Ni mambo gani yanaharibu na kutengua udhu?

Ni mambo gani yanaharibu na kutengua udhu?

Yanayotengua Udhu



Mtu aliyetawadha hutokwa na udhu wake kwa kupatwa au kutokewa na mojawapo kati ya haya yafuatayo:



1.Kutokwa na kitu chochote kwenye sehemu za siri. Ni pamoja na kwenda haja ndogo au kubwa. Kutokwa na upepo, maji maji yatokayo katika utupu wa mbele kutokana na matamanio au sababu nyinginezo.



2.Kutokwa na fahamu kwa kulala usingizi kwa kuegemea mahali bila ya kumakinisha makalio yake ardhini. Tunajifunza katika hadithi ifu atayo:



Amesimulia Basrah (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) kasema:Kutawadha kuna kuwa lazima kwa mwenye kulala usingizi kitandani, kwa sababu anapolala kitandani maungo yake hulegea ”.(Tirmidh, Abuu Daud).



3.Kushika sehemu za siri kwa viganja vya mikono kama tunavyojifunza katika hadithi ifuatayo:



Amesimulia Basrah (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) kasema: “Mmoja wenu atakapogusa tupu yake, na aende kutaw adha tena ”.(Malik, Ahm ad, Abuu Daud, Tirmidh, Nasai, Ibn Majah)



Haya matatu ndio yanayotengua udhu bila ya khitilafu yoyote kati ya Waislamu.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2912

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maana ya Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya Twahara Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu

Soma Zaidi...
Sanda ya mtoto

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zoezi la nne mada ya fiqh.

Maswali mbalimbali kuhusu fiqh.

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria

Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza malipo ya funga au swaumu

Mambo haya yanaweza kuharibu funga ya mtu ama kupunguza malipo ya funga.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake.

Soma Zaidi...