Kuwa na tamaa huhitaji vitu vya watu si jambo jema. Ila kama tamaa hii itakuhamasisha na wewe kutafuta kitu hicho, kwa uwezo ambao Allah amekupa bila ha kuvuka mipaka yake, hili sio tatizo. Sura hii itakufundisha mengi
SURAT AT-TAKAATHUR
Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii ilishuka Makka. Imam Bukhari anaeleza ya kuwa ilishuka Madina. Lakini sahaba mmoja, Ibni Abbas, anasema ya kuwa ilishuka Makka. Neno Takaathur anasema Ibn Abbas maana yake ni tamaa nyingi ya mali na watoto (Bukhari). Abu Huraira anasimulia ya kuwa Mtume s.a.w. aliposoma sura hii alisema, "Mwanadamu anasema, hii ni mali yangu, hii ni mali yangu. Kumbe aliyokula na kuvaa ameichakaza, aliyotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, ndiyo kaiweka akiba na iliyobaki si yake ni mali ya watu."
Sababu za kushuka sura hii:-
Muqatil na Al-Kalb wamesema “sura hii ilishuka kutokana na makabila mawili ya Kikurayshi, ambayo ni Banu Abd Manafi na Banu Sahm. Kila kabila lilikuwa likijisifu na kujigamba juu ya lingine. Hivyo ikafikia hadi wakaanza kuheabu ni kabila lipi lina machifu wengi na viongozi wengi kuliko lingine. Banu Abd Manafi walikuwa wakisema “sisi tuna machifu wengi, viongozi wengi na hata kabila letu lina watu wengi”. pia banu Sahm walikuwa wakisema hivyohivyo. Basi baada ya kuhesabu ikaonekana kweli Banu Abd Manafi wana watu wengi kwenye kabila lao. Baada ha yapo wakasema “twendeni tukahesabu makaburi ya watu wetu waliokufa. Hivyo wakayaendea makaburi hapo wakaata jibu kuwa Banu Saham ni wengi waliokufa kuliko Banu Abd Manafi.
Qatada amesema kuwa sura hii ilishuka kuwahusu Mayahudi waliosema “sisi ni wengi ssana kuliko wakina fulani na fulani ….., hivyo walikuwa wakiendelea na madai yao haya na kujisahau, kumuasi mungu hadi mauti anawafikia.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.
Soma Zaidi...Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.
Soma Zaidi...Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.
Soma Zaidi...Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo
Soma Zaidi...Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani
Soma Zaidi...Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto.
Soma Zaidi...FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.
Soma Zaidi...Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.
Soma Zaidi...