image

walioruhusiwa kufungua (kula) mwezi wa ramadhani

walioruhusiwa kufungua (kula) mwezi wa ramadhani


Download kitabu hiki hapa

Walioruhusiwa kufungua mwezi wa ramadhani
Hawa wamegawanyika katika makundi matatu
1.kuna ambao inajuzu kufungua na kufunga
2.Ni wajibu kufungua
3.Haijuzu kwao kufungua.

1.wanaojuziwa kufunga au kufungua
1.mgonjwa. Watu wagonjwa inafaa kwao kufunga au kutofunga. Maradhi yapo katika namna tatu.

A)maradhi hafifu kama mafua ambayo hata hayaathiri funga hata kidogo. Ni haramu futofunga kwa maradhi ya namna hii.

B)Maradhi ambayo sio mkubwa lakini yanaathiri funga, hapa mgonjwa ana hiyari ya kufunga au kutofunga.

C)Maradhi makubwa ambayo mtu akifunga yatapelekea kuzidi kwa ugonjwa na hatimaye kudhoofu afya. Ni haramu kufunga kwa maradhi haya maana Allah amekataza kujiingiza kwenye maangamizo. Amesema Allah: “na msiziue nafsi zenu” (quran 4:29)

2.msafiri: msafiri mwenye kusafiri safari ambayo inajuzu kupunguza swala inafaa kufungua. Na kama aatfunga pia funga yake inafaha. Ama kuhusu kipi kilicho bora kati ya kufunga na kutofungwa, maulamaa wameigawa safari katika makundi yafuatayo:

A)safari ambayo inatia uzito na mashaka kufunga. Hapa ni bora zaidi kutofunga kuliko kufunga. Imepokewa hadithi kutoka kwa Jabir kuwa alikuwa mtume katika safari, akaona kuna watu wapo katika hali flani akauliza wana nini hawa akajibiwa wamefunga na hapo akasema “si katika jambo jema kufunga kwenye safari” (Bukhari). Pia katika safi nyingine watu walipokuwa wapo kwenye jua kali safarini mtume alisema: wameondoka watu waliofungua leo na malipo ” (Muslim)

B)Safari ambayo haina shaka wala taabu katika funga. Hapa maulamaa wamesema katika hali hii kufunga ni bora zaidi, kwa kauli ya Allah: aliposema “na mkifunga ni bora kwenu”(quran 2:184)

C)Ikiwa safari inamashaka makubwa na taabu kiasi kwamba inaweza kusababisha taabu na maangamivu. Hapa kutofunga ni jambo la lazima, yaani ni haramu kwa msafiri kufunga.

Muda wa kufungua.
Maulamaa wamnaeleza kuhusu ni muda gani mtu anatakiwa afungue katika hali zifuatazo:-

1.Kuanza safari kabla ya alfajiri. Hapa inaruhusiwa kufungua muda wowote.

2.Kutia nia ya safari baada ya alfajir. Yaani safari imetokea baada ya kuswali au mchana. Hapa maulamaa wengi wamesema mtu hataruhusiwa kufungua. Ila kwa uchambuzi zaidi uliofanywa juu ya safari za mtume na mapokezi mengi ni kuwa inafaha kufungua muda wowote na hii ndio kauli yenye nguvu.

3.Mtu kutia niya ya kufunga akiwa safarini na baadaye kutia niya ya kufungua. Hapa inajuzu kufungua.

Muda wa kufungua safarini.
Pindi msafiri atakapokusudia kufanya makazi ya kudumu basi hapa ruhusa ya kufungua inakatika. Ila kama hajakusudia kufanya makazi ya kudumu ataendelea kutofunga. Amesimulia Ibn ‘Abas kuwa “…hakuacha Mtume kuendelea kutofunga (kula) mpaka ukakatika mwezi” (Bukhari).

Na pindi akirudi katika makazi yake usiku atafunga siku inayofata. Ama akirudi katikati ya mchana hapa maulamaa wapo walosema atajizuia kula na kunywa. Ila kauli yenye nguvu ni kuwa ataendelea kula kama alivyokuwa safarini. Ila stara ya kula izingatiwe. Ibn Mas’ud amesema kuwa: mwenye kula mwanzoni mwa mchana, basi na aendelee mapaka mwishoni” (Ibn Abi Shayb)

3.wazee (vikongwe).
Wazee sana yaani vikongwe ni ruhusa kwao kutofunga. Ila pia wakitaka wanaweza kufunga. Na kama wakitofunga hawatakiwi kujalipa funga ila watalisha masikini katika kila siku ambayo hawajafunga kulisha masikini..

4.mgonjwa ambaye ugonjwa wake hautarajiwi kupona hukumu yake ni sawa na ya wazee au vikongwe.

5.Mwenye mimba na mwenye unyonyesha.
,as-aa hii ni katika mas-al zeny utata sana kwa maulamaa. wapo waosema akifungua mweny mimba au menye kunyonyesha kwa kuhofia afya ya mototo aidha kutopata maziwa au kudhoofu kwa afya ya mtoto aliyepo tumboni basi hapa hukumu ni kufungua na kulisha masikni kwa kila siku ambayo hatafunga. Na itawalazimu baadaye kujalipa. A ikitoea hawakufunga kwa ajili ya kuhofia afya zao kua kama watafunga huenda wkaumwa basihapa hukumu ni kutofunga ila itawalazimu kujalipa badae bila ya ulisha masiini.

Baada ya uchamuzi wa kina juu ya hadthi mbalimbali maulamaa wengine wameona watu hawa wnaruhuswa kufungua na watalisha masikini kwa kila sikuambayo haakufunga na hakuna haja ya kuja kulipa. Na huu ndio msimamo wenye nguvu zaidi. Na masahaba wengi walikuwa wakiamini hivi akiwemo Ibn ‘Abas na Ibn ‘umar.

Maulamaa hawa wanatoa hoja hizi:-
1.amesema Ibn Abas kuwa (hadithi ni ndefu ila ndani yake akasema ) “….mwenye mimba au mwenye kunyonyesha watakapohofia watalisha kila siku makisini” (hadithi hii ni sahihi na ameipokea Bayhaqiy).

2.Amesimulia Nafi’i kuwa ….alikuwepo binti mmoja mwenye mimba na akapiga chafya katika mwezi wa ramadhani basi Ibn ‘Umar akamuamrisha afungue na badala yake alishe katika kila siku masikini” (hadithi hii ni sahihi na ameipokea Drqutniy)

2.watu ambao ni wajibu kufungua na wanatakiwa walipe.
1.Hawa ni watu aina mbili nao ni wenye heddhi au nifasi. Hawa ni lazima kufungua na watalipa siku hizi baada ya ramadhani na kabla ya kuingia ramadhani nyingine. Na akitwaharika mwanamke ndani ya mchana wa ramadhani ataendelea na kula kwake. Na akitwaharika kabla ya alfajiri na akawa ametia niya ya kufunga itasihi funga yake na ijapo atachelewa kuoga. Mtu mwenye damu ya ugonjwa ataendelea kufunga.

2.Kwenye kuhofia maangamivu kwa kufunga. Yaani pindi akiwa mtu katika hali ambayo akifunga huenda akafariki au kupata matatizo makubwa sana basi mtu huyu ni wajubu kwake kufungua.

3.ambao haijuzi kufungua
Ni kila muislamu aliye balehe na kuwa na akili timamu, mkazi wa mji na asiwe mgonjwa.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 150


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Hatua za kinga za ugumba na Utasa.
Ugumba ni “ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasa  kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba. Soma Zaidi...

hizi ndizo sharti za swala
Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

Utaratibu wa kutekeleza hija, matendo hatua kwa hatua, pamoja na kusherehekea sikuku baada ya hija
4. Soma Zaidi...

IBADA YA HIJA NA NAMNA YA KUITEKELEZA
Soma Zaidi...

Swala ya jamaa na mnamna ya kuswali swala ya jamaa, nyumbni, msikitini na kwa wanawake
Soma Zaidi...

Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya kusimamisha swala
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

taratibu na namna ya kutaliki, na mambo ya kuzingatia
Taratibu za Kutaliki KiislamuKama palivyo na taratibu za kuoa Kiislamu ndivyo hivyo pia ilivyo katika kuvunja ndoa. Soma Zaidi...

Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali
Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali. Soma Zaidi...

Zijuwe aina kuu 6 za talaka katika uislamu
Talaka zimegawanyika katika makundi mengi. Katika somo hili utakwenda kukifunza aina kuu za talaka katika uislamu. Soma Zaidi...

Tathmini ya swala zetu, kwa nini swala zetu hazijibiwi?
Soma Zaidi...