Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Riba na Madhara Yake Katika Jamii

Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
Rejea Qur’an (2:275-276)



Uharamu wa Riba

i. Uislamu umeharamisha riba kwa sababu ni dhulma (unyonyaji) kwa mnyonge mwenye dhiki aliyekopa ili kukidhi haja ya msingi kimaisha.


ii. Riba inahamisha mali na rasilimali kutoka kwa maskini au wanyonge kwenda kwa matajiri.

iii. Riba huondoa usawa na uadilifu katika kugawa na kutumia mali na rasilimali baina ya maskini au wanyonge na matajiri.

iv. Riba imeharamishwa kwa sababu huleta maisha ya kivivu na kutowajibika kwa matajiri, kuchuma bila jasho lolote.

v. Riba ina sababisha watu maskini na wanyonge wabakie kuishi kidhalili kwa kuwatumikia matajiri tu.

vi. Riba husababisha uchumi kuzorota kwa kumikiwa na watu wachache au vyombo kama mabenki, bima, kwa mfumo wa riba.



Madhara ya Riba Katika Jamii

i. Riba inachafua nafsi ya tajiri, kwa kuwa bahili, mchoyo asiyetayari kuwasaidia maskini, wanyonge na wenye shida mpaka bila malipo yeyote ya ziada.


ii. Riba huchafua mali ya tajiri kutokana na njia haramu za kuchuma na kumiliki bila kuzingatia mipaka.

iii. Riba inakandamiza wanyonge, maskini na wenye dhiki na matatizo, wenye kuhitajia misaada ili waweze kuishi.

iv. Riba inaharibu uchumi na maendeleo ya jamii kwa kudhulumu kundi la maskini na kufaidisha kundi la matajiri.

v. Riba inahamisha uchumi, mali na rasilimali kutoka kwa maskini na wanyonge kwenda kwa matajiri.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1676

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana: