mama jaribu kujali maisha yenu na watoto pia nenda kliniki kwa wakati, tumia kila dawa ipasavyo na nakuhakikishia utajifungua salama achana na mila na desturi za zamani maisha yamebadilika kuna magonjwa mengi na vitu vingi kwa hiyo okoa maisha yako na mtoto wako.
5.Njia nyingine ni kupima Malaria kwa wajawazito pindi tu wanapoanza mahudhurio ya kliniki, hii inatumika kila sehemu ambapo wanawake wanapoanza kliniki kati ya vipimo vinavyopikwa na Malaria nayo imo kwa kuft hivyo ni kutafuta njia ili kutokomeza ugonjwa huu. Kwa hiyo akina Mama wale wazembe wa kuhudhuria kliniki Malaria ipo na inaweza kumshika mjamzito na kusababisha madhara makubwa kama vile mimba kutoka na kuzaa mtoto mfu, kwa hiyo acha uvivu nenda kliniki
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Habari nilitaka kujua kuhusu ugonjwa wa fungusi kwenye uume
Je na wewe unasumbuliwa na fangasi wenye uume. Post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Vyanzo vya kuharibika kwa mimba ya miezi kuanzia 0-3
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Soma Zaidi...Dalili za kasoro ya moyo ya kuzaliwa kwa watu wazima
Ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (kasoro ya moyo ya kuzaliwa) ni hali isiyo ya kawaida katika muundo wa moyo wako unaozaliwa nao. utu uzima. Ingawa maendeleo ya kimatibabu yameboreshwa, watu wazima wengi walio na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa wanaweza wasip
Soma Zaidi...Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Soma Zaidi...Dalili za kuharibika kwa mimba
Katika post hii utajifunza ishara na dalili ninazoonyesha kuwa mimba ipo hatarini kutoka ama inaweza kuwa imeshatoka.
Soma Zaidi...Yajue madhara ya kutoa mimba mara Kwa mara
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale wenye tabia ya kutoa mimba mara Kwa mara .
Soma Zaidi...