4.
4.2 Sheria Katika Uislamu
? Maana ya Sheria
Kilugha: njia ya Kufuata
Kimatumizi: ni taratibu, sharti, kanuni na amri zilizowekwa kuongoza jamii.
Kazi ya Sheria katika Jamii
i. Kulinda binaadamu binafsi dhidi ya madhara mbali mbali ya mwenendo wake mbaya.
ii. Kulinda na kuhifadhi maisha ya watu na mali au rasilimali zao kutokana na kuuliwa, kujeruhiwa, kuharibiwa, kuibiwa, n.k bila sababu ya msingi.
iii. Kuhifadhi na kulinda amani na usalama katika jamii kutokana na migongano, vurugu, n.k.
iv. Kuhifadhi na kulinda maadili ya jamii kama njia ya msingi ya kumbakisha mwanaadamu katika mwenendo mema.
v. Kuweka na kupanga utaratibu wa namna ya kuendesha shughuli na maisha ya kila siku kibinafsi na kijamii.
vi. Sheria ya Kiislamu ina kazi ya kulinda na kuhifadhi misingi mitano ya mwanaadamu ambao ni; imani, uhai, akili, heshima na hadhi na mali.
Chimbuko la Sheria za Kitwaghuti
- Zimetungwa na binaadamu kwa kutumia vipawa vya akili, elimu, mila, desturi, uzoefu, mazingira na matashi ya nafsi zao.
- Katiba ndio msingi (chombo) mkuu wa sheria za Kitwaghuti ambayo hugawanya utekelezaji wake katika vyombo vikuu vitatu;
1. Bunge (Legislature) β chombo kikuu cha kutunga sheria
2 Serikali (Executive) β chombo kikuu cha utendaji
3 Mahakama (Judiciary) β chombo kikuu cha kutafsiri sheria na kutoa haki.
Udhaifu wa Sheria za Kitwaghuti
- Pamoja na mwanaadamu kupewa na vipawa vya akili, ujuzi, elimu, n.k bado ana madhaifu mengi kama ifuatayo;
i. Mwanaadamu ana ujuzi wa mambo machache sana juu ya ulimwengu na yale yanayomzunguka.
Rejea Qurβan (17:85)
ii. Mwanaadamu anaathiriwa sana na matashi ya ubinafsi, uchoyo, upendeleo, chuki, n.k.
iii. Binaadamu wametofautiana mno katika fikra, uoni, vipawa, uzoefu
(mazoea).
iv. Mwanaadamu pia anaathiriwa sana na mabadiliko ya kimazingira na zama
(nyakati).
- Kutokana na mapungufu haya, usimamizi na utekelezaji wa sheria za kitwaghuti hufanywa na watu wachache (watawala) kwa ajili ya manufaa yao tu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.
Soma Zaidi...Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.
Soma Zaidi...Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.
Soma Zaidi...Mtume amemfundisha kuwa watoto wafundishwe kuswali wakiwa na miaka saba na waadhibiwe wakiacha wakiwa na miaka 10
Soma Zaidi...