Kumuandaa maiti punde baada ya kufariki dunia

Kumuandaa maiti punde baada ya kufariki dunia

Mambo Anayofanyiwa Mtu mara tu baada ya Kufa



Baada ya kushuhudia kuwa ndugu yetu ameshakata roho vyema tuseme na kuzingatia maneno yafuatayo kama alivyotufahamisha Allah (s.w)
โ€œ... Hakika sisi ni wa Allah na kwake tutarejea ...โ€ (2:156).



Maneno haya ni ya msingi sana katika hali hii ya kufiwa, kwani yanawaliwaza wafiwa na kuwaepusha na fadhaa zinazoweza kutokea juu ya kifo cha marehemu. Ukizingatia maneno ya aya hii utaona kuwa kwa vyovyote iwavyo, kurejea kwa Allah ni jambo lisilozuilika. Hivyo, chochote kile kitakachokuwa ndio sababu ya kifo cha marehemu kitakuwa ni sababu tu ya kifo hicho aliyoiweka Allah (s.w)



Baada ya maliwazo haya maiti ile yapasa kufanyiwa yafuatayo:


1. Kwa taratibu rudishia mdomo usibakie wazi kwa kufunga kidevu kwa kitambaa na kukizungushia kichwani.



2. Funga macho ya marehemu kwa taratibu na huku ukisoma:



โ€œKwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah. Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake baadaye. Na jaalia atakayokutana nayo yawe bora kuliko aliyoachana nayoโ€.



3. Lainisha viungo vya maiti kwa kukunja na kukunjua pole pole sehemu zote zenye viungo katika mikono na miguu. Kama patakuwa na ugumu wowote katika kumnyoosha viungo hivyo, maji ya moto au mafuta yanaweza kutumika ili kulainisha. Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na alazwe huku uso ukielekea Qibla kwenye kitanda kisichokuwa na godoro.



4. Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo kisha kumgubikwa kwa shuka kubwa, pia ni vyema afungwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu chenye uzito kidogo juu ya tumbo ili lisifutuke sana.



5. Marashi na ubani vitumike sana mahali alipo maiti ili kuzima harufu ya uvundo itokayo kwa maiti.Mwanaadamu ni msafi sana anapokuwa hai. Lakini muda mfupi tu baada ya kufa huanza kutoa harufu kali ya uozo.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1328

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 web hosting    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii.

Soma Zaidi...
Hatua za kinga za ugumba na Utasa.

Ugumba ni รขโ‚ฌล“ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasaร‚ย  kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.

Soma Zaidi...
Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?

Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi?

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya swala

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoweza kutoa udhu wako

Post hii itakufundisha mambo ambayo yanabatilisha udhu.

Soma Zaidi...
Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia

Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.

Soma Zaidi...
Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu.

Soma Zaidi...
Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii

Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...