image

Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir

6. Swala ya Idil-Fitri na Idil-Hajj

Iddil-Fitri na Iddil-Hajj ni swala za Sunnah zilizokokotezwa. Iddi hizi mbili zinazofahamika vyema kwa Waislamu kuwa ni vilele vya siku mbili baada ya kukamilisha nguzo ya Funga na Hajj. Kielelezo cha kilele cha sherehe katika Uislamu si ngoma wala tarumbeta, wala si kula na kunywa sana, bali ni kumkumbuka Allah (s.w) na kumtaja kwa wingi.

 


Swala ya Idd inaswaliwa baada ya jua kuchomoza na kabla ya jua kufika katikati. Ina rakaa mbili na khutuba kama swala ya Ijumaa lakini tofauti na Ijumaa, khutuba hufuatia baada ya swala. Kama ilivyo swala ya Ijumaa, swala za Idd mbili ni swala za jamaa. Ni sunnah ku swalia Idd uwanjani ili kukusanya jamaa kubwa zaidi.

 


Swala ya Idd ikiangukia Ijumaa

 


Mtume (s.a.w) ametoa ruhusa ya kutoswali swala ya Ijumaa iwapo itakuwa imeswaliwa swala ya Idd iliyoangukia siku ya Ijumaa kwa mujibu wa Hadithi zifuatazo:-
Zaid bin Arqam (r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) alisw alisha Idd kisha akatoa ruhusa kwa swala ya Ijumaa, akasema: “Anayetaka kuswali na aswali”. (Vitabu Vitano vya Hadith).

 


Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Katika siku yenu hii ya leo zimekutana Idd mbili (yaani Idd na Ijumaa)basi anayetaka asiswali Ijumaa (swala ya Idd inatosheleza) lakini sisi tutaswali Ijumaa”. (Abu Daud).

 


Kutokana na Hadithi hii ya mwisho, hii ni ruhusa tu na ni bora kuswali Iddi na Ijumaa kwani Mtume mwenyewe alifanya hivyo.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 882


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Aina ya talaka zisizo rejewa
2. Soma Zaidi...

Yanayofaa kwa maamuma katika kumfata imamu kwenye swala ya jamaa
Soma Zaidi...

Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu
Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika. Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu
Soma Zaidi...

Twahara
FIQH 1. Soma Zaidi...

Wenye ruhusa za kutofunga ramadhan
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya shahada kama nguzo ya kwanza ya uislamu
4. Soma Zaidi...

Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir Soma Zaidi...

Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq
Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

jamii
Soma Zaidi...

Sanda ya mtoto
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...