Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

(i)Dai kuwa Qur-an ni Mashairi aliyotunga Muhammad (s.

Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

(i)Dai kuwa Qur-an ni Mashairi aliyotunga Muhammad (s.a.w):



Dai hili lilitolewa na Makuraishi katika enzi hizo za kushuka kwa Qur-an pia linaendelea kutolewa na makafiri wa karne hizi. Kwa mfano Stober, baada ya kusoma tafsiri ya Qur-an alidai kuwa itakuwa imeandikwa na Mwarabu ambaye ni mweledi wa historia ya Mayahudi na mila za nchi yake ambaye pia ni mshairi mzuri.
Udhaifu:



Wasomaji wa mashairi ya Kiarabu wanafahamu kuwa mashairi hayo yana mizani,beti na vina na yanaimbika kwa kiasi kwamba wakati mwingine inabidi hata maana au sarufi viwekwe pembeni alimradi tu shairi liimbike. Hivi sivyo kabisa ulivyo mfumo wa Qur-an. Qur-an si mashairi bali ni ujumbe wenye maana kamili ulioandikwa katika fasihi ya hali ya juu kwa kuzingatia sarufi na miiko yote ya lugha hai


.
Historia imeshuhudia kuwa Qur-an si mashairi. Ilikuwa kawaida ya washairi wakati ule wa Mtume (s.a.w) kubandika mashairi yao kwenye mlango wa Ka'aba kama changa-moto kwa washairi wengine. Ilitokea siku moja mshairi mashuhuri wa wakati huo, Labbiib ibn Rabiah, akabandika shairi lake kwenye mlango wa Ka'aba ili kutoa changamoto kwa washairi wengine. Shairi lake lilikuwa limetungwa kwa utaalamu mkubwa sana na lilikuwa zuri mno kiasi cha kutothubutu mtu yeyote kupambanisha shairi lake na hilo. Lakini baada ya kubandikwa kipande cha Sura ya Qur-an karibu na shairi lake, Labbiid mwenyewe (ambaye alikuwa Mshirikina) baada ya kusoma mistari michache ya sura hiyo alinaswa na mvuto wake na kuiamini dini iliyofunuliwa kutoka kwa Allah (s.w) na kubandua shairi lake




                   


Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1400

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

HUKUMU ZA IDGHAM
HUKUMU ZA IDGHAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Mauun
Sababu za kushuka surat al Mauun

Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat at Takaathur
Sababu za kushuka surat at Takaathur

Kuwa na tamaa huhitaji vitu vya watu si jambo jema. Ila kama tamaa hii itakuhamasisha na wewe kutafuta kitu hicho, kwa uwezo ambao Allah amekupa bila ha kuvuka mipaka yake, hili sio tatizo. Sura hii itakufundisha mengi

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)
Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)

Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al humazah
Sababu za kushuka surat al humazah

Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka.

Soma Zaidi...
Saratul-humaza
Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
 Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum
Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum

SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.

Soma Zaidi...