Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa akina Mama.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ni huduma ambayo inatolewa kwa jamii ili kuweza kupata idadi ya watoto wanaohitajika na kuwapatia nafasi kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama.
2.Akina mama wanapata afya nzuri na kupumzika kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine.
Ni wazi kabisa mama akiwa na mimba uweza kupata uchovu na masumbuko mbalimbali na kwa wakati mwingine kuna ambao wakati wa mimba wanaweza kuugua na kukosa nguvu mda wote lakini wakijifungua wanakuwa kawaida kwa hiyo na wakati wa kujifungua mama Upata uchungu na kuangaika sana wengine hata kutoa damu nyingi kwa hiyo wakipata mda wa kupumzika kutoka kwa mtoto mmoja kwenda mwingine watakuwa na afya njema kuliko kubeba mimba kila mara na afya udhoofika.
3.Uzazi wa mpango uzuia vifo vya akina Mama ambavyo utokea wakati wa kujifungua.
Ni kweli Mama akina mama wengi wanaweza kuingia kwenye hatari ya kufariki wakati wa kujifungua kwa hiyo kutokana na kuwepo kwa uzazi wa mpango kumefanya kupunguza vifo vya akina Mama kwa sababu ya kujifungua kwa mda kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine kuliko kujifungua karibu kila mwaka na viungo vya mwili vinakuwa bado na hali hiyo usababisha kuvuja damu nyingi au kupasuka wakati wa kujifungua na Mama anaweza kupoteza maisha.
4.Uzazi wa mpango umesaidia akina mama ushiriki kwenye kazi mbalimbali za kiuchumi kwa sababu Mama anakuwa na nguvu za kutosha kuweza kuleta maendeleo kuliko kukaa katika kulea watoto ambao wamefuata na kama mapacha kwa hiyo kutokana na kuwepo kwa uzazi wa mpango akina Mama wengi wameweza kushiriki kazi mbalimbali za kiuchumi.
5.Uzazi wa mpango umefanya akina mama kubwa na idadi ya watoto wanaowapenda na kuwatunza na wameweza kuwa na nafasi kutoka kwa mtoto mmoja kwenda mwingine na pia watoto wenyewe wanaweza kuleana na kusaidiana kwa sababu ya kuwepo kwa nafasi kubwa kutoka kwa mtoto mmoja kwenda mwingine.
6.Kwa hiyo tunaona wazi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa akina Mama kwa hiyo kama jamii tunapaswa kuwahimiza akina mama kushiriki kwenye uzazi wa mpango ili kuweza kupata idadi ya watoto wanaowahitaji na kuepuka kutumia mda mwingi kulea watoto wanaofuatana na kufanya kushuka kwa uchumi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi dalili za mimba inayotaka kutoka yenyewe, Kuna wakati mwingine mama anabeba mimba na mimba hiyo I atishia kutoka na huwa inaonyesha dalili mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni dalili za mimba kutaka kutoka yenyewe.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi malengo kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, ni malengo ambayo yametolewa ili kuweza kusaidia mtoto azaliwe vizuri na mambo mengine kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.
Soma Zaidi...Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo usaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kufunga kizazi kwa wanawake.
Soma Zaidi...Kichefuchefu ni moja katika dalili za mimba za mapema, Lucinda je upo uwezekano kwa mwanamke kuwa na ujauzito bila hata ya kuwa na kichefuchefu?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...